-
“Ni Nani Ambaye Anastahili Kufungua Hati-Kunjo?”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
1. Ni nini kinachotukia sasa katika ile njozi ya Yohana?
YA HALI YA JUU MNO! YENYE KUVUVIA HOFU MNO! Ndivyo ilivyo ile njozi yenye kuchochea ya kiti cha ufalme cha Yehova katika mazingira yacho katikati ya taa za moto, makerubi, wazee 24, na bahari ya kioo. Lakini Yohana, ni kitu gani unachofuata kuona? Yohana anakaza macho yake juu ya kitovu chenyewe cha mandhari hii ya kimbingu, akituambia hivi: “Na mimi nikaona katika mkono wa kulia wa Mmoja aketiye juu ya kiti cha ufalme hati-kunjo iliyoandikwa ndani na kwenye upande-pindu, imefungwa kikiki kwa vifungo saba. Na mimi nikaona malaika kabambe akipiga mbiu kwa sauti kubwa: ‘Ni nani ambaye anastahili kufungua hati-kunjo na kulegeza vifungo vyayo?’ Lakini wala katika mbingu wala juu ya dunia wala chini ya dunia hakukupatikana hata mmoja anayeweza kufungua hati-kunjo hiyo au kutazama ndani yayo. Na mimi nikabubujisha machozi mengi kwa sababu hakuna mmoja aliyepatikana kuwa anastahili kufungua hati-kunjo hiyo au kutazama ndani yayo.”—Ufunuo 5:1-4, NW.
-
-
“Ni Nani Ambaye Anastahili Kufungua Hati-Kunjo?”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
3 Je! yule malaika kabambe atapata mtu anayestahili kufungua hiyo hati-kunjo? Kulingana na Kingdom Interlinear, hati-kunjo iko “juu ya mkono wa kulia” wa Yehova. Hii hudokeza kwamba yeye anaitoa juu ya kiganja chake kilichofunguliwa. Lakini inaonekana kwamba hakuna mmoja katika mbingu au juu ya dunia anayestahili kupokea na kufungua hati-kunjo hiyo. Wala hata chini ya dunia, miongoni mwa watumishi wa Mungu ambao wamekufa, hakuna yeyote aliye na sifa zinazofaa kupokea heshima hii ya juu sana. Si ajabu kwamba Yohana anaonekana amefadhaika! Pengine yeye hatajifunza kamwe vile “vitu ambavyo lazima vitukie.” Vilevile katika siku yetu, watu wa Mungu waliopakwa mafuta wamengojea kwa hamu sana Yehova apeleke nuru yake na ukweli juu ya Ufunuo. Hili angefanya kwa mwendeleo katika wakati uliowekwa wa utimizo wa unabii huo, ili aongoze watu wake katika njia ya “wokovu mtukufu.”—Zaburi 43:3, 5, NW.
-