Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kujipanga Kitengenezo Sasa kwa Ajili ya Miaka Elfu Itakayokuja
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Septemba 1
    • 3, 4. (a) Utawala wa Yehova kupitia Yesu Kristo na wale 144,000 utakuwa wa urefu gani hasa? (b) Ni usemi gani unaotumiwa kwa kipindi hicho cha wakati, na hilo lilionyeshwaje katika vichwa vya vichapo fulani vya Mnara wa Mlinzi?

      3 Urefu wa utawala wa Ufalme wa Yehova kupitia Yesu Kristo na wanafunzi wake 144,000 waliotukuzwa ulitabiriwa kuwa ungekuwa wa miaka elfu moja. Kuhusu Utawala huo wa Miaka Elfu, mtume Yohana mzee alisema hivi: “Na mimi niliona viti vya ufalme, na kulikuwa wale walioketi juu yavyo, na nguvu na kuhukumu zilipewa kwao. Ndiyo, mimi niliona nafsi za wale waliouawa kwa shoka kwa ajili ya ushahidi waliotoa kwa Yesu na kwa ajili ya kusema juu ya Mungu, na wale ambao hawakuwa wameabudu wala hayawani-mwitu wala mfano wake na ambao hawakuwa wamepokea alama juu ya kipaji cha uso wao na juu ya mkono wao. Na wao wakaja kwenye uhai na wakatawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo kwa miaka elfu moja. (Mabaki ya wafu hayakuja kwenye uhai mpaka miaka elfu ilipokuwa imekwisha.) Huu ndio ufufuo wa kwanza. Mwenye furaha na mtakatifu ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hawa kifo cha pili hakina mamlaka. Lakini wao watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala wakiwa wafalme pamoja na yeye kwa miaka elfu.”—Ufunuo 20:4-6. NW.

  • Kujipanga Kitengenezo Sasa kwa Ajili ya Miaka Elfu Itakayokuja
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Septemba 1
    • 5. Hali ya Shetani na roho wake waovu itakuwa nini wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo?

      5 Ule usemi “miaka elfu moja” kwenye Ufunuo 20:4, NW si wa mfano bali unarejezea miaka elfu moja ya kalenda-jua. Wakati wa Mileani hiyo, Shetani Ibilisi na makundi yake ya roho waovu watakuwa katika abiso, kwa kuwa kabla tu ya kueleza juu ya Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo, mtume Yohana alisema: “Na mimi nikaona malaika mmoja akija chini kutoka katika mbingu mwenye ufunguo wa abiso na mnyororo mkubwa katika mkono wake. Na yeye akakamata drakoni, nyoka wa awali kabisa, ambaye ndiye Ibilisi na Shetani, na akamboba yeye kwa miaka elfu moja. Na yeye alimvurumisha ndani ya abiso na akaifunga na akatia muhuri juu yake, ili asipate kuongoza vibaya mataifa tena mpaka miaka elfu ilipokuwa imekwisha. Baada ya vitu hivi ni lazima yeye aachwe legelege kwa kitambo kidogo.” —Ufunuo 20:1-3, NW.

  • Kujipanga Kitengenezo Sasa kwa Ajili ya Miaka Elfu Itakayokuja
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Septemba 1
    • 7. Biblia inaonyesha nini kuhusu wakati na hali ya Utawala wa Mileani wa Yesu Kristo?

      7 Hata hivyo, kulingana na Maandiko, Utawala wa kweli wa Mileani wa Yesu Kristo ungali mbele. Utimizo wa kisasa wa unabii wa Biblia unaonyesha umekaribia sana. Wakati wa Mileani ya kweli, Shetani na roho waovu wake watawekwa katika abiso kihalisi, na Yesu Kristo na warithi washiriki wake 144,000 watatawala juu ya aina yote ya wanadamu bila kuzuiwa na tengenezo la Ibilisi. Baraka ya milele ya aina yote ya wanadamu waliokombolewa, kwa kutimiza agano la Yehova pamoja na “rafiki” yake Abrahamu, itaanza na “umati mkubwa,” utakaookoka “dhiki” isiyo na ulinganisho ambayo mfumo huu mbovu unamalizika kwayo. Itaenea kwa mabilioni ya wanadamu wafu watakaokombolewa kwa “damu ya Mwana-Kondoo,” Yesu Kristo. (Yakobo 2:21-23; Ufunuo 7:1-17; Mwanzo 12:3; 22:15-18; Mathayo 24:21, 22, NW) Kwa kusudi hili, hawa watafufuliwa kutoka usingizi wao wa kifo katika makaburi ya ukumbusho ili wapate uhai duniani.—Yohana 5:28, 29.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki