Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Kristo
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Atangazwa Kuwa Mwadilifu na Mwenye Kustahili. Kwa mwendo wake wote wa maisha ya utimilifu kwa Mungu, kutia ndani dhabihu yake, Yesu Kristo alitimiza lile “tendo moja la kutetewa kuwa haki” ambalo lilimthibitisha kuwa anastahili kutumikia mbinguni akiwa Mfalme-Kuhani aliyetiwa mafuta wa Mungu. (Ro 5:17, 18) Kupitia ufufuo wake kutoka kwa wafu hadi kwenye uzima akiwa Mwana wa Mungu wa kimbingu, “alitangazwa kuwa mwadilifu katika roho.” (1Ti 3:16) Viumbe vya kimbingu vilimtangaza kuwa “anastahili kupokea uwezo na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka,” akiwa kama simba kwa ajili ya haki na hukumu na pia kama mwana-kondoo katika kujitoa mwenyewe kama dhabihu ya kuokoa wengine. (Ufu 5:5-13) Alikuwa ametimiza kusudi lake la msingi la kutakasa jina la Baba yake. (Mt 6:9; 22:36-38) Alifanya hivyo, si kwa kulitumia jina hilo tu, bali pia kwa kumfunua Mtu linayewakilisha, akaonyesha sifa bora sana za Baba yake—upendo wake, hekima, haki, na nguvu—na kuwezesha watu wajue au kujionea mambo ambayo jina la Mungu linawakilisha. (Mt 11:27; Yoh 1:14, 18; 17:6-12) Na zaidi ya yote, alifanya hivyo kwa kutegemeza enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote mzima, akaonyesha kwamba serikali yake mwenyewe ya Ufalme ingetegemea kabisa Chanzo hicho Kikuu Zaidi cha mamlaka. Kwa hiyo ingeweza kusemwa hivi kumhusu: “Mungu ni kiti chako cha ufalme milele.”—Ebr 1:8.

  • Roho
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Kwenye Ufunuo 1:4 “zile roho saba” za Mungu zinatajwa ni kama kwamba ziko mbele ya kiti chake cha enzi, na kisha jumbe saba zinatolewa, kila mmoja ukimalizia kwa onyo juu ya ‘kusikia yale ambayo roho inayaambia makutaniko.’ (Ufu 2:7, 11, 17, 29; 3:6, 13, 22) Jumbe hizo zina matamko ya hukumu yenye kupenya moyoni na ahadi za thawabu kwa ajili ya uaminifu. Mwana wa Mungu anaonyeshwa kuwa ana hizi “roho saba za Mungu” (Ufu 3:1); nazo zinatajwa kana kwamba ni “taa saba za moto” (Ufu 4:5), na pia kama macho saba ya mwana-kondoo anayechinjwa, “macho ambayo yanamaanisha roho saba za Mungu ambazo zimetumwa katika dunia nzima.” (Ufu 5:6) Kwa kuwa saba inatumiwa kuwa kiwakilishi cha ukamilifu katika maandishi mengine ya kinabii (ona NUMBER, NUMERAL), inaonekana kwamba hizi roho saba zafananisha uwezo kamili wa kimatendo wa kuona, kutambua, au kugundua wa Yesu Kristo aliyetukuzwa, Mwana-Kondoo wa Mungu, ambao unamwezesha kuikagua dunia yote.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki