-
Ukaribishaji-Wageni wa Kikristo Katika Ulimwengu UliogawanyikaMnara wa Mlinzi—1996 | Oktoba 1
-
-
“Kwa hiyo, sisi, tuko chini ya wajibu wa kuwapokea watu wa namna hiyo kwa ukaribishaji-wageni, ili tupate kuwa wafanyakazi wenzi katika kweli.”—3 YOHANA 8, NW.
-
-
Ukaribishaji-Wageni wa Kikristo Katika Ulimwengu UliogawanyikaMnara wa Mlinzi—1996 | Oktoba 1
-
-
3. Twaweza kupataje shangwe na uradhi wa kweli?
3 Jinsi mambo yangekuwa tofauti ikiwa watu wangeiga njia ya Yehova ya kushughulika na wengine—kuwa wenye fadhili, wenye ukarimu, na wakaribishaji-wageni! Alijulisha wazi kwamba siri ya kupata furaha ya kweli haimo katika kujaribu kwetu kuridhisha tamaa zetu wenyewe. Bali, huu ndio ufunguo: “Ni heri kutoa kuliko kupokea.” (Matendo 20:35) Ili kupata shangwe na uradhi wa kweli, lazima tushinde vizuizi na migawanyiko iwezayo kutuwekea mipaka. Na lazima tuwafikie wale wanaomtumikia Yehova pamoja nasi. Ni muhimu tutii shauri hili: “Kwa hiyo, sisi, tuko chini ya wajibu wa kuwapokea watu wa namna hiyo kwa ukaribishaji-wageni, ili tupate kuwa wafanyakazi wenzi katika kweli.” (3 Yohana 8, NW) Kuonyesha ukaribishaji-wageni kwa wanaostahili, kwa kadiri hali zetu zinavyoruhusu, kuna faida katika njia mbili—hufaidi watoaji pamoja na wapokeaji. Ni nani basi, walio miongoni mwa wanaostahili tupaswao ‘kuwapokea kwa ukaribishaji-wageni’?
-