-
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 20
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi Sana
1. Baada ya kueleza habari ya kutiwa muhuri kwa wale 144,000, Yohana anaona kikundi gani kingine?
AKIISHA kueleza habari ya kutiwa muhuri kwa 144,000, Yohana anaendelea kuripoti mmojapo mafunuo yenye kutaharakisha zaidi sana katika Andiko lote. Lazima moyo wake uwe uliruka-ruka kwa shangwe alipokuwa akiuripoti, akisema: “Baada ya vitu hivi mimi nikaona, na, tazama! umati mkubwa ambao hakuna binadamu aliyeweza kuhesabu kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na ndimi, wakisimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wamevalia majoho meupe; na kulikuwa na matawi ya mitende katika mikono yao.” (Ufunuo 7:9, NW) Ndiyo, kuzuiliwa kwa zile pepo nne kunaruhusu wakati kwa ajili ya wokovu wa kikundi kingine mbali na washiriki 144,000 wa Israeli wa kiroho: umati mkubwa wa lugha nyingi, wa kimataifa.a—Ufunuo 7:1.
2. Waelezaji wa kilimwengu wameelezaje umati mkubwa, na hata Wanafunzi wa Biblia zamani walionaje kikundi hiki?
2 Waelezaji wa kilimwengu wamefasiri huu umati mkubwa kuwa watu wa mnofu wasio Wayahudi ambao wameongolewa kwenye Ukristo au kuwa Wakristo wafia-imani wanaoelekea mbinguni. Zamani, hata Wanafunzi wa Biblia waliwaona kuwa jamii ya pili ya kimbingu, kama ilivyotajwa katika 1886 katika Buku I la Studies in the Scriptures, The Divine Plan of the Ages: “Wao wanapoteza zawadi ya kiti cha ufalme, na ile asili ya kimungu, lakini mwishowe watafikia uzawa wakiwa viumbe wa roho wa hali ya chini zaidi ya asili ya kimungu. Ingawa hawa ni wakfu kikweli, wao wanashindwa na roho ya ulimwengu kwa kadiri ya kwamba wao wanakosa kutoa maisha yao kuwa dhabihu.” Hata karibuni zaidi kama 1930, hilo wazo lilitolewa katika Light, Kitabu cha Kwanza: “Wale wanaojumlika kuwa huu umati mkubwa wanashindwa kuitikia mwaliko wa kuwa mashahidi wenye bidii kwa ajili ya Bwana.” Ilielezwa kuwahusu kuwa kikundi cha wenye uadilifu wa kujifanyia wenyewe waliokuwa na maarifa ya ukweli lakini walifanya kidogo sana kuuhubiri. Walipaswa kwenda mbinguni wakiwa jamii ya pili ambayo haingeshiriki kutawala pamoja na Kristo.
3. (a) Ni tumaini gani walilotolewa wengine wa wale wenye mioyo inayofaa ambao baadaye walikuwa wenye bidii katika kazi ya kuhubiri? (b) Katika 1923 Mnara wa Mlinzi ulielezaje mfano wa kondoo na mbuzi?
3 Hata hivyo, kulikuwako wengine walioshirikiana na Wakristo wapakwa-mafuta ambao baadaye walikuwa wenye bidii zaidi sana katika kazi ya kuhubiri. Wao hawakuwa na tamaa za kwenda mbinguni. Kweli kweli, tumaini lao lilipatana na kichwa cha hotuba iliyotolewa na Mashahidi wa Yehova kuanzia 1918 kufika 1922. Mwanzoni kabisa, hiyo ilikuwa “Ulimwengu Umekoma—Mamilioni Wanaoishi Sasa Hawatakufa Kamwe.”b Upesi baada ya hapo gazeti Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 1923, lilieleza mfano wa Yesu wa kondoo na mbuzi (Mathayo 25:31-46), likataarifu: “Kondoo huwakilisha vikundi vyote vya mataifa, si vilivyozaliwa kwa roho lakini vyenye mwelekeo wa uadilifu, ambavyo kiakili hukiri Yesu Kristo kuwa Bwana na ambavyo hutazamia na kutumaini wakati ulio bora chini ya utawala wake.”
4. Nuru kuhusu jamii ya kidunia ilipataje kuwa nyangavu zaidi katika 1931? katika 1932? katika 1934?
4 Miaka kadhaa baadaye, katika 1931, Vindication, Kitabu cha Kwanza, kilizungumzia Ezekieli sura ya 9 kikitambulisha wale watu wenye kutiwa alama juu ya kipaji cha uso kwa ajili ya kuhifadhiwa kwenye mwisho wa ulimwengu kuwa kondoo wa huo mfano wa juu. Vindication, Kitabu cha Tatu, kilichotolewa 1932, kilieleza habari ya unyoofu wa mwelekeo wa moyoni wa mtu asiye Mwisraeli, Yehonadabu, aliyejiunga na Mfalme mpakwa-mafuta, Yehu Mwisraeli katika gari lake akaenda naye akaone bidii ya Yehu katika kufisha wanadini bandia. (2 Wafalme 10:15-17) Kitabu hicho kilitoa elezo hili: “Yehonadabu aliwakilisha au akatangulia kuweka kivuli cha jamii ya watu ambao wako duniani leo katika wakati ambao kazi ya Yehu [ya kujulisha wazi hukumu za Yehova] inaendelea, ambao ni wa nia njema, hawapatani na tengenezo la Shetani, ambao wanachukua msimamo wao katika upande wa uadilifu, na ndio ambao Bwana atahifadhi hai wakati wa Har–Magedoni awachukue kupitia taabu hiyo, na kuwapa uhai wa milele duniani. Hao wanajumlika kuwa ‘jamii ya kondoo.’ Katika 1934 Mnara wa Mlinzi ulieleza wazi kwamba Wakristo hawa walio na matumaini ya kidunia wapaswa wajiweke wakfu kwa Yehova na wabatizwe. Nuru kuhusu hii jamii ya kidunia ilikuwa iking’aa kwa uangavu zaidi na zaidi.—Mithali 4:18.
5. (a) Ni utambulisho gani wa umati mkubwa uliofanywa katika 1935? (b) Wakati J. F. Rutherford katika 1935 alipouliza wanamkusanyiko waliokuwa na tumaini la kuishi milele duniani wasimame, kulitukia nini?
5 Ule uelewevu wa Ufunuo 7:9-17 ulikuwa sasa unakaribia kububujika pamoja na uangavu wao wote wenye kumeremeta! (Zaburi 97:11) Kwa kurudiarudia gazeti Mnara wa Mlinzi lilikuwa limeonyesha tumaini la kwamba mkusanyiko mmoja uliokuwa umeratibiwa Mei 30 kufika Juni 3, 1935, katika Washington D.C., U.S.A., ungekuwa “faraja halisi na manufaa” kwa wale waliotolewa picha na Yehonadabu. Hivyo ndivyo ilivyokuwa! Katika hotuba yenye kusisimua juu ya “Mkutano Mkubwa” iliyotolewa kwa wanamkusanyiko wapatao 20,000, J. F. Rutherford, ambaye wakati huo alikuwa akielekeza kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote, alitoa uthibitisho wa Kimaandiko kwamba kondoo wengine wa ki-siku-hizi ni jamii ile ile ya umati mkubwa wa Ufunuo 7:9. Kwenye upeo wa hotuba hii, msemaji huyo aliuliza: “Wale wote ambao wana tumaini la kuishi milele juu ya dunia tafadhali mnaweza kusimama?” Sehemu kubwa ya hadhirina ilipokuwa ikisimama, msemaji alitangaza: “Tazameni! Mkutano mkubwa!” Kukawa na kimya, kikifuatwa na vigelegele vyenye mngurumo. Ilifurahi kama nini jamii ya Yohana—na pia kikundi cha Yehonadabu! Keshoye, Mashahidi wapya 840 walibatizwa, walio wengi zaidi wa hawa wakidai kuwa wa huo umati mkubwa.
Kuthibitisha Utambulisho wa Umati Mkubwa
6. (a) Ni kwa nini sisi tunaweza kuelewa waziwazi kwamba umati mkubwa ni kikundi cha ki-siku-hizi cha Wakristo walio wakfu ambao wanatumaini kuishi milele duniani? (b) Yale majoho meupe ya huo umati mkubwa yanafananisha nini?
6 Sisi tunaweza kutaarifuje tukiwa na uhakika sana hivyo kwamba ule umati mkubwa ni kikundi hiki cha ki-siku-hizi cha Wakristo waliojiweka wakfu ambao wanatumaini kuishi milele juu ya dunia ya Mungu? Wakati uliotangulia, Yohana alikuwa ameona katika njozi kikundi cha kimbingu ‘ambacho kilinunuliwa kwa ajili ya Mungu kutoka kila kabila na ulimi na vikundi vya watu na taifa.’ (Ufunuo 5:9, 10, NW) Umati mkubwa una chanzo kinachofanana na hicho lakini wanakoenda ni tofauti. Tofauti na Israeli wa Mungu, hesabu yao haikukusudiwa kimbele. Hakuna mtu anayeweza kusema mapema watakuwa wangapi. Majoho yao meupe yameoshwa kwa damu ya yule Mwana-Kondoo, kufananisha kwamba wao wana msimamo wenye uadilifu mbele za Yehova kwa sababu ya imani yao katika dhabihu ya Yesu. (Ufunuo 7:14) Nao wanapungapunga matawi ya mitende, wakimshangilia Mesiya kuwa Mfalme wao.
7, 8. (a) Kule kupungwapungwa kwa matawi ya mitende bila shaka kulimkumbusha mtume Yohana juu ya matukio gani? (b) Ni nini maana ya uhakika wa kwamba hao wa umati mkubwa wanapungapunga matawi ya mitende?
7 Anapotazama katika njozi hii, mawazo ya Yohana lazima yawe yanamrudisha nyuma zaidi ya miaka 60 kwenye juma la mwisho la Yesu duniani katika Nisani 9, 33 W.K., wakati umati ulipokuja makundi makundi ili kumkaribisha Yesu ndani ya Yerusalemu, wao “walichukua matawi ya mitende wakatoka nje kumlaki. Na wao wakaanza kupaaza sauti: ‘Okoa, sisi twaomba wewe! Mbarikiwa ni yeye ambaye anakuja katika jina la Yehova, hata mfalme wa Israeli!’” (Yohana 12:12, 13, NW) Hali moja na hiyo, kule kupungapunga matawi ya mitende na kupaaza sauti upande wa umati mkubwa huonyesha shangwe yao isiyozuilika katika kumkubali Yesu kuwa Mfalme wa Yehova aliyewekwa rasmi.
8 Pasipo shaka, hayo matawi ya mitende na vilio vya kuchachawa pia vinamkumbusha Yohana ile Sikukuu ya Vibanda ya kale ya Israeli. Kwa ajili ya sikukuu hii Yehova aliamuru: “Na ni lazima nyinyi mjichukulie kwa ajili yenu wenyewe katika siku ya kwanza tunda la miti mizuri sana, na matagaa ya mitende na matanzu ya miti yenye matawi na mipopla ya bonde la mvo, na ni lazima nyinyi mshangilie mbele za Yehova Mungu wenu siku saba.” Matawi ya mitende yalitumiwa kuwa alama ya kushangilia. Vibanda vya muda vilikuwa kikumbusha kwamba Yehova alikuwa amewaokoa watu wake kutoka Misri, waishi katika mahema katika jangwa. “Mkazi mgeni na mvulana asiye na baba na mjane” walishiriki hii sikukuu. Waisraeli wote walipaswa ‘wawe si kitu ila wenye kujawa na shangwe.’—Walawi 23:40; Kumbukumbu 16:13-15, NW.
9. Umati mkubwa unajiunga katika kilio gani cha shangwe?
9 Basi, inafaa kwamba, umati mkubwa, ingawa si sehemu ya Israeli wa kiroho, upungepunge matawi ya mitende kwa kuwa wanaonyesha kwa shangwe na asante kwamba ushindi na wokovu hutoka kwa Mungu na Mwana-Kondoo kama Yohana anavyoona hapa: “Nao hufuliza kulia kwa sauti kubwa, kusema: ‘Wokovu wetu ni kwa Mungu wetu, ambaye ameketi juu ya kiti cha ufalme, na kwa Mwana-Kondoo.’” (Ufunuo 7:10, NW) Ijapokuwa wao wametengwa kutoka vikundi vyote vya kikabila, huo umati mkubwa unalia kwa hiyo “sauti kubwa” moja tu. Wao wanawezaje kufanya hivi, wajapokuwa ni wa mataifa na lugha mbalimbali?
10. Umati mkubwa unaweza kuliaje kwa umoja kwa “sauti kubwa” moja ijapokuwa ni wa mataifa na lugha mbalimbali?
10 Huu umati mkubwa ni sehemu ya tengenezo la mataifa mengi ambalo ndilo pekee lina umoja kweli kweli duniani leo. Wao hawana viwango tofauti-tofauti kwa nchi tofauti-tofauti bali wanatumia kwa ajili ya upatani kanuni za Biblia zinazofaa kokote wanakoishi. Wao hawajiingizi katika harakati za kitaifa, zenye kutaka mapinduzi bali wao ‘wamefua panga zao zikawa majembe ya plau.’ (Isaya 2:4, NW) Wao hawana mgawanyiko wa mafarakano au vikundi vya kidini, hivi kwamba wanapaaza sauti zilizovurugika au jumbe za pamoja zenye kupingana-pingana kama zinavyofanya dini za Jumuiya ya Wakristo; wala wao hawaachii jamii ya viongozi wa kidini wenye kulipwa mshahara wafanye kusifu kwa ajili yao. Wao hawapaazi sauti kwamba wokovu wao hutoka kwa roho takatifu kwa kuwa wao si watumishi wa kamungu ka utatu. Katika maeneo ya kijiografia 200 kuzunguka dunia, wao wana umoja katika kuita juu ya jina la Yehova wanaposema lugha safi ya ukweli. (Sefania 3:9) Kwa kufaa, wao wanakiri peupe kwamba wokovu wao unakuja kutoka kwa Yehova Mungu wa wokovu, kupitia Yesu Kristo, Wakili Mkuu Wake wa wokovu.—Zaburi 3:8; Waebrania 2:10.
11. Tekinolojia ya ki-siku-hizi imesaidiaje wale wa umati mkubwa kufanya sauti yao kubwa iwe kubwa hata zaidi?
11 Tekinolojia ya ki-siku-hizi imesaidia kufanya sauti kubwa ya umati mkubwa wenye umoja ivume kwa ukubwa hata zaidi. Hakuna kikundi kinginecho cha kidini duniani ambacho kina uhitaji wa kuchapisha misaada ya kujifunza Biblia katika lugha zaidi ya 400, kwa maana hakuna kikundi kinginecho ambacho kinapendezwa na kufikia vikundi vyote vya watu wa dunia kwa ujumbe mmoja wenye umoja. Kama msaada zaidi katika jambo hili, chini ya uangalizi wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova lililopakwa mafuta mfumo uitwao, Multilanguage Electronic Phototypesetting System (MEPS) uliundwa. Kufikia wakati kitabu hiki kilipochapishwa, namna tofauti-tofauti za MEPS zinatumiwa katika maeneo zaidi ya 125 kuzunguka dunia, na jambo hili limesaidia kufanya iwezekane utangazaji sawia wa jarida la mara mbili kwa mwezi, Mnara wa Mlinzi, katika lugha zaidi ya 130. Pia watu wa Yehova wanatangaza kisawia, vitabu kama hiki, kwa lugha kadhaa. Hivyo, Mashahidi wa Yehova, ambao ule umati mkubwa ndio walio wengi sana, wanaweza kila mwaka kugawa mamia ya mamilioni ya vichapo katika lugha zote zinazojulikana vizuri zaidi, wakiwezesha misongamano mingi zaidi ya kutoka makabila yote na lugha wajifunze Neno la Mungu na kuunga sauti zao kwenye ile sauti kubwa ya umati mkubwa.—Isaya 42:10, 12.
Mbinguni au Duniani?
12, 13. Ni katika njia gani umati mkubwa ‘umesimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo’?
12 Sisi tunajuaje kwamba ‘kusimama mbele ya kiti cha ufalme’ hakumaanishi kwamba umati mkubwa umo mbinguni? Kuna ithibati nyingi iliyo wazi juu ya jambo hili. Mathalani, neno la Kigiriki linalotafsiriwa hapa “mbele” (e·noʹpi·on) humaanisha kihalisi “katika [mwono wa]” nalo linatumiwa mara kadhaa kuhusu wanadamu duniani ambao wako “mbele” au “katika mwono wa” Yehova. (1 Timotheo 5:21; 2 Timotheo 2:14; Warumi 14:22; Wagalatia 1:20, NW) Katika pindi moja wakati Waisraeli walipokuwa katika jangwa, Musa alimwambia Haruni hivi: “Sema kwa kusanyiko zima la wana wa Israeli, ‘Njooni karibu mbele za Yehova, kwa sababu yeye amesikia manung’uniko yenu.’” (Kutoka 16:9, NW) Waisraeli hao hawakulazimika kusafirishwa mpaka mbinguni ili wakasimame mbele za Yehova katika pindi hiyo. (Linga Walawi 24:8.) Badala ya hivyo, uko huko jangwani walisimama katika mtazamo wa Yehova, na uangalifu wake ukawa juu yao.
13 Kwa kuongezea, sisi tunasoma hivi: “Wakati Mwana wa binadamu anapowasili katika utukufu wake . . . mataifa yote yatakusanywa mbele ya yeye.”c Jamii ya kibinadamu kwa ujumla haitakuwamo katika mbingu wakati unabii huu unapotimizwa. Bila shaka, wale ambao ‘huondoka kwenda kuingia katika kukatiliwa mbali milele’ hawatakuwamo katika mbingu. (Mathayo 25:31-33, 41, 46, NW) Badala ya hivyo, aina ya binadamu husimama duniani katika mtazamo wa Yesu, naye hugeuza uangalifu wake awahukumu. Hali kadhalika, umati mkubwa uko “mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo” katika maana ya kwamba huo husimama katika mtazamo wa Yehova na Mfalme wake, Kristo Yesu, ambao kutoka kwao unapokea hukumu yenye kupendeleka.
14. (a) Ni nani wanaosimuliwa kuwa wako “kuzunguka kiti cha ufalme” na “juu ya Mlima Sayuni” wa kimbingu? (b) Ingawa umati mkubwa unatumikia Mungu “katika hekalu lake,” ni kwa sababu gani hilo haliwafanyi kuwa jamii ya kikuhani?
14 Wazee 24 na kikundi cha wapakwa-mafuta 144,000 wanasimuliwa kuwa wako ‘kuzunguka kiti cha ufalme cha Yehova pande zote’ na “juu ya Mlima Sayuni” wa kimbingu. (Ufunuo 4:4; 14:1, NW) Umati mkubwa si jamii ya kikuhani nao haufikii cheo hicho kilichokwezwa. Kweli, baadaye unasimuliwa katika Ufunuo 7:15 kuwa unatumikia Mungu “katika hekalu lake.” Lakini hekalu hili halirejezei patakatifu pa ndani zaidi, pale Patakatifu Zaidi Sana. Badala ya hivyo, ni ua wa kidunia wa hekalu la Mungu la kiroho. Neno la Kigiriki na·osʹ, linalotafsiriwa hapa “hekalu,” mara nyingi huwasilisha maana pana ya jengo zima lote lililojengwa kwa ajili ya ibada ya Yehova. Leo, hili ni jengo la kiroho ambalo hutia ndani mbingu na dunia pia.—Linga Mathayo 26:61; 27:5, 39, 40; Marko 15:29, 30; Yohana 2:19-21, New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.
-
-
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 121]
-