-
Ufunuo na WeweUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
15. Ni nini maana ya maneno ya Yesu kwamba yeye “hutoa ushahidi wa vitu hivi” na “mimi ninakuja upesi”?
15 Sasa Yesu aongeza neno la mwisho la kitia-moyo: “Yeye ambaye hutoa ushahidi wa vitu hivi asema, ‘Ndiyo; mimi ninakuja upesi.’” (Ufunuo 22:20a, NW) Yesu ndiye “shahidi mwaminifu na wa kweli.” (Ufunuo 3:14, NW) Ikiwa yeye hutoa ushahidi wa njozi za Ufunuo, lazima ziwe za kweli. Yeye na Yehova Mungu mwenyewe pia wanakazia kwa kurudia-rudia uhakika wa kwamba wanakuja “upesi,” au karibuni, Yesu akisema hivyo hapa kwa mara ya tano. (Ufunuo 2:16; 3:11; 22:7, 12, 20) ‘Kuja’ huko ni kutekeleza hukumu juu ya kahaba, juu ya “wafalme” wa kisiasa na wengine wote wanaopinga “ufalme wa Bwana [Yehova] wetu na wa Kristo wake.”—Ufunuo 11:15; 16:14, 16; 17:1, 12-14, NW.
16. Ukijua kwamba Yehova Mungu na Yesu wanakuja upesi, imekupasa wewe uchukue tendo gani la kuazimia?
16 Kujua kwako kwamba Yehova Mungu na Yesu wanakuja upesi kwapasa kukutie moyo uweke “karibu akilini kuwapo kwa siku ya Yehova.” (2 Petro 3:12, NW) Wowote unaoonekana kuwa uthabiti wa dunia ya mfumo wa mambo wa Shetani ni udanganyo. Lolote linaloonekana kuwa fanikio ambalo mbingu za watawala walimwengu chini ya Shetani huenda wakapata linapita tu. Vitu hivi vinapitilia mbali. (Ufunuo 21:1) Udumu pekee unapatikana katika Yehova, Ufalme wake chini ya Yesu Kristo, na ulimwengu mpya wake ulioahidiwa. Usikose kamwe kuona hilo!—1 Yohana 2:15-17.
-
-
Ufunuo na WeweUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
19. Ni maneno gani yenye kufunga ya mtume Yohana mwenye umri wa uzee, na wewe unayaitikiaje?
19 Hivyo, pamoja na Yohana, sisi tunasali kwa bidii: “Ameni! Njoo, Bwana Yesu.” Na Yohana, mtume mwenye umri wa uzee, aongeza: “Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo na ziwe pamoja na watakatifu.” (Ufunuo 22:20b, 21, NW) Na ziwe pia na nyinyi nyote mnaosoma kichapo hiki. Na mwe na imani ya kwamba upeo mtukufu wa Ufunuo umekaribia, ili nyinyi pia mweze kujiunga nasi katika kusema kutoka moyoni “Ameni!”
-