-
“Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
17 Katika 1918 jamii ya Yohana ya Wakristo wapakwa-mafuta—kama kundi hilo mathubuti katika Filadelfia—ilikuwa sharti ikabili upinzani kutoka “sinagogi la Shetani” la ki-siku-hizi. Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, ambao hudai kuwa Wayahudi wa kiroho, waliongoza kwa hila watawala wakandamize Wakristo wa kweli. Hata hivyo, hao walijaribu sana ‘kushika neno la uvumilivu wa Yesu’; kwa sababu hiyo, kwa msaada wa kiroho, “nguvu chache” zenye maana, waliokoka na wakaamshwa waingie kupitia mlango ambao sasa ulifunguliwa mbele yao. Katika njia gani?
“Mlango Uliofunguliwa”
18. Ni kuweka rasmi gani alikofanya Yesu katika 1919, na hivyo mwekwa alikuwaje kama mtumishi wa nyumba mwaminifu wa Hezekia?
18 Katika 1919 Yesu alitimiza ahadi yake na kukitambua kile kikosi kidogo cha Wakristo wapakwa-mafuta cha kweli kuwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” wake. (Mathayo 24:45-47) Hao waliingia ndani ya pendeleo linalofanana na lile alilofurahia Eliakimu mtumishi wa nyumba mwaminifu katika wakati wa Hezekia.d Yehova alisema hivi kwa habari ya Eliakimu: “Na ufunguo wa nyumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga; naye atafunga wala hapana atakayefungua.” Eliakimu alibeba begani madaraka mazito kwa ajili ya Hezekia, yule mwana wa kifalme wa Daudi. Hali moja na hiyo leo, jamii ya Yohana ya wapakwa-mafuta imewekelewa begani mwayo “ufunguo wa nyumba ya Daudi” katika maana ya kwamba wameaminishwa masilahi ya kidunia ya Ufalme wa Kimesiya. Yehova ameimarisha watumishi wake kwa ajili ya pendeleo hili, akiongezea nguvu chache zao kuwa nishati yenye msukumo inayotosha kwa ushuhuda mkubwa wa tufe lote.—Isaya 22:20, 22; 40:29.
19. Jamii ya Yohana ilishughulikiaje madaraka ambayo ilipewa na Yesu katika 1919, kukiwa na tokeo gani?
19 Tangu 1919 na kuendelea mabaki ya wapakwa-mafuta, wakifuata kielelezo cha Yesu, walianzisha kampeni yenye bidii ya kutangaza kotekote habari njema za Ufalme. (Mathayo 4:17; Warumi 10:18) Kama tokeo, wengine wa lile sinagogi la Shetani la ki-siku-hizi, Jumuiya ya Wakristo, walijia baki hili la wapakwa-mafuta, wakatubu na ‘wakainama,’ wakikiri mamlaka ya mtumwa huyo. Wao vilevile walikuja kutumikia Yehova katika muungano na wale wazee-wazee wa jamii ya Yohana. Hilo liliendelea mpaka hesabu kamili ya ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu wakakusanywa. Kufuatia hili, “umati mkubwa . . . kutoka mataifa yote” umekuja ‘ukainamia’ mtumwa mpakwa-mafuta. (Ufunuo 7:3, 4, 9, NW) Pamoja, mtumwa huyu na huu umati mkubwa wanatumikia wakiwa kundi moja la Mashahidi wa Yehova.
-
-
“Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
25. Kila Mkristo mmoja mmoja leo anaweza kutumiaje kanuni iliyo katika shauri ambalo Yesu alitoa kwa kundi katika Filadelfia?
25 Lo! ujumbe huo lazima uwe ulikuwa kitia-moyo kama nini kwa Wakristo waaminifu katika Filadelfia! Na hakika kuna somo lenye nguvu nyingi kwa ajili ya jamii ya Yohana sasa, wakati wa siku ya Bwana. Lakini kanuni zao ni za maana kwa kila Mkristo mmoja mmoja, awe ni wa wapakwa-mafuta au wa kondoo wengine. (Yohana 10:16) Kila mmoja wetu angefanya vema kufuliza kuzaa tunda la Ufalme kama walivyofanya hawa Wakristo katika Filadelfia. Sote tuna angalau nguvu chache. Sisi sote tunaweza kufanya jambo fulani katika utumishi wa Yehova. Acheni tuitumie nguvu hii! Kwa habari ya mapendeleo ya Ufalme yaliyoongezeka, acheni sisi tuwe chonjo kuingia mlango wowote unaofunguliwa kwetu. Sisi hata tunaweza kusali kwa Yehova afungue mlango kama huo. (Wakolosai 4:2, 3) Tunapofuata kigezo cha Yesu cha uvumilivu na kujithibitisha kuwa wa kweli kwa jina lake, tutaonyesha kwamba sisi, vilevile, tuna sikio la kusikia kile ambacho roho ya Mungu husema kwa makundi.
-