-
Endelea Kutembea Katika Nuru ya KimunguMnara wa Mlinzi—1986 | Julai 15
-
-
16. Ni upendo gani ambao ni lazima tusiwe nao, lakini ni jambo gani lingekuwa kweli juu yetu kama tungekuwa na maoni na tamaa za makuu ya kilimwengu?
16 Kama sisi ni wenye umri mdogo au mkubwa katika kuwa Wakristo, kuna upendo ambao ni lazima tusiwe nao. (Soma 1 Yohana 2:15-17 NW.) Ni lazima ‘tusiupende ulimwengu wala cho chote kilichomo.’ Bali, tunahitaji kuepuka kutiwa doa na ufisadi wa jamii ya kibinadamu isiyo na uadilifu na ni lazima tusipumue “roho” yao, au kusukumwa na mwelekeo wao mkuu wenye dhambi. (Waefeso 2:1,2, NW; Yakobo 1:27) Kama tungekuwa na maoni na tamaa za kujitakia makuu ya kilimwengu, “upendo wa Baba” haungekuwa ndani yetu. (Yakobo 4:4) Hilo ni jambo linalopasa kufikiriwa katika sala kweli kweli, sivyo?
-
-
Endelea Kutembea Katika Nuru ya KimunguMnara wa Mlinzi—1986 | Julai 15
-
-
19. Ni jambo gani litakaloupata ulimwengu huu, nalo linapasa liwe na matokeo gani juu yetu?
19 Kumbuka kwamba “ulimwengu unapita” na utaharibiwa. (2 Petro 3:6) Tamaa na matumaini yao zitaangamia pamoja nao, hali moja na watu mmoja mmoja wanaoupenda. “Lakini,” anasema Yohana “yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anabaki milele.” Kwa hiyo acheni tuendelee kuutazama uzima wa milele kwa ‘kuzikataa kabisa tamaa za kilimwengu’ na kuendelea kutembea katika nuru ya kimungu.—Tito 2:11-14, NW.
-