-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1988 | Juni 1
-
-
Maelezo yenye maana zaidi yanapatikana kwenye Yuda 7. Yuda alikuwa tu amezungumza juu ya (1) Waisraeli walioangamizwa kwa ukosefu wa imani, na (2) malaika waliotenda dhambi na ‘wamewekwa katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.’ Kisha Yuda akaandika: ‘Kama vile Sodoma na Gomora, . . . imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.” Andiko hili linarejeza kwenye majiji halisi yaliyoharibiwa milele, si watu. Hata hivyo, kwa sababu ya Yuda 5 na 6, inaelekea kwamba watu walio wengi wangeuchukua mstari wa 7 kumaanisha adhabu ya hukumu ya watu mmoja mmoja. (Vivyo hivyo, Mathayo 11:20-24 ingeeleweka kuwa yenye kuwachambua watu, si mawe wala majengo.) Hivyo, Yuda 7 ingemaanisha kwamba watu waovu wa Sodoma/Gomora walihukumiwa na kuharibiwa milele.a
Tukiangalia mahali pengine, tunalipata kuwa jambo lenye kuangaliwa kwamba Biblia inafungamanisha Gharika na Sodoma/Gomora zaidi ya mara moja. Katika maana gani ya mistari inayozunguka?
Alipoulizwa juu ya “umalizio wa mfumo wa mambo,” Yesu alitabiri juu ya “mwisho” unaokuja na “dhiki kubwa ambayo haijatokea tangu mwanzo wa ulimwengu.” (Mathayo 24:3, 14, 21, NW) Aliendelea kusema juu ya “siku za Noa” na yale “yaliyotukia katika siku za Loti” kama vielelezo vya watu ambao hawakujali onyo juu ya uharibifu uliokuwa ukija. Yesu aliongezea hivi: “Ndivyo itakavyokuwa katika siku ile ambapo Mwana wa mwanadamu atakapofunuliwa.” (Luka 17:26-30, NW; linganisha Mathayo 24:36-39.) Je! Yesu alikuwa akitoa kielezi cha mwelekeo tu, au je! mistari inayozunguka ambayo katika hiyo yeye alitumia vielelezo hivi inadokeza kwamba hukumu za milele zilihusika?
Baadaye, Petro aliandika juu ya hukumu za Mungu na kuwaadhibu Kwake wale wanaostahili. Kisha Petro akatumia vielelezo vitatu: Malaika waliotenda dhambi, ulimwengu wa kale wa siku ya Noa, na wale walioharibiwa katika Sodoma na Gomora. Petro alisema hivi kwa habari ya kile cha mwisho, ‘akiweka kiolezo kwa ajili ya watu wasiomwogopa Mungu cha mambo yatakayokuja.’ (2 Petro 2:4-9, NW) Baada ya hapo, alilinganisha uharibifu ambao watu walipatwa nao katika Gharika na “siku ya hukumu na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu” inayokuja. Huo unatangulia mbingu mpya na dunia mpya iliyoahidiwa,—2 Petro 3:5-13.
Vivyo hivyo, mwishoni mwa mfumo huu mbovu wa mambo, je! wale ambao Mungu ataua watakuwa wamepata hukumu ya hatima? Hilo ndilo jambo ambalo 2 Wathesalonike 1:6-9 linaonyesha: “Ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi; na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake; katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu; watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake.”
Kuna ulinganifu wenye kupendeza katika nahau kati ya maelezo haya na kile ambacho Yuda alisema kwamba kilitukia kwa habari ya Sodoma. Zaidi ya hilo, Mathayo 25:31-46 na Ufunuo 19:11-21 unaonyesha kwamba “mbuzi” wanaokatiliwa mbali katika vita ya Mungu inayokuja “watakatiliwa milele” katika “ziwa la moto,” linalofananisha kuangamizwa daima.b—Ufunuo 20:10, 14.
Kwa sababu hiyo, kuongezea yale ambayo Yuda 7 inasema, Biblia inatumia Sodoma/Gomora na Gharika kuwa violezo vya uharibifu wa mwisho wa mfumo huu mbovu. Basi, ni wazi kwamba, wale waliouawa na Mungu katika hukumu hizo za wakati uliopita walipatwa na uharibifu usioweza kubadilishwa tena. Bila shaka, kila mmoja wetu anaweza kuthibitisha hilo kwa kuendelea kwake kuwa mwaminifu kwa Yehova sasa. Katika njia hiyo tutastahili kuwa hai katika ulimwengu mpya ili tuone wale ambao yeye atafufua na wale ambao yeye hatafufua. Tunajua kwamba hukumu zake ni kamilifu. Elihu alituhakikishia hivi: “Mungu asidhaniwe kutenda udhalimu; wala Mwenyezi kufanya uovu.”—Ayubu 34:10, 12.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1988 | Juni 1
-
-
a Kwenye Ezekieli 16:53-55, NW, “Sodoma na miji yayo inayoitegemea” inatajwa, si kuhusiana na ufufuo, bali kwa njia ya mfano kuhusiana na Yerusalemu na binti zake. (Linganisha Ufunuo 11:8.) Ona pia Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) Juni 1, 1952, kurasa 337.
b Linganisha “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1, 1979 (Kiingereza).
-