Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ni Nani Wanaoenda Mbinguni?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
    • Ni watu wangapi watakaofufuliwa waishi mbinguni?

      Biblia inaonyesha kwamba watu 144,000 watafufuliwa waishi mbinguni. (Ufunuo 7:4) Katika maono yaliyorekodiwa kwenye Ufunuo 14:1-3 mtume Yohana aliona “Mwana-Kondoo amesimama juu ya Mlima Sayuni, na pamoja naye 144,000.” Katika maono hayo, “Mwana-Kondoo” anawakilisha Yesu aliyefufuliwa. (Yohana 1:29; 1 Petro 1:19) “Mlima Sayuni” unawakilisha cheo cha juu cha Yesu na wale 144,000 watakaotawala naye mbinguni.​—Zaburi 2:6; Waebrania 12:22.

      Wale “walioitwa na waliochaguliwa” ili kutawala na Kristo katika Ufalme wanaitwa “kundi dogo.” (Ufunuo 17:14; Luka 12:32) Hilo linaonyesha kwamba watakuwa wachache kwa kulinganishwa na idadi kamili ya kondoo wa Yesu.​—Yohana 10:16.

  • Ni Nani Wanaoenda Mbinguni?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
    • Maoni yasiyo sahihi: 144,000 inayotajwa katika Ufunuo ni idadi ya mfano, si halisi.

      Ukweli: Ingawa kitabu cha ufunuo kina namba za mfano, baadhi ya namba zinazotajwa ni halisi. Kwa mfano, kinasema kuhusu “majina kumi na mawili ya mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.” (Ufunuo  21:14) Fikiria uthibitisho unaofanya tufikie mkataa kwamba 144,000 ni idadi halisi.

      Ufunuo 7:4 inasema kwamba “hesabu ya wale waliotiwa muhuri, [au waliothibitishwa kuwa wataishi mbinguni ni] 144,000.” Muktadha wa mstari huu unataja kikundi kingine tofauti: “umati mkubwa, ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu.” Watu wanaofanyiza “umati mkubwa” watapata wokovu kutoka kwa Mungu. (Ufunuo 7:9, 10) Ikiwa namba 144,000 ingekuwa ya mfano, ikiwakilisha kikundi kisicho na idadi kamili, basi tofauti kati ya vikundi hivyo viwili haingekuwa wazi.a

      Isitoshe, wale 144,000 wanafafanuliwa kuwa “walinunuliwa kutoka kati ya wanadamu wakiwa matunda ya kwanza.” (Ufunuo 14:4) Maneno “matunda ya kwanza” yanarejelea wawakilishi wachache waliochaguliwa. Yanafafanua vizuri kuhusu wale watakaotawala mbinguni pamoja na Kristo juu ya idadi isiyojulikana ya watu watakaoishi duniani.​—Ufunuo 5:10.

      a Vivyo hivyo Profesa Robert L. Thomas aliandika hivi kuhusu namba 144,000 inayotajwa katika Ufunuo 7:4: “Hiyo ni namba hususa tofauti na idadi isiyojulikana inayotajwa kwenye Ufunuo 7:9. Ikiwa namba [144,000] ni ya mfano basi hakuna namba katika kitabu hicho inayopaswa kuonwa kuwa halisi.”​—Revelation 1-7: An Exegetical Commentary, ukurasa wa 474.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki