-
Ukitenda Dhambi Nzito Unapaswa Kufanya Nini?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
4. Yehova anawaonyesha rehema watenda dhambi
Mtu ambaye ametenda dhambi nzito akikataa kufuata viwango vya Yehova, ataondolewa kutanikoni na hatutashirikiana naye. Soma 1 Wakorintho 5:6, 11, na kisha mzungumzie swali hili:
Kama vile chachu inavyochachisha donge lote la mkate, kushirikiana na mtenda dhambi asiyetubu kunawezaje kuathiri kutaniko?
Wakiiga rehema ya Yehova kuelekea wanadamu watenda dhambi, wazee huwatafuta na kuwasaidia wale walioondolewa kutanikoni. Ingawa nidhamu waliyopokea ilikuwa na maumivu, iliwasaidia kutambua uzito wa makosa yao na wengi wamerudi kutanikoni.—Zaburi 141:5.
Yehova anaonyeshaje kwamba ni mwenye usawaziko, rehema, na upendo kupitia jinsi anavyoshughulika na watenda dhambi?
5. Yehova hutusamehe tunapotubu
Yesu alitumia mfano unaotusaidia kuelewa jinsi Yehova anavyohisi mtu anapotubu. Soma Luka 15:1-7, kisha mzungumzie swali hili:
Simulizi hili linakufundisha nini kumhusu Yehova?
Soma Ezekieli 33:11, kisha mzungumzie swali hili:
-
-
Endelea Kuwa Mshikamanifu kwa YehovaFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
1. Wengine wanawezaje kufanya iwe vigumu kwetu kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova?
Watu fulani watajaribu kutushawishi tuache kumtumikia Yehova. Je, kuna watu wanaoweza kufanya jambo baya hivyo? Baadhi ya watu ambao wameacha kumtumikia Yehova, wanaeneza uwongo kuhusu tengenezo la Mungu ili kuharibu imani yetu. Watu hao wanaitwa waasi-imani. Pia, baadhi ya viongozi wa dini hueneza uwongo kutuhusu ili kuwafanya watu wasio waangalifu waache kumtumikia Yehova. Ni hatari kubishana na watu wanaotupinga, kusoma vitabu na mijadala yao kwenye mitandao, kutembelea tovuti zao, au kutazama video zao. Yesu alisema hivi kuhusu wale wanaojaribu kuwavunja moyo wengine waache kuwa washikamanifu kwa Yehova: “Waacheni. Wao ni viongozi vipofu. Basi, kipofu akimwongoza kipofu, wote wawili watatumbukia ndani ya shimo.”—Mathayo 15:14.
2. Ni maamuzi gani yanayoweza kuonyesha kwamba sisi ni washikamanifu kwa Yehova?
Upendo wetu kwa Yehova utatuchochea kuepuka kushirikiana kwa njia yoyote na dini za uwongo. Hatupaswi kufanya kazi au kushirikiana na shirika lolote la kidini wala kujihusisha na shughuli zozote zinazohusiana na dini za uwongo. Yehova anatuonya hivi: “Tokeni [katika Babiloni Mkubwa], watu wangu.”—Ufunuo 18:2, 4.
CHIMBA ZAIDI
Jifunze jinsi unavyoweza kuepuka kumruhusu mtu yeyote avunje ushikamanifu wako kwa Yehova. Pia, chunguza jinsi unavyoweza kuonyesha kwamba wewe ni mshikamanifu kwa kujitenga na Babiloni Mkubwa.
3. Jihadhari na walimu wa uwongo
Tunapaswa kutendaje tunaposikia habari zisizofaa kuhusu tengenezo la Yehova? Soma Methali 14:15, kisha mzungumzie swali hili:
Kwa nini hatupaswi kuwa wepesi kuamini kila jambo tunalosikia?
Soma 2 Yohana 9-11, kisha mzungumzie maswali haya:
Tunapaswa kuwatendeaje waasi-imani?
Mbali na kuepuka kushirikiana na waasi-imani moja kwa moja, ni mambo gani mengine tunayopaswa kuepuka ili tusishawishiwe na mafundisho yao?
Unafikiri Yehova atahisije ikiwa tutasikiliza mambo yasiyofaa yanayosemwa kumhusu au kuhusu tengenezo lake?
4. Uwe mshikamanifu kwa Mungu, Mkristo mwenzako anapotenda dhambi
-