Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kujipanga Kitengenezo Sasa kwa Ajili ya Miaka Elfu Itakayokuja
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Septemba 1
    • 3, 4. (a) Utawala wa Yehova kupitia Yesu Kristo na wale 144,000 utakuwa wa urefu gani hasa? (b) Ni usemi gani unaotumiwa kwa kipindi hicho cha wakati, na hilo lilionyeshwaje katika vichwa vya vichapo fulani vya Mnara wa Mlinzi?

      3 Urefu wa utawala wa Ufalme wa Yehova kupitia Yesu Kristo na wanafunzi wake 144,000 waliotukuzwa ulitabiriwa kuwa ungekuwa wa miaka elfu moja. Kuhusu Utawala huo wa Miaka Elfu, mtume Yohana mzee alisema hivi: “Na mimi niliona viti vya ufalme, na kulikuwa wale walioketi juu yavyo, na nguvu na kuhukumu zilipewa kwao. Ndiyo, mimi niliona nafsi za wale waliouawa kwa shoka kwa ajili ya ushahidi waliotoa kwa Yesu na kwa ajili ya kusema juu ya Mungu, na wale ambao hawakuwa wameabudu wala hayawani-mwitu wala mfano wake na ambao hawakuwa wamepokea alama juu ya kipaji cha uso wao na juu ya mkono wao. Na wao wakaja kwenye uhai na wakatawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo kwa miaka elfu moja. (Mabaki ya wafu hayakuja kwenye uhai mpaka miaka elfu ilipokuwa imekwisha.) Huu ndio ufufuo wa kwanza. Mwenye furaha na mtakatifu ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hawa kifo cha pili hakina mamlaka. Lakini wao watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala wakiwa wafalme pamoja na yeye kwa miaka elfu.”—Ufunuo 20:4-6. NW.

      4 Kwa kuwa miaka elfu ni mileani, kipindi hicho kinaitwa Utawala wa Kristo wa Mileani. Wale wanaokubali na kufundisha fundisho hili la Biblia wakati fulani huitwa wamileani au wakiliasti, kulingana na neno la Kigiriki kwa “elfu.” Jambo la kupendeza ni kwamba, mabuku ya Studies in the Scriptures (ambayo yalitangazwa kwa chapa wakati mmoja na Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti) hapo awali yaliitwa Millennial Dawn. Na kitabu cha nyimbo ambacho kilitumiwa wakati mmoja na Wanafunzi wa Kimataifa wa Biblia kilikuwa na kichwa Hymns of the Millenial Dawn.

  • Kujipanga Kitengenezo Sasa kwa Ajili ya Miaka Elfu Itakayokuja
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Septemba 1
    • 7. Biblia inaonyesha nini kuhusu wakati na hali ya Utawala wa Mileani wa Yesu Kristo?

      7 Hata hivyo, kulingana na Maandiko, Utawala wa kweli wa Mileani wa Yesu Kristo ungali mbele. Utimizo wa kisasa wa unabii wa Biblia unaonyesha umekaribia sana. Wakati wa Mileani ya kweli, Shetani na roho waovu wake watawekwa katika abiso kihalisi, na Yesu Kristo na warithi washiriki wake 144,000 watatawala juu ya aina yote ya wanadamu bila kuzuiwa na tengenezo la Ibilisi. Baraka ya milele ya aina yote ya wanadamu waliokombolewa, kwa kutimiza agano la Yehova pamoja na “rafiki” yake Abrahamu, itaanza na “umati mkubwa,” utakaookoka “dhiki” isiyo na ulinganisho ambayo mfumo huu mbovu unamalizika kwayo. Itaenea kwa mabilioni ya wanadamu wafu watakaokombolewa kwa “damu ya Mwana-Kondoo,” Yesu Kristo. (Yakobo 2:21-23; Ufunuo 7:1-17; Mwanzo 12:3; 22:15-18; Mathayo 24:21, 22, NW) Kwa kusudi hili, hawa watafufuliwa kutoka usingizi wao wa kifo katika makaburi ya ukumbusho ili wapate uhai duniani.—Yohana 5:28, 29.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki