Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Gayo Alivyowasaidia Ndugu Zake
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Mei
    • Huenda wageni hao walikuwa wamishonari, wajumbe wa Yohana, au waangalizi wanaosafiri. Vyovyote vile, walisafiri ili waeneze habari njema. Yohana alisema hivi: “Walisafiri kwa ajili ya jina lake.” (3 Yoh. 7) Yohana alikuwa ametoka tu kumtaja Mungu (tazama mstari wa 6), kwa hiyo inaonekana maneno “kwa ajili ya jina lake” yanarejelea jina Yehova. Hivyo, ndugu hao walikuwa sehemu ya kutaniko la Kikristo na walistahili kukaribishwa kwa uchangamfu. Ni kama Yohana alivyoandika: “Sisi tuna wajibu wa kuwakaribisha watu wa namna hiyo, ili tuwe wafanyakazi wenzi katika kweli.”—3 Yoh. 8.

  • Jinsi Gayo Alivyowasaidia Ndugu Zake
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Mei
    • Kwanza, huenda wengi wetu tumepata ujuzi wa kweli kupitia waaminifu ambao walikuwa tayari kusafiri ili kutufundisha Biblia. Ni kweli kwamba si washiriki wote wa kutaniko la Kikristo leo wanaosafiri mbali ili kueneza habari njema. Hata hivyo, kama Gayo, kwa njia moja ama nyingine tunaweza kuwategemeza na kuwatia moyo wale wanaosafiri, kama vile mwangalizi wa mzunguko na mke wake. Au tunaweza kuwategemeza ndugu na dada wanaohamia maeneo yenye uhitaji mkubwa wa wahubiri wa Ufalme katika nchi yao, au hata nje ya nchi. Kwa hiyo, acheni “[tufuate] mwendo wa ukaribishaji-wageni.”—Rom. 12:13; 1 Tim. 5:9, 10.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki