Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ziwa la Moto Ni Nini? Je, Ni Sawa na Moto wa Mateso au Gehena?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
      • Ibilisi. (Ufunuo 20:10) Kwa kuwa Ibilisi ni kiumbe wa roho, hawezi kuumizwa na moto halisi.​—Kutoka 3:2; Waamuzi 13:20.

  • Ziwa la Moto Ni Nini? Je, Ni Sawa na Moto wa Mateso au Gehena?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
    • ‘Wanateswaje mchana na usiku milele na milele’?

      Ikiwa ziwa la moto ni mfano wa uharibifu, kwa nini Biblia inasema kwamba Ibilisi, mnyama-mwitu, na yule nabii wa uwongo “watateswa mchana na usiku milele na milele”? (Ufunuo 20:10) Fikiria sababu nne kwa nini mateso hayo si mateso halisi:

      1. Ili Ibilisi ateswe milele, angehitaji kuendelea kuishi milele. Hata hivyo, Biblia inasema ataangamizwa, au hataendelea kuwapo.​—Waebrania 2:​14.

      2. Uzima wa milele ni zawadi kutoka kwa Mungu, si adhabu.​—Waroma 6:​23.

      3. Mnyama-mwitu na yule nabii wa uwongo ni mifano tu ambayo haiwezi kuteswa kihalisi.

      4. Muktadha wa Biblia unaonyesha kwamba mateso ya Ibilisi ni kizuizi au uharibifu wa milele.

      Neno linalotumiwa kurejezea “mateso” katika Biblia linaweza kumaanisha pia hali ya kuzuiwa. Kwa mfano, katika tafsiri nyingi, maneno “walinzi wa jela” yanatumiwa kuwakilisha neno la Kigiriki “watesaji” kwenye Mathayo 18:34, kuonyesha uhusiano kati ya maneno “mateso” na “kizuizi.” Vivyo hivyo, masimulizi yanayofanana kwenye Mathayo 8:​29 na Luka 8:​30, 31 yanahusianisha “mateso” na mahali panapoitwa “abiso.” Abiso ni mahali pa mfano ambapo hakuna utendaji au kifo. (Waroma 10:7; Ufunuo 20:​1, 3) Kwa kweli, kitabu cha Ufunuo kinatumia neno “mateso” mara kadhaa kwa njia ya mfano.​—Ufunuo 9:5; 11:10; 18:​7, 10.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki