Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutia Muhuri Israeli wa Mungu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 6. Ni nani anayeambia malaika wazuie pepo nne, na hilo linaruhusu wakati kwa ajili ya nini?

      6 Yohana anaendelea kueleza jinsi baadhi ya watu wanavyotiwa alama kwa ajili ya kuokoka, akisema: “Na mimi nikaona malaika mwingine akipanda juu kutoka kwenye zukio la jua, akiwa na muhuri wa Mungu anayeishi; na yeye alilia kwa sauti kubwa kwa wale malaika wanne ambao kwao ruhusa ilipewa ya kudhuru dunia na bahari, akisema: ‘Msidhuru dunia au bahari au miti, mpaka baada ya sisi tuwe tumetia muhuri watumwa wa Mungu wetu katika vipaji vya nyuso zao.’”—Ufunuo 7:2, 3, NW.

  • Kutia Muhuri Israeli wa Mungu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 8. Kutia muhuri ni nini, nako kulianza wakati gani?

      8 Huku kutia muhuri ni nini, na hawa watumwa wa Mungu ni nani? Kutia muhuri huku kulianza katika Pentekoste 33 W.K. wakati Wakristo Wayahudi wa kwanza walipopakwa mafuta kwa roho takatifu. Baadaye, Mungu aliendelea kuita na kupaka mafuta “watu wa mataifa.” (Warumi 3:29; Matendo 2:1-4, 14, 32, 33; 15:14, NW) Mtume Paulo aliandika juu ya Wakristo wapakwa-mafuta wakiwa na uhakikisho wa kwamba wao ‘ni wa Kristo’ na akaongeza kwamba Mungu “pia ametia muhuri wake juu yetu na ametupa sisi dalili ya kitu ambacho kitakuja, yaani, roho, katika mioyo yetu.” (2 Wakorintho 1:21, 22; linga Ufunuo 14:1, NW.) Hivyo, wakati watumwa hawa wanapolelewa kuwa wana wa kiroho wa Mungu, wanapokea dalili yenye kutangulia urithi wao wa kimbingu—muhuri au rehani. (2 Wakorintho 5:1, 5; Waefeso 1:10, 11) Ndipo wanapoweza kusema: “Roho yenyewe hutoa ushuhuda pamoja na roho yetu kwamba sisi tu watoto wa Mungu. Ikiwa, basi, sisi ni watoto, sisi ni warithi pia: warithi kweli kweli wa Mungu, lakini warithi washirika pamoja na Kristo, iwapo sisi tunateswa pamoja ili kwamba sisi tuweze pia kutukuzwa pamoja.”—Waroma 8:15-17, NW.

      9. (a) Ni uvumilivu gani unaotakwa upande wa mabaki ya wana wa Mungu waliozaliwa kwa roho? (b) Kutahiniwa kwa wale wapakwa-mafuta kutaendelea mpaka lini?

      9 “Iwapo sisi tunateswa pamoja”—hiyo inamaanisha nini? Ili kupokea taji la uhai, Wakristo wapakwa-mafuta lazima wavumilie, wakiwa waaminifu mpaka kifo. (Ufunuo 2:10) Si shauri la ‘wakiisha okolewa, wanaokolewa daima.’ (Mathayo 10:22; Luka 13:24) Badala ya hivyo, wao wanapewa onyo hili la upole: “fanyeni yoteyote mwezayo mfanye kuitwa na kuchaguliwa kwa nyinyi kuwe hakika kwa ajili yenu wenyewe.” Kama vile mtume Paulo, mwishowe kabisa ni lazima wao waweze kusema: “Mimi nimepiga vita nzuri, mimi nimekimbia katika shindano mpaka mwisho, mimi nimeshika imani.” (2 Petro 1:10, 11; 2 Timotheo 4:7, 8, NW) Hivyo hapa duniani kule kutahiniwa na kupepetwa kwa yale mabaki ya wana wa Mungu waliozaliwa kwa roho lazima kuendelee mpaka Yesu na malaika wanaoandamana naye wawe wamekwisha kuutia kikiki muhuri ‘katika kipaji cha uso’ wa hawa wote, kuwatambulisha kabisa kabisa, bila kutanguka, kuwa “watumwa wa Mungu wetu” waliojaribiwa na waaminifu. Ndipo muhuri unapokuwa alama ya daima. Kwa wazi, wakati pepo nne za dhiki zinapoachiliwa, Waisraeli wote wa kiroho watakuwa wamekwisha tiwa muhuri kabisa kabisa, hata ingawa wachache watakuwa wangali wanaishi katika mnofu. (Mathayo 24:13; Ufunuo 19:7) Hesabu nzima ya washiriki itakuwa imekamilika!—Warumi 11:25, 26.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki