-
Kuwapo kwa Mesiya na Utawala WakeMnara wa Mlinzi—1992 | Oktoba 1
-
-
Jinsi ya Kurudi kwa Kristo
3. Watu wengi huamini nini juu ya kurudi kwa Kristo?
3 Kulingana na kitabu An Evangelical Christology, “kuja kwa pili au kurudi kwa Kristo (parousia) kunasimamisha Ufalme wa Mungu, hatimaye, waziwazi, na kwa umilele wote.” Ni imani ya wengi kwamba kurudi kwa Kristo kutaonekana waziwazi, kukionekana kihalisi na kila mtu kwenye sayari. Ili kuunga mkono wazo hilo, wengi huelekezea Ufunuo 1:7, linalosomwa hivi: “Tazama, yuaja na mawingu; na kila jicho litamwona, na hao waliomchoma.” Lakini je, mstari huo uchukuliwe kihalisi?
4, 5. (a) Tunajuaje kwamba Ufunuo 1:7 halina maana ya kihalisi? (b) Maneno ya Yesu mwenyewe yanathibitishaje uelewevu huo?
4 Kumbuka, kitabu cha Ufunuo kimetolewa “kwa njia ya ishara.” (Ufunuo 1:1, NW) Kwa hiyo, fungu hilo lazima liwe la ufananisho; kwa vyovyote vile, wale “waliomchoma” wangewezaje kuona kurudi kwa Kristo? Wamekuwa wafu kwa karibu karne 20! Zaidi ya hayo, malaika walisema kwamba Kristo angerudi “jinsi iyo hiyo” alivyoondoka. Basi, aliondokaje? Kukiwa na mamilioni wakitazama? La, ni waaminifu wachache tu waliotazama tukio hilo. Na wakati malaika waliposema nao, je, mitume walikuwa wakimtazama Yesu kihalisi akisafiri moja kwa moja hadi mbinguni? La, funiko la wingu lilikuwa limemfunika Yesu asionekane. Muda fulani baadaye, ni lazima awe aliingia mbingu za roho akiwa mtu wa roho, asiweze kuonekana kwa macho ya kibinadamu. (1 Wakorintho 15:50) Kwa hiyo, kile ambacho mitume waliweza kuona tu ni mwanzo wa safari ya Yesu; wasingeweza kuona mwisho wayo, kurudi kwake kwenye kuwapo kwa kimbingu kwa Baba yake, Yehova. Wangeweza kutambua hilo tu kwa macho yao ya imani.—Yohana 20:17.
5 Biblia hufundisha kwamba Yesu arudi katika njia inayofanana sana na hiyo. Yesu mwenyewe alisema hivi muda mfupi kabla ya kifo chake: “Baada ya muda mrefu kidogo ulimwengu hautaniona tena.” (Yohana 14:19, NW) Alisema pia kwamba “Ufalme wa Mungu hauji kwa namna itakayoweza kuonekana.” (Luka 17:20, Habari Njema kwa Watu Wote) Kwa hiyo, “kila jicho litamwona” katika maana gani? Ili kujibu hilo, tunahitaji kwanza uelewevu dhahiri wa lile neno ambalo Yesu na wafuasi wake walitumia kwa habari ya kurudi kwake.
6. (a) Kwa nini maneno kama vile “kurudi,” “kuwasili,” “adventi,” na “kuja” si tafsiri zifaazo kwa lile neno la Kigiriki pa·rou·siʹa? (b) Ni nini kinachoonyesha kwamba pa·rou·siʹa, au “kuwapo,” hudumu muda mrefu zaidi ya tukio lolote la muda mfupi tu?
6 Jambo la hakika ni kwamba, Kristo afanya mengi zaidi ya “kurudi” tu. Neno hilo (“kurudi”) kama vile maneno “kuja,” “kuwasili,” au “adventi,” hudokeza tukio moja katika muda mfupi wa wakati. Lakini neno la Kigiriki ambalo Yesu na wafuasi wake walitumia humaanisha mengi zaidi. Neno hilo ni pa·rou·siʹa, linalomaanisha kihalisi “kuwa kando” au “kuwapo.” Wanachuo wengi hukubali kwamba neno hilo hutia ndani si kuwasili tu bali pia kuwapo kunakofuata—kama vile katika ziara rasmi ya mkuu fulani wa kifalme. Kuwapo huko si tukio la muda mfupi tu; hiyo ni muhula wa pekee, kipindi cha wakati chenye kutokeza. Kwenye Mathayo 24:37-39, NW, Yesu alisema kwamba “kuwapo [pa·rou·siʹa] kwa Mwana wa binadamu” kungekuwa kama “siku za Noa” zilizofikia upeo katika Furiko. Noa alikuwa akijenga safina na kuwaonya waovu kwa muda wa miongo kadhaa kabla ya Furiko kuwasili na kufutilia mbali huo mfumo wa ulimwengu wenye ufisadi. Vilevile, basi, kuwapo kwa Kristo kusikoonekana hudumu kwa kipindi cha miongo kadhaa kabla hakijafikia upeo katika uharibifu mkubwa.
7. (a) Ni nini kinachothibitisha kwamba pa·rou·siʹa haionekani kwa macho ya kibinadamu? (b) Maandiko yanayosimulia kurudi kwa Kristo kuwa kwenye kuonekana kwa “kila jicho” yatatimizwa kwa jinsi gani na wakati gani?
7 Pasipo shaka, ile pa·rou·siʹa haionekani kihalisi kwa macho ya kibinadamu. Kama ingaliweza kuonekana kihalisi, ni kwa nini Yesu alitumia wakati mwingi, kama vile tutakavyoona, akiwapa wafuasi wake ishara ya kuwasaidia watambue kuwapo huko?a Hata hivyo, Kristo anaporudi ili kuharibu mfumo wa ulimwengu wa Shetani, uhakika wa kuwapo kwake utadhihirika sana kwa wote. Ni wakati huo kwamba “kila jicho litamwona.” Hata wapinzani wa Yesu wataweza kutambua, kwa hofu yao, kwamba utawala wa Kristo ni halisi.—Ona Mathayo 24:30; 2 Wathesalonike 2:8; Ufunuo 1:5, 6.
-
-
Kuwapo kwa Mesiya na Utawala WakeMnara wa Mlinzi—1992 | Oktoba 1
-
-
a Huko nyuma katika 1864 mwanatheolojia R. Govett alieleza jambo hilo hivi: “Hilo laonekana kwangu kuwa jambo la waziwazi sana. Utoaji wa ishara ya Kuwapo unaonyesha kwamba hiyo ni siri. Hatuhitaji ishara yoyote kutuonyesha kuwapo kwa kile tunachoona.”
-