-
Kufisha Babuloni MkubwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
11. Malaika wa Yehova anasema nini juu ya pembe kumi zilizo juu ya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu wa ufananisho?
11 Katika sura ya Ufunuo iliyotangulia, malaika, wa sita na wa saba walimimina mabakuli ya kasirani ya Mungu. Hivyo sisi tuliarifiwa kwamba wafalme wa dunia wanakusanywa kwenye vita ya Mungu kwenye Har–Magedoni na kwamba ‘Babuloni Mkubwa apaswa kukumbukwa katika mwono wa Mungu.’ (Ufunuo 16:1, 14, 19, NW) Sasa tutajifunza kirefu zaidi jinsi hukumu za Mungu juu ya hawa zitatekelezwa. Sikiliza tena malaika wa Yehova anaponena kwa Yohana. “Na pembe kumi ambazo wewe uliona humaanisha wafalme kumi, ambao bado kupokea ufalme, lakini wao hupokea mamlaka wakiwa wafalme saa moja pamoja na hayawani-mwitu. Hawa wana fikira moja, na hivyo wao humpa hayawani-mwitu nguvu na mamlaka yao. Hawa watapigana na Mwana-Kondoo, lakini, kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme, Mwana-Kondoo atashinda wao. Pia, wale wenye kuitwa na wachaguliwa na waaminifu pamoja na yeye watafanya hivyo.”—Ufunuo 17:12-14, NW.
-
-
Kufisha Babuloni MkubwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
13. Ni katika njia gani pembe kumi zina “fikira moja,” na hiyo huhakikisha mwelekeo gani kwa Mwana-Kondoo?
13 Leo, utukuzo wa taifa ndio mojapo kani zenye nguvu zaidi sana zinazosukuma pembe kumi hizi. Zina “fikira moja” kwa kuwa hizo zinataka kuhifadhi enzi zao za kitaifa badala ya kukubali Ufalme wa Mungu. Hilo ndilo lilikuwa kusudi lao katika kuchangia Ushirika wa Mataifa na tengenezo la Umoja wa Mataifa katika ile mara ya kwanza—kuhifadhi amani ya ulimwengu na hivyo kulinda salama kuwako kwazo. Mwelekeo kama huo unahakikisha kwamba pembe kumi zitapinga Mwana-Kondoo, “Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme,” kwa sababu Yehova amekusudia kwamba Ufalme wake chini ya Yesu Kristo hivi karibuni utachukua mahali pa falme hizi.—Danieli 7:13, 14; Mathayo 24:30; 25:31-33, 46.
-