-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
“Lazima Wewe Uliache”
“Tokeni kwake, watu wangu,” Biblia ilionya zamani sana. Katika yeye nani? “Babiloni Mkubwa, mama wa makahaba na wa mambo yenye kuchukiza sana ya dunia.” (Ufu. 17:5; 18:4, NW) Kwa nini kuondoka katika Babiloni? “Kwa maana dhambi zake zimetungamana pamoja hadi mbinguni, na Mungu amekumbuka matendo yake yasiyo ya haki.” (Ufu. 18:5, NW) Ni nani huyu mama aliye kahaba ambaye watu wapaswa kujitenga naye?
-
-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Basi, wasomaji wa Watch Tower walitiwa moyo wafanye nini? Russell aliandika hivi: “Ikiwa kanisa unalohusiana nalo, huishi katika muungano wa uzinzi pamoja na ulimwengu, lazima wewe uliache, ikiwa utadumisha mavazi yako yakiwa meupe.” Russell na washirika wake hawakuelewa mweneo kamili wa uvutano wa Babiloni Mkubwa. Hata hivyo, wasomaji wa Watch Tower walihimizwa wajitenge na mifumo ya kanisa ambayo ilikuwa yenye ufisadi na ya kilimwengu.—Yn. 18:36.
-