-
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya BwanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
17. Hilo tetemeko la dunia kubwa linaathirije jua, mwezi, na nyota?
17 Kama vile Yohana aendeleavyo kuonyesha, tetemeko la dunia kubwa linaandamana na matukio yenye kuogofya ambayo yanahusu hata mbingu. Yeye anasema: “Nalo jua likawa jeusi kama gunia la nywele, na mwezi mzima wote ukawa kama damu, na nyota zote za mbingu zikaanguka kwenye dunia, kama vile wakati mtini unapotikiswa na upepo mkali hurusha tini zao zisizoiva.” (Ufunuo 6:12b, 13, NW) Ni kituko chenye kugutusha kama nini! Je! wewe unaweza kuwazia giza lenye kuogopesha ambalo lingetokea kama unabii huo ungetimizwa kihalisi? Hakungekuwa tena na nuru ya jua yenye joto na yenye kufariji mchana! Hakungekuwa tena na nuru ya mwezi ya kirafiki na yenye rangi ya fedha usiku! Na zile miriadi za nyota hazingemetameta dhidi ya kisetiri-nyuma cha kimahameli cha anga. Badala ya hivyo, kungekuwa na weusi ti, wenye baridi, usiokoma.—Linga Mathayo 24:29.
-
-
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya BwanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
17. Hilo tetemeko la dunia kubwa linaathirije jua, mwezi, na nyota?
17 Kama vile Yohana aendeleavyo kuonyesha, tetemeko la dunia kubwa linaandamana na matukio yenye kuogofya ambayo yanahusu hata mbingu. Yeye anasema: “Nalo jua likawa jeusi kama gunia la nywele, na mwezi mzima wote ukawa kama damu, na nyota zote za mbingu zikaanguka kwenye dunia, kama vile wakati mtini unapotikiswa na upepo mkali hurusha tini zao zisizoiva.” (Ufunuo 6:12b, 13, NW) Ni kituko chenye kugutusha kama nini! Je! wewe unaweza kuwazia giza lenye kuogopesha ambalo lingetokea kama unabii huo ungetimizwa kihalisi? Hakungekuwa tena na nuru ya jua yenye joto na yenye kufariji mchana! Hakungekuwa tena na nuru ya mwezi ya kirafiki na yenye rangi ya fedha usiku! Na zile miriadi za nyota hazingemetameta dhidi ya kisetiri-nyuma cha kimahameli cha anga. Badala ya hivyo, kungekuwa na weusi ti, wenye baridi, usiokoma.—Linga Mathayo 24:29.
-
-
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya BwanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
20. Ni tokeo gani lenye kuhofisha linalongojea huu mfumo wa mambo wakati tetemeko la dunia kubwa linapopiga?
20 Kwa njia iyo hiyo, wakati tetemeko la dunia kubwa linapopiga, mfumo wote huu wa ulimwengu utagharikishwa katika tamausho la giza tititi. Vile vimeti viangavu, vyenye kung’aa vya mfumo wa kidunia wa Shetani havitatoa miale ya tumaini. Tayari leo, viongozi wa kisiasa wa dunia, hasa katika Jumuiya ya Wakristo, wana sifa mbaya sana kwa sababu ya ufisadi wao, kusema uwongo na mtindo wao wa maisha wa utovu wa adili. (Isaya 28:14-19) Hawawezi kuitibariwa tena. Nuru yao yenye kusinzia itapatwa na giza kabisa Yehova atekelezapo hukumu. Uvutano wao ulio kama mwezi juu ya mambo ya dunia utafunuliwa kuwa umetiwa damu, wenye kuleta kifo. Nyota zao mashuhuri za kilimwengu zitazimwa kama vimondo viangukavyo ghafula na zitatawanywa kama tini zisizoiva katika upepo-dhoruba wenye kuvuma. Tufe letu lote litatetemeka chini ya “dhiki kubwa kama ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa, la, wala haitatukia tena.” (Mathayo 24:21, NW) Lo! ni tazamio lenye kujaa hofu kama nini!
-