-
Jinsi Gayo Alivyowasaidia Ndugu ZakeMnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Mei
-
-
MSAADA KUHUSU HALI FULANI NGUMU
Yohana hakumwandikia Gayo ili kumshukuru tu. Alitaka pia kumsaidia ashughulikie tatizo fulani zito. Kwa sababu fulani, mshiriki mmoja wa kutaniko la Kikristo aliyeitwa Diotrefe hakutaka kuwaonyesha ukarimu waangalizi wanaosafiri. Hata alijaribu kuwazuia wengine wasionyeshe ukarimu. —3 Yoh. 9, 10.
Hapana shaka kwamba Wakristo waaminifu hawangependa kuishi na Diotrefe hata ikiwa wangeweza kufanya hivyo. Alipenda kuwa na mahali pa kwanza kutanikoni, hakupokea kwa heshima jambo lolote kutoka kwa Yohana, na alipiga porojo kuhusu mtume huyo na wengine. Ingawa Yohana hakuwahi kumwita mwalimu wa uwongo, Diotrefe alipinga mamlaka yake. Tamaa ya Diotrefe ya kujitafutia makuu na mtazamo wake usio wa Kikristo ulifanya ushikamanifu wake utiliwe shaka. Kisa cha Diotrefe kinaonyesha roho ya mgawanyiko ambayo watu wenye kujitafutia makuu na wenye majivuno wanaweza kuleta kutanikoni. Kwa hiyo, Yohana alimwambia Gayo maneno haya ambayo pia yanahusu kila mmoja wetu: “Uwe mwigaji, si wa yaliyo mabaya.”—3 Yoh. 11.
-
-
Jinsi Gayo Alivyowasaidia Ndugu ZakeMnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Mei
-
-
Pili, hatupaswi kushangaa ikiwa kwa nadra watu fulani wanapinga mamlaka kutanikoni leo. Mamlaka ya Yohana ilipingwa na vilevile mamlaka ya mtume Paulo. (2 Kor. 10:7-12; 12:11-13) Hivyo basi, tunapaswa kutendaje tunapokabili hali kama hiyo kutoka kwa baadhi ya watu kutanikoni? Paulo alimshauri hivi Timotheo: “Mtumwa wa Bwana hahitaji kupigana, bali anahitaji kuwa mpole kwa wote, mwenye sifa za kustahili kufundisha, akiendelea kujizuia chini ya uovu, akiwafundisha kwa upole wale wasio na mwelekeo unaofaa.” Tunapodumisha upole hata tunapochokozwa, huenda watu fulani wanaochambua mamlaka wakabadili mtazamo wao. Na huenda Yehova “akawapa toba inayoongoza kwenye ujuzi sahihi juu ya kweli.”—2 Tim. 2:24, 25.
-