Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Jicho Lako Ni “Rahisi”?
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Mei 1
    • 9. Shetani anatiaje moyo leo watu wawe na “tamaa ya macho”?

      9 Leo, Shetani bado anatumia njia ile ile katika mipango yake ya kuvuta watu wote waache kufanya mapenzi ya Mungu. Kwa kutumia umeremeti na marembo ya ulimwengu, Shetani anaendeleza “tamaa ya mwili na tamaa ya macho na kujionyesha kwa mtu mali yake.” (1 Yohana 2:16, NW ) Jambo hilo linaonekana wazi katika mipango ya utangazaji wa bidhaa inayotumiwa na ulimwengu wa kibiashara. Je, si kweli kwamba matangazo ya bidhaa yaliyo na mafanikio makubwa zaidi ni yale yanayotumia uwezo mwingi wa kuvutia macho? Yale maelfu ya matangazo ya bidhaa yenye rangi-rangi na ishara zinazowaka-waka kwa njia ya kupendeza, zile picha zenye rangi nyingi katika magazeti, miwako-wako ya werevu sana katika televisheni—na mabilioni ya shilingi zinazotumiwa kuyatokeza—yote yanashuhudia kwamba kusudi la utangazaji bidhaa ni kusisimua “tamaa ya macho” ya wanunuzi.

      10. Kwa kweli ulimwengu wa kibiashara unatia moyo jambo gani?

      10 Ingawa mengi ya matangazo hayo hayamwachii mtu nafasi ya kufikiri vizuri, jambo lililo la ujanja zaidi ni kwamba matangazo hayo ya kibiashara hayawi yakitia moyo ununuzi wa bidhaa tu bali pia ufuataji wa mitindo. Mara nyingi sana bidhaa hizo zinaonyeshwa kuwa zikitumiwa na watu walio na mapendeleo makubwa zaidi, walio mashuhuri zaidi, wenye furaha zaidi, na walio warembo zaidi. Ujumbe wa matangazo hayo ni kwamba mnunuzi akitumia bidhaa hiyo, njia yake ya maisha itaonyesha wazi yeye ni mmoja wa watu hao mashuhuri. Watangazaji wanajua kwamba mtu akiisha kukubali namna fulani ya maisha, si vigumu sana kumshawishi akubali bidhaa na vitu vinavyoambatana nayo. Basi, jinsi lilivyo jambo la hekima Wakristo walio wakfu kutii shauri linalopatikana kwenye Waebrania 13:5! Hapo tunasoma hivi: “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo.”

  • Je, Jicho Lako Ni “Rahisi”?
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Mei 1
    • 15, 16. (a) Ni “tamaa ya macho” gani nyingine ambayo ni lazima tuiepuke? (b) Wewe ungelitumiaje shauri lililo katika Mithali 27:20 kuhusu mazungumzo yetu?

      15 Lakini, je, ni wale tu wanaoweka jicho lao juu ya kuwa matajiri wanaokabiliwa na hatari ya kutembea katika giza? Hapana, kwa maana “tamaa ya macho” inatia ndani pia mambo mengine mengi. Yakumbuke maneno ya Yesu kwenye Mathayo 5:28: “Kila mtu anayeendelea kutazama mwanamke ili awe na nyege kwa ajili yake amekwisha kufanya uzinzi pamoja naye katika moyo wake.” (NW ) Kwa hakika onyo hilo linaweza kutumiwa pia juu ya mtu kuachilia macho yake yaendelee kuangalia habari ambazo zimebuniwa ili kusisimua au kuamsha nyege na tamaa zisizofaa.

      16 Halafu Yesu alisema juu ya mahangaikio kuhusu chakula, vinywaji, na mavazi. (Mathayo 6:25-32) Ingawa vitu hivyo vinahitajiwa, tamaa inayopita kiasi ya kutaka kuwa na vilivyo wa karibuni zaidi, vilivyo vya utajiri mwingi zaidi, vinavyotafutwa na watu wengi zaidi, inaweza kutumikisha akili na moyo wetu. (Warumi 16:18; Wafilipi 3:19) Hata katika tafrija, shughuli tunazofanya wakati wa starehe, michezo, mazoezi, na kadhalika, inatupasa tudumishe usawaziko unaofaa na kujilinda tusije tukanaswa katika mitindo na visisimuaji vya ulimwengu. Katika maeneo haya yote, ingekuwa vizuri tuyazingatie maneno yenye hekima yanayopatikana kwenye Mithali 27:20, New World: “Sheoli na mahali pa uharibifu wenyewe havitosheki; wala “macho ya mwanadamu hayatosheki.” Kwa kweli, tunahitaji kujizoeza kujiweza ili hali yetu ya kiroho isihatirishwe tunapojaribu kuyatosheleza macho yetu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki