Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Aja na Kitia-Moyo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 1. Sasa Yohana anaandikia nani, na ni nani leo wanaopaswa kuona ujumbe wake ukiwa wenye upendezi wenye kuvuta fikira?

      YALE yanayofuata yapasa yawe yenye upendezi wenye kuvuta fikira kwa kila mmoja anayeshirikiana na makundi ya watu wa Mungu leo. Hapa pana mfululizo wa jumbe. Hizo zina tumizi maalumu kadiri “ule wakati uliowekwa” uzidivyo kukaribia. (Ufunuo 1:3, NW) Ni kwa manufaa yetu ya milele kwamba tutii matangazo hayo. Maandishi hayo yanasomwa hivi: “Yohana kwa yale makundi saba ambayo yako katika wilaya ya Esia: Na mwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa ‘Yule Mmoja ambaye yuko na ambaye alikuwako na ambaye anakuja,’ na kutoka kwa zile roho saba zilizo mbele ya kiti cha ufalme chake, na kutoka kwa Yesu Kristo.”—Ufunuo 1:4, 5a, NW.

  • Yesu Aja na Kitia-Moyo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 3. (a) Katika salamu ya Yohana, “fadhili zisizostahiliwa na amani” hutoka wapi? (b) Ni usemi gani wa mtume Paulo unaofanana na salamu ya Yohana?

      3 “Fadhili zisizostahiliwa na amani”—hizo ni zenye kutamanika kama nini hasa tunapothamini chanzo chazo! Yule “Mmoja” ambaye kutoka kwake zinatiririka ni Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu mwenyewe, “Mfalme wa umilele,” aishiye “kutoka wakati usio dhahiri mpaka wakati usio dhahiri.” (1 Timotheo 1:17; Zaburi 90:2, NW) Vilevile, zinazohusika hapa ni “zile roho saba,” usemi ambao unaonyesha utendaji kamili wa kani-tendaji ya Mungu, au roho takatifu, inapoleta uelewevu na baraka kwa wote wanaoupa unabii huu uangalifu. Aliye na sehemu pia ni “Yesu Kristo,” ambaye kwa habari zake Yohana aliandika baadaye hivi: “Yeye alijaa fadhili zisizostahiliwa na ukweli.” (Yohana 1:14, NW) Hivyo, salamu za Yohana zina elementi zile zile ambazo mtume Paulo alitaja katika kufunga barua yake ya pili kwa kundi la Korintho: “Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo na upendo wa Mungu na kushiriki roho takatifu ziwe pamoja nanyi nyote.” (2 Wakorintho 13:14, NW) Maneno hayo na yatumike pia kwa kila mmoja wetu anayependa ukweli leo!—Zaburi 119:97.

      “Shahidi Mwaminifu”

      4. Yohana anaendelea kumwelezeaje Yesu Kristo, na ni kwa sababu gani semi hizo za maelezeo zinafaa?

      4 Kufuata Yehova, Yesu ndiye mtu mtukufu zaidi sana katika ulimwengu wote mzima, kama Yohana anavyotambua, akimsimulia kuwa “‘Shahidi Mwaminifu,’ ‘mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,’ na ‘Mtawala wa wafalme wa dunia.’” (Ufunuo 1:5b, NW) Kama vile mwezi katika mbingu, yeye amesimamishwa imara kuwa Shahidi aliye mkubwa zaidi sana kwa Uungu wa Yehova. (Zaburi 89:37) Baada ya yeye kushika ukamilifu mpaka kifo cha dhabihu, akapata kuwa wa kwanza miongoni mwa aina ya binadamu kuinuliwa kwenye uhai wa kiroho usioweza kufa. (Wakolosai 1:18) Sasa akiwa katika kuwapo kwa Yehova, amekwezwa kwenye hali ya juu, juu sana ya wafalme wote wa kidunia, akiwa amevishwa “mamlaka yote . . . katika mbingu na juu ya dunia.” (Mathayo 28:18, NW; Zaburi 89:27; 1 Timotheo 6:15) Katika 1914 yeye aliwekwa awe Mfalme atawale miongoni mwa mataifa ya kidunia.—Zaburi 2:6-9.

      5. (a) Yohana anaendelea kuonyeshaje uthamini kwa Bwana Yesu Kristo? (b) Ni nani wanaonufaika na zawadi ya Yesu ya uhai wake mkamilifu wa kibinadamu, na Wakristo wapakwa-mafuta wameshirikije baraka ya pekee?

      5 Yohana anaendelea kuonyesha uthamini kwa Bwana Yesu Kristo katika maneno haya yenye uchangamshi: “Kwake yeye ambaye hupenda sisi na ambaye alifungua sisi kutoka madhambi yetu kwa njia ya damu yake mwenyewe—naye alifanya sisi kuwa ufalme, makuhani kwa Mungu na Baba yake—ndiyo, kwake yeye kuwe utukufu na uweza milele. Ameni.” (Ufunuo 1:5c, 6, NW) Yesu alitoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu ili wale wa ulimwengu wa aina ya binadamu wanaozoea imani katika yeye waweze kurudishwa kwenye uhai mkamilifu. Wewe, msomaji mpenzi, waweza kutiwa ndani ya hili! (Yohana 3:16) Lakini kifo cha dhabihu cha Yesu kilifungulia njia baraka ya pekee kwa ajili ya wale wanaokuwa Wakristo wapakwa-mafuta kama Yohana. Hawa wametangazwa kuwa waadilifu kwa msingi wa dhabihu ya ukombozi ya Yesu. Wakikataa katakata matazamio yote ya uhai wa kidunia, kama alivyofanya Yesu, hao wa lile kundi dogo wamezaliwa kwa roho ya Mungu, wakiwa na taraja la kufufuliwa wakatumikie wakiwa wafalme na makuhani pamoja na Yesu Kristo katika Ufalme wake. (Luka 12:32; Warumi 8:18; 1 Petro 2:5; Ufunuo 20:6) Lo! ni pendeleo tukufu kama nini! Si ajabu Yohana alipaaza sauti kwa uthabiti hivyo kwamba utukufu na uweza una Yesu!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki