Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 10. Ni kitia-moyo gani anachotoa Yesu kwa kundi katika Filadelfia?

      10 Yakija kutoka chanzo kama hicho chenye mamlaka, maneno ya Yesu kwa Wakristo katika Filadelfia lazima yawe yenye kufariji hasa! Yeye anawasifu, akisema: “Mimi najua matendo yako—tazama! mimi nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa, ambao hakuna mmoja awezaye kufunga—kwamba wewe una nguvu chache, na wewe ulishika neno langu na hukuthibitika kuwa bandia kwa jina langu.” (Ufunuo 3:8, NW) Kundi limekuwa lenye kutenda, nao mlango umefunguliwa mbele yalo—bila shaka mlango wa nafasi ya utumishi wa kihuduma. (Linga 1 Wakorintho 16:9; 2 Wakorintho 2:12.) Kwa hiyo, Yesu analitia moyo kundi litumie kwa faida kamili ile nafasi ya kuhubiri. Wao wamevumilia na kuonyesha kwamba wana nguvu za kutosha, kwa msaada wa roho ya Mungu, kuendelea kufanya “matendo” zaidi katika utumishi wa Yehova. (2 Wakorintho 12:10; Zekaria 4:6) Wametii amri za Yesu nao hawakumkana Kristo ama kwa neno ama kwa tendo.

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 14. Ni jinsi gani Isaya 49:23 na Zekaria 8:23 yamekuwa na utimizo wa maana katika nyakati za ki-siku-hizi?

      14 Katika nyakati za ki-siku-hizi, unabii kama vile Isaya 49:23 na Zekaria 8:23 umekuwa na utimizo wenye umaana sana. Likiwa tokeo la kuhubiri kwa jamii ya Yohana, hesabu kubwa za watu zimepitia ule mlango uliofunguliwa wakaingia ndani ya utumishi wa Ufalme.b Walio wengi wa hawa wametoka katika Jumuiya ya Wakristo, ambayo dini zayo hudai kwa ubandia kuwa Waisraeli wa kiroho. (Linga Warumi 9:6.) Hawa, wakiwa umati mkubwa, wanafua mavazi yao na kuyafanya meupe kwa kutumia imani katika damu ya dhabihu ya Yesu. (Ufunuo 7:9, 10, 14) Kwa kutii utawala wa Kristo wa Ufalme, wanatumaini kurithi baraka zao hapa duniani. Wanakuja kwa ndugu za Yesu wapakwa-mafuta na ‘kuwainamia,’ kiroho, kwa sababu ‘wamesikia kwamba Mungu yu pamoja nao.’ Wanahudumia hawa wapakwa-mafuta, ambao pamoja nao wanakuwa wenye umoja katika ushirika wa ndugu ulimwenguni pote.—Mathayo 25:34-40; 1 Petro 5:9.

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • b Gazeti Mnara wa Mlinzi linalotangazwa na jamii ya Yohana, limeendelea kukazia umuhimu wa kutwaa nafasi hii na kushiriki kikamilifu kadiri iwezekanavyo katika kazi ya kuhubiri; mathalani, ona makala “Wote na Wautangaze Utukufu wa Yehova” na “Sauti Yao Ilifika Katika Dunia Yote” katika toleo la Januari 1, 2004. Katika toleo la Juni 1, 2004, katika makala “Wanaomtukuza Mungu Hubarikiwa,” mkazo uliwekwa juu ya kuingia “mlango uliofunguliwa” ndani ya utumishi wa wakati wote. Kulikuwako kilele cha mapainia 1,093,552 walioripoti utumishi kama huo katika pindi ya mwezi mmoja katika 2005.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki