Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mungu Ni Nani?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 2. Biblia inatufundisha nini kumhusu Yehova?

      Biblia inasema kwamba kati ya miungu yote ambayo watu huabudu, Yehova ndiye Mungu pekee wa kweli. Kwa nini? Kuna sababu kadhaa. Yehova ndiye mwenye mamlaka yote, na yeye ndiye aliye “Juu Zaidi, juu ya dunia yote.” (Soma Zaburi 83:18.) Yeye ndiye “Mweza-Yote,” kwa sababu ana uwezo wa kufanya chochote anachotaka kufanya. Yeye ndiye ‘aliyeumba vitu vyote,’ kutia ndani ulimwengu na kila kitu kilicho hai duniani. (Ufunuo 4:​8, 11) Yehova peke yake ndiye amekuwepo sikuzote, na ataendelea kuwepo milele.​—Zaburi 90:2.

  • Ni Ibada Gani Inayokubalika kwa Mungu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Tunapaswa kumwabudu Yehova peke yake kwa sababu yeye ndiye Muumba wetu. (Ufunuo 4:11) Hilo linamaanisha kwamba tunapaswa kumpenda na kumwabudu yeye peke yake, bila kutumia sanamu, mifano, au picha.​—Soma Isaya 42:8.

      Ibada yetu inapaswa kuwa “takatifu na yenye kukubalika” kwa Yehova. (Waroma 12:1) Hilo linamaanisha kwamba tunapaswa kuishi kulingana na viwango vyake vya maadili. Kwa mfano, wale wanaompenda Yehova wanapenda na kufuata viwango vyake kuhusu ndoa. Pia, wanaepuka mazoea yasiyofaa kama vile kuvuta sigara, kutumia dawa za kulevya au kunywa pombe kupita kiasi.a

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki