Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Endelea Kutembea Katika Nuru ya Kimungu
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Julai 15
    • 24. Ni nani wanaokuwa na “upakwa-mafuta” kwa roho takatifu, na kwa sababu gani ‘hawahitaji mtu ye yote kuwafundisha’?

      24 Ili tutembee katika nuru ya kimungu na tusipotezwe na waasi-imani, tunahitaji maagizo ya kiroho yanayofaa. (Soma 1 Yohana 2:26-29, NW.) Waliozaliwa kwa roho wana “upakwa-mafuta” kwa roho takatifu, wamepata kumjua Mungu na Mwana wake na ‘hawahitaji mtu ye yote [mwasi-imani] awe akiwafundisha.’ Kwa roho yake yenye kupaka mafuta, Mungu ‘anafundisha’ Waisraeli wa kiroho “juu ya mambo yote” yanayohitajiwa ili kumwabudu kwa njia inayokubalika. (Yohana 4:23, 24; 6:45) Sisi tunafurahi sana kwamba tukiwa Mashahidi wa Yehova tunapokea maagizo hayo ya kiroho kutoka kwa Mungu kupitia kwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili.”—Mathayo 24:45-47.

  • Endelea Kutembea Katika Nuru ya Kimungu
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Julai 15
    • 26 Kwa kuwa sasa tunaishi katika wakati wa “kuwapo” kwa Yesu, tunaweza kuhakikishaji kwamba hatuna jambo la kuaibikia na kwamba tunatembea kweli kweli katika nuru ya kimungu? Ni kwa ‘kuzoea uadilifu.’ ‘Tukijuwa kwamba Mungu ni mwadilifu,’ Yohana anafikiri kwa kutoa sababu, ‘tunakuwa macho kwamba kila mmoja anayezoea uadilifu amezaliwa kutoka kwake.’ ‘Kuzoea uadilifu’ kunamaanisha kutii amri za Mungu, kuepuka ukosefu wa uadilifu, na kujitia katika kazi nzuri kama vile kufanya wanafunzi na kusaidia waamini wenzetu. (Marko 13:10; Wafilipi 4:14-19; 1 Timotheo 6:17, 18) ‘Kuzaliwa kutoka kwa’ Mungu kunamaanisha ‘kuzaliwa mara ya pili’ kama watoto wake wa kiroho.—Yohana 3:3-8

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki