-
Biblia Inatupatia TumainiFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Biblia inaahidi nini kuhusu wakati ujao?
Biblia inaeleza kwamba wakati ujao “kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.” (Soma Ufunuo 21:4.) Matatizo yanayofanya tukate tamaa maishani leo, kama vile umaskini, ukosefu wa haki, magonjwa, na kifo, hayatakuwapo tena. Biblia inaahidi kwamba wanadamu watafurahia kuishi milele katika Paradiso duniani.
-
-
Kwa Nini Wanadamu Wanateseka na Kupatwa na Mambo Mabaya?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
7. Mungu atakomesha mateso yote yanayowapata wanadamu
Soma Isaya 65:17 na Ufunuo 21:3, 4, kisha mzungumzie swali hili:
Kwa nini inafariji kujua kwamba Yehova ataondoa madhara yote yanayowapata wanadamu?
Je, wajua?
Shetani aliposema uwongo wa kwanza alimchongea Yehova, yaani, alimharibia Yehova sifa kwa kudai kwamba ni Mtawala asiye na haki na upendo. Hivi karibuni, Yehova atalitakasa jina lake atakapoondoa mateso yanayowapata wanadamu. Hilo linamaanisha, atathibitisha kwamba utawala wake ndio utawala bora. Kutakaswa kwa jina la Yehova ndilo jambo muhimu zaidi ulimwenguni.—Mathayo 6:9, 10.
-