Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kukirihi “Vitu Vyenye Kina Kirefu vya Shetani”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 8. (a) Ni nini tamko la hukumu la Yesu juu ya yule “Yezebeli” katika Thiatira? (b) Uvutano wa kike usiofaa umehisiwaje katika nyakati za ki-siku-hizi?

      8 Yesu anaendelea kuwaambia wazee katika Thiatira hivi: “Na mimi nilimpa wakati wa kutubu, lakini yeye hataki kutubu uasherati wake. Tazama! Mimi niko karibu kutupa yeye katika kitanda cha ugonjwa, na wale wanaofanya uasherati pamoja na yeye katika dhiki kubwa, wasipotubu matendo yake.” (Ufunuo 2:21, 22, NW) Kama vile yule Yezebeli wa kwanza kabisa kwa wazi alivyomtawala Ahabu na kisha akamkaidi Yehu, mfishaji wa Mungu, ndivyo uvutano huu wa kike huenda ukawa unajaribu kutumia hila juu ya waume na wazee. Inaonekana kwamba wazee katika Thiatira wanavumilia uvutano huu usio na kiasi wa Yezebeli. Hapa Yesu anatoa onyo kali kwao, pamoja na kwa kundi lililo kwenye tufe lote la watu wa Yehova leo. Katika nyakati za ki-siku-hizi, baadhi ya wanawake kama hao wenye nia ngumu wameshawishi waume zao wawe waasi-imani na hata wamechukua hatua ya kimahakama dhidi ya watumishi waaminifu wa Yehova.—Linga Yuda 5-8.

  • Kukirihi “Vitu Vyenye Kina Kirefu vya Shetani”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 10. (a) Ni kwa nini Yezebeli na watoto wake walipokea hukumu? (b) Wale wanaokuwa watoto wa Yezebeli wako katika hali gani ya hatari, na watu kama hao imewapasa wafanye nini?

      10 Akirejezea “huyo mwanamke Yezebeli,” Yesu anaendelea: “Na watoto wake mimi nitaua kwa tauni yenye kufisha, ili makundi yote yajue kwamba mimi ndiye ambaye huchunguza figo na mioyo, na mimi nitatoa kwa nyinyi mmoja mmoja kulingana na matendo yenu.” (Ufunuo 2:23, NW) Yesu ameruhusu Yezebeli na watoto wake wakati wa kutubu, lakini wao wanaendelea katika njia zao za ukosefu wa adili na kwa sababu hiyo lazima wapokee hukumu. Hapa pana ujumbe wenye nguvu nyingi kwa Wakristo leo. Wale wanaoiga Yezebeli, wawe ni wanaume au wanawake, na hivyo wamekuwa watoto wake kwa kuhalifu kanuni za Biblia juu ya ukichwa na maadili au kwa kuwa wenye kichwa kigumu hivi kwamba wanapuuza utaratibu wa kitheokrasi, kwa njia ya kiroho wamo katika hali yenye hatari sana ya ugonjwa. Ni kweli, ikiwa mmoja kama huyo anawaita wazee katika kundi wakamwombee, hiyo “sala ya imani itafanya huyo asiye na maelekeo mazuri ahisi vema, na Yehova atainua yeye”—maadamu yeye anatenda kwa unyenyekevu kupatana na sala hizo. Lakini yeyote asifikiri kwamba yeye anaweza kudanganya Mungu au Kristo kwa kujaribu kuficha matendo ya ukosefu wa adili au kwa kujivika wonyesho wa nje-nje wa utumishi wenye bidii.—Yakobo 5:14, 15, NW.

  • Kukirihi “Vitu Vyenye Kina Kirefu vya Shetani”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 13. Ni nini litakalowapata wale wanaoshindwa na uvutano wenye makosa wa kike?

      13 Akiwa Mjumbe na Hakimu wa Yehova, Mwana wa Mungu anatenda kwa usahihi katika kutambulisha Yezebeli wa ki-siku-hizi na kumtupa ndani ya kitanda cha ugonjwa, kwa kuwa ugonjwa wake wa kiroho ni wenye kusendeka kweli kweli. (Malaki 3:1, 5) Wale ambao wameshindwa na uvutano huu wenye makosa wa kike pia watapatwa na dhiki kubwa—ile huzuni ya kutengwa na ushirika, kukatiliwa mbali na kundi la Kikristo kama kwamba ni wafu. Isipokuwa hawa wanatubu, wanageuka, na wanakubaliwa tena ndani ya kundi, wanakabili pia kifo cha kimwili kwa “tauni yenye kufisha”—mwishowe kabisa, katika ile dhiki kubwa. Kwa wakati huu, kurudishwa kunawezekana ikiwa wanatubia kabisa matendo yao yenye kosa.—Mathayo 24:21, 22; 2 Wakorintho 7:10.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki