Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jiji Kubwa Lateketezwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 22. (a) Sauti kutoka katika mbingu inasema nini? (b) Ni nini kilichoongoza kwenye mshangilio wa watu wa Mungu katika 537 K.W.K., na katika 1919?

      22 Maneno yanayofuata ya Yohana yanaelekeza kwenye utimizo zaidi wa kigezo cha kiunabii: “Na mimi nikasikia sauti nyingine kutoka katika mbingu ikisema: ‘Ondokeni katika yeye, watu wangu, ikiwa nyinyi hamtaki kushiriki pamoja na yeye katika madhambi yake, na ikiwa nyinyi hamtaki kupokea sehemu ya tauni zake.’” (Ufunuo 18:4, NW) Unabii wa anguko la Babuloni wa kale katika Maandiko ya Kiebrania unatia ndani pia amri ya Yehova kwa watu wake: “Kimbieni mtoke katikati ya Babuloni.” (Yeremia 50:8, 13, NW) Hali moja na hiyo, kwa sababu ya ukiwa unaokuja wa Babuloni Mkubwa, watu wa Mungu wanahimizwa sasa waponyoke. Katika 537 K.W.K. fursa ya kuponyoka kutoka Babuloni ilileta mshangilio mkubwa upande wa Waisraeli waaminifu. Katika njia iyo hiyo, kuachiliwa kwa watu wa Mungu kutoka utekwa wa Babuloni Mkubwa kuliongoza kwenye mshangilio upande wao. (Ufunuo 11:11, 12) Na tangu wakati huo mamilioni ya wengine yametii amri hiyo wakimbie.

  • Jiji Kubwa Lateketezwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 24. (a) Ni lazima watu wa Mungu wakimbie kutoka Babuloni Mkubwa ili waepuke nini? (b) Wale wanaoshindwa kukimbia kutoka katika Babuloni Mkubwa wanashiriki naye madhambi gani?

      24 Ni maneno yenye nguvu, hayo! Kwa hiyo tendo linatakwa. Yeremia alihimiza watu katika siku yake watende, akisema: “Kimbieni kutoka katikati ya Babuloni, . . . kwa maana ni wakati wa kisasi ambacho ni cha Yehova. Kuna tendeo ambalo yeye analipa kurudisha kwa yeye. Ondokeni katikati yake, O watu wangu, na kila mmoja aandalilie nafsi yake mponyoko kutoka kasirani yenye kuwaka ya Yehova.” (Yeremia 51:6, 45, NW) Katika njia kama hiyo, sauti kutoka katika mbingu inaonya watu wa Mungu leo wakimbie kutoka Babuloni Mkubwa ili wasipokee sehemu ya tauni zake. Hukumu za Yehova zilizo kama tauni juu ya ulimwengu huu, kutia na Babuloni Mkubwa, zinapigiwa mbiu sasa. (Ufunuo 8:1–9:21; 16:1-21) Watu wa Mungu wanahitaji kujitenga wenyewe na dini bandia ikiwa wao wenyewe hawataki kupatwa na tauni hizi na mwishowe kabisa wafe naye. Waaidha, kubaki ndani ya tengenezo hilo kungewafanya washiriki katika madhambi yake. Wao wangekuwa na hatia kama yeye ya uzinzi wa kiroho na ya kumwaga damu “ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.”—Ufunuo 18:24, NW; linga Waefeso 5:11; 1 Timotheo 5:22.

      25. Ni katika njia zipi watu wa Mungu waliondoka katika Babuloni wa kale?

      25 Ingawa hivyo, ni jinsi gani watu wa Mungu huondoka katika Babuloni Mkubwa? Katika kisa cha Babuloni wa kale, Wayahudi walikuwa sharti wafanye safari halisi kutoka katika jiji la Babuloni moja kwa moja hadi Bara la Ahadi. Lakini zaidi ya hilo lilihusika. Kiunabii Isaya aliambia Waisraeli hivi: “Geukeni mbali, geukeni mbali, ondokeni humo, msiguse kitu kisicho safi; ondokeni katikati yake, jitunzeni wenyewe safi, nyinyi ambao mnapeleka vyombo vya Yehova.” (Isaya 52:11, NW) Ndiyo, wao walipaswa waache mazoea yote yasiyo safi ya dini ya Kibabuloni ambayo yangeelekea kuitia kutu ibada yao kwa Yehova.

      26. Wakristo Wakorintho walitiije maneno haya, ‘Ondokeni kutoka miongoni mwao na mwache kabisa kugusa kitu kisicho safi’?

      26 Mtume Paulo alinukuu maneno ya Isaya katika barua yake kwa Wakorintho, akisema: “Msipate kuwa wenye kufungiwa nira isivyofaa pamoja na wasioitikadi. Kwa maana ni ushirika gani uadilifu unao pamoja na ukosefu wa kutii sheria? Au ni hisa gani nuru inayo pamoja na giza? . . . ‘Kwa hiyo ondokeni kutoka miongoni mwao, na kujitenga nyinyi wenyewe,’ asema Yehova, ‘Na acheni kabisa kugusa kitu kisicho safi.’” Haikuwa lazima Wakristo wa Korintho waache Korintho ili watii amri hiyo. Hata hivyo, wao walikuwa na lazima ya kuepuka kihalisi mahekalu yasiyo safi ya dini bandia, pamoja na kujitenga wenyewe kiroho na matendo yasiyo safi ya waabudu sanamu hao. Katika 1919 watu wa Mungu walianza kukimbia kutoka katika Babuloni Mkubwa kwa njia hiyo, wakijisafisha wenyewe mabaki yoyote ya mafundisho na mazoea yasiyo safi. Hivyo, waliweza kutumikia yeye wakiwa watu wake waliosafishwa.—2 Wakorintho 6:14-17, NW; 1 Yohana 3:3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki