Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Umati Mkubwa Unatoa Utumishi Mtakatifu
    Mnara wa Mlinzi—1995 | Februari 1
    • Umati Mkubwa Unatoa Utumishi Mtakatifu

      “Wanamtumikia [“Wanamtolea utumishi mtakatifu,” “NW”] mchana na usiku katika hekalu lake.”—UFUNUO 7:15.

      1. Ni hatua gani kubwa ya uelewevu wa kiroho iliyofikiwa katika 1935?

      KATIKA Mei 31, 1935, kulikuwa na shangwe kuu miongoni mwa wahudhuriaji wa mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika Washington, D.C. Huko, kwa mara ya kwanza, halaiki kubwa (au, umati mkubwa) ya Ufunuo 7:9 (NW) ilitambuliwa wazi kupatana na sehemu yote ya Biblia na kwa kupatana na matukio ambayo tayari yalikuwa yameanza kutukia.

      2. Ni nini kilichoonyesha kwamba watu wenye kuongezeka walikuwa wametambua kwamba Mungu hakuwa amewaita kwa uhai wa kimbingu?

      2 Karibu majuma sita mapema, kwenye mwadhimisho wa Mlo wa Jioni wa Bwana katika makutaniko ya Mashahidi wa Yehova, watu 10,681 kati ya wale waliokuwapo (karibu 1 kwa kila watu 6) hawakushiriki kula mifano ya mkate na divai, na 3,688 kati ya hao walikuwa watangazaji wenye kutenda wa Ufalme wa Mungu. Kwa nini hawakushiriki kula na kunywa mifano? Kwa sababu kwa msingi wa yale waliyojifunza katika Biblia, waling’amua kwamba Mungu hakuwa amewaita kwa uhai wa kimbingu bali kwamba wao washiriki katika maandalizi ya Yehova yenye upendo kwa njia nyingine. Kwa hiyo katika mkusanyiko huo, msemaji alipouliza: “Wale wote walio na tumaini la kuishi milele duniani tafadhali wasimame,” nini kilitokea? Maelfu walisimama, wakifuatwa na mashangilio yaliyofanywa kwa muda mrefu na wasikilizaji.

      3. Kwa nini kutambuliwa kwa halaiki kubwa kuliipa huduma ya shambani nguvu mpya, na Mashahidi walihisije juu ya jambo hili?

      3 Yale ambayo wahudhuriaji walijifunza katika mkusanyiko huo yaliipa huduma nguvu mpya. Wao walikuja kung’amua kwamba sasa, kabla ya mwisho wa mfumo wa kale, si maelfu machache tu bali halaiki kubwa ya watu ingepewa fursa ya kuingia katika mpango wa Yehova kwa ajili ya kuhifadhiwa uhai, ikitazamia kuishi milele katika dunia paradiso. Huo ulikuwa ujumbe wenye kuchangamsha moyo kama nini uliotolewa kwa wapendao kweli! Mashahidi wa Yehova walitambua kwamba kulikuwa na kazi kubwa ya kufanya—kazi yenye shangwe. Miaka mingi baadaye, John Booth, aliyekuja kuwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza, alikumbuka hivi: “Kusanyiko hilo lilitupa mambo mengi ya kushangilia.”

      4. (a) Kwa kadiri gani hasa kumekuwa na kukusanywa kwa umati mkubwa tangu 1935? (b) Ni kwa njia gani wale wa umati mkubwa wanatoa uthibitisho kwamba imani yao ni yenye kutenda?

      4 Katika miaka iliyofuata, idadi ya Mashahidi wa Yehova iliongezeka sana. Ujapokuwa mnyanyaso ambao mara nyingi ulikuwa wenye jeuri waliyotendewa wakati wa Vita ya Ulimwengu 2, idadi yao iliongezeka kwa karibu mara tatu katika mwongo mmoja. Na wale wahubiri 56,153 ambao wamekuwa wakitoa ushahidi wa peupe katika 1935 waliongezeka, kufikia 1994, hadi watangazaji wa Ufalme zaidi ya 4,900,000 katika nchi zaidi ya 230. Wengi sana kati yao wanatazamia sana kutiwa miongoni mwa wale ambao Yehova awapendelea kwa kuwapa uhai mkamilifu katika dunia paradiso. Kwa kulinganishwa na kundi dogo, kwa kweli wao wamekuwa umati mkubwa. Wao si watu wasemao wana imani na kukosa kuionyesha. (Yakobo 1:22; 2:14-17) Hao wote huwaeleza wengine habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu. Je, wewe ni mmoja wa umati huo wenye furaha? Kuwa Shahidi mtendaji ni ishara muhimu, lakini kuna mengi zaidi yahusikayo.

      “Wamesimama Mbele ya Kile Kiti cha Enzi”

      5. Ni nini kinachoonyeshwa na hakika ya kwamba umati mkubwa “wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi”?

      5 Katika njozi aliyopewa mtume Yohana, yeye aliwaona wakiwa “wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 7:9) Kusimama kwao mbele ya kile kiti cha enzi cha Mungu, kama kufafanuliwavyo katika muktadha huu, kwaonyesha kwamba wao watambua kabisa enzi kuu ya Yehova. Huo wahusisha mambo mengi. Kwa mfano: (1) Wao watambua haki ya Yehova ya kuamulia watumishi wake yaliyo mema na yaliyo mabaya. (Mwanzo 2:16, 17; Isaya 5:20, 21) (2) Wao husikiliza Yehova asemapo nao kupitia Neno lake. (Kumbukumbu la Torati 6:1-3; 2 Petro 1:19-21) (3) Wao wathamini umaana wa kunyenyekea wale ambao Yehova amewapa amana ya uangalizi. (1 Wakorintho 11:3; Waefeso 5:22, 23; 6:1-3; Waebrania 13:17) (4) Ingawa hawajakamilika, wao hujitahidi kuitikia mwelekezo wa kitheokrasi kwa utayari kutoka moyoni bali si kwa manung’uniko. (Mithali 3:1; Yakobo 3:17, 18) Wao wako mbele ya kile kiti cha enzi ili kutoa utumishi mtakatifu kwa Yehova, ambaye wanamstahi na kumpenda sana. Kwa habari ya huu umati mkubwa, ‘kusimama’ kwao mbele ya kile kiti cha enzi kwaonyesha ukubali wa Yule aketiye juu ya kiti cha enzi. (Linganisha Ufunuo 6:16, 17.) Ukubali huo wategemea nini?

      “Wamevikwa Mavazi Meupe”

      6. (a) Ni nini kinachomaanishwa na umati mkubwa ‘kuvikwa mavazi meupe’? (b) Umati mkubwa unapataje msimamo mwadilifu mbele ya Yehova? (c) Ni kwa kadiri gani imani katika damu iliyomwagwa ya Kristo huwa na uvutano juu ya maisha za umati mkubwa?

      6 Ufafanuzi wa mtume Yohana wa kile alichoona wasema kwamba washiriki wa huu umati mkubwa “wamevikwa mavazi meupe.” Mavazi hayo meupe yaonyesha msimamo wao safi, ulio mwadilifu mbele ya Yehova. Walipataje msimamo huo? Tayari tumeona kwamba katika njozi ya Yohana walikuwa wamesimama “mbele za Mwana-Kondoo.” Wao watambua Yesu Kristo kuwa “Mwana-Kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu.” (Yohana 1:29) Yohana alisikia mmoja wa wazee ambao, katika njozi, alikuwapo katika kiti cha enzi cha Mungu akieleza hivi: “Wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo. Kwa hiyo wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu.” (Ufunuo 7:14, 15) Kwa njia ya mfano, wao wamefua mavazi yao kwa kudhihirisha imani katika damu ya Kristo inayokomboa. Hawakubali tu kwa akili fundisho la Biblia la fidia. Uthamini kwayo huwa na uvutano juu ya jinsi walivyo kindani; na kwa hiyo, ni “kwa moyo” kwamba wao wadhihirisha imani. (Warumi 10:9, 10) Jambo hilo huwa na uvutano sana katika mambo wafanyayo na maisha zao. Katika imani, wao hujitoa wakfu kwa Yehova kwa msingi wa dhabihu ya Kristo, huonyesha wakfu huo kwa utumbukizo ndani ya maji, huishi kikweli kwa kupatana na wakfu wao, na hivyo kuja kuwa na uhusiano uliokubalika na Mungu. Ni pendeleo zuri kama nini—la kutunzwa kwa makini sana!—2 Wakorintho 5:14, 15.

      7, 8. Tengenezo la Yehova limesaidiaje umati mkubwa kudumisha mavazi yao bila kuchafuliwa?

      7 Kwa hangaiko lenye upendo kwa ajili ya hali njema yao ya kudumu, tengenezo la Yehova limeelekeza fikira kwa mitazamo na mienendo iwezayo kutia doa, au kuchafua, mavazi ya mtu ya utambulisho ili kwamba, yajapo maungamo ya nje, mtu huyo asiweze hasa kupatana na ufafanuzi ule wa kiunabii katika Ufunuo 7:9, 10. (1 Petro 1:15, 16) Likikazia kile kilichokuwa kimetangazwa mapema, Mnara wa Mlinzi, katika 1941 na baadaye, lilionyesha kwa kurudia-rudia kwamba lingekuwa kosa kubwa kuhubiri kwa wengine na kisha, katika pindi zisizo za mahubiri, kujiingiza katika mwenendo kama uasherati au uzinzi. (1 Wathesalonike 4:3; Waebrania 13:4) Katika 1947, ilikaziwa kwamba viwango vya ndoa ya Kikristo vya Yehova vyatumika katika nchi zote; bila kujali mambo yanayoruhusiwa na desturi za mahali, wale walioendelea kuwa na wake zaidi ya mmoja hawangekuwa Mashahidi wa Yehova.—Mathayo 19:4-6; Tito 1:5, 6.

      8 Katika 1973, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote walionyeshwa kwamba ni lazima wao wote waepuke kabisa vitendo ambavyo bila shaka vinachafua kama vile matumizi mabaya ya tumbaku, hata wawe wapi—si katika Jumba la Ufalme tu au katika utumishi wa shambani bali pia katika kazi za kimwili au mahali fulani pa pekee ambapo hapaonwi na watu. (2 Wakorintho 7:1) Katika 1987 kwenye mikusanyiko ya wilaya ya Mashahidi wa Yehova, vijana Wakristo walishauriwa sana kwamba ili kudumisha msimamo safi mbele ya Mungu, ni lazima walinde dhidi ya kuishi maisha maradufu. (Zaburi 26: 1, 4) Tena na tena, Mnara wa Mlinzi limeonya dhidi ya sehemu mbalimbali za roho ya ulimwengu kwa sababu “dini [“aina ya ibada,” NW] iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba” yatia ndani kudumisha “kujilinda na dunia pasipo mawaa.”—Yakobo 1:27.

      9. Ni nani hasa atakayepewa kibali mbele ya kiti cha enzi cha Mungu baada ya dhiki kubwa?

      9 Ni wale ambao imani yao inawasukuma kuishi kwa njia ya kubaki safi kiroho na kiadili ambao watakuwa “wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi” wakiwa watumishi wa Mungu wanaokubalika baada ya dhiki kubwa inayokuja. Hao ndio watu ambao hawaanzi tu maisha ya Kikristo bali wanaodumu katika maisha hayo.—Waefeso 4:24.

      “Matawi ya Mitende Mikononi Mwao”

      10. Matawi ya mitende yaliyoonwa na Yohana yakiwa mikononi mwa umati mkubwa yana umaana gani?

      10 Miongoni mwa sehemu zenye kutokeza sana za umati mkubwa, kama ilivyoonwa na mtume Yohana, ni kwamba “wana matawi ya mitende mikononi mwao.” Hilo lina umaana gani? Bila shaka hayo matawi ya mitende yalimkumbusha Yohana juu ya msherehekeo wa Kiyahudi wa tabenakulo, msherehekeo wenye shangwe zaidi katika kalenda ya Kiebrania, uliokuwa ukifanywa baada ya mavuno ya kiangazi. Kwa kupatana na Sheria, matawi ya mitende, pamoja na matawi ya miti mingine, yalikuwa yakitumiwa kutengeneza vibanda vya kukaliwa wakati wa msherehekeo. (Mambo ya Walawi 23:39-40; Nehemia 8:14-18) Pia yalikuwa yakipungwa na waabudu hekaluni wakati wa kuimba Halelu (Zaburi 113-118). Kupungwa kwa matawi ya mitende na umati mkubwa bila shaka pia kulikumbusha Yohana juu ya pindi ambayo Yesu alipanda punda kuingia ndani ya Yerusalemu huku umati wa waabudu wakipunga kwa shangwe matawi ya mitende na kupaaza sauti: “Ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli!” (Yohana 12:12, 13) Kwa hiyo kupungwa kwa matawi ya mitende kwaonyesha kwamba umati mkubwa wakaribisha kwa shangwe Ufalme wa Yehova na Mfalme wake mtiwa-mafuta.

      11. Kwa nini watumishi wa Mungu hupata shangwe kikweli katika kumtumikia Yehova?

      11 Ni roho hiyo ya shangwe ambayo umati mkubwa waonyesha hata sasa wamtumikiapo Yehova. Hiyo haimaanishi kwamba hawakabili magumu au kwamba hawapatwi na huzuni au uchungu. Lakini uradhi unaotokana na kumtumikia na kumpendeza Yehova husaidia kuondoa mambo hayo. Kwa hiyo, mishonari aliyetumika pamoja na mume wake kwa miaka 45 katika Guatemala alisema juu ya hali za kizamani walizokuwa nazo, kazi ngumu na safari zenye hatari zilizokuwa sehemu ya maisha yao walipojaribu kufikia vijiji vya Wahindi kwa ujumbe wa Ufalme. Yeye alimalizia hivi: “Huo ulikuwa wakati wa maisha zetu tulipokuwa na furaha zaidi.” Ingawa alikuwa akihisi matokeo ya uzee na ugonjwa, miongoni mwa mambo aliyoandika mwisho katika kitabu chake yalikuwa maneno haya: “Yalikuwa maisha mazuri, yenye kuthawabisha sana.” Ulimwenguni pote, Mashahidi wa Yehova huhisi vivyo hivyo kuhusu huduma yao.

  • Umati Mkubwa Unatoa Utumishi Mtakatifu
    Mnara wa Mlinzi—1995 | Februari 1
    • “Watu wa Kila Taifa, na Kabila, na Jamaa, na Lugha”

      16. Inathibitishwaje kuwa kweli kwamba umati mkubwa watoka kwa “kila taifa”?

      16 Kutoka mataifa yote, wale wa umati mkubwa wanakuja. Mungu hapendelei, na andalizi la fidia kupitia Yesu Kristo latosha kufunika hao wote. Umati mkubwa ulipotambuliwa Kimaandiko kwa mara ya kwanza katika 1935, Mashahidi wa Yehova walikuwa wanatenda katika nchi 115. Kufikia miaka ya 1990, utafutaji wa wenye mfano wa kondoo ulikuwa umefikia nchi zaidi ya maradufu ya zile nchi za kwanza.—Marko 13:10.

      17. Ni nini kinachofanywa ili kusaidia watu wa kila “kabila, na jamaa, na lugha” wawe ndani ya umati mkubwa?

      17 Katika kutafuta wale watazamiwao kuwa washiriki wa umati mkubwa, Mashahidi wa Yehova hawajaelekeza tu uangalifu kwa vikundi vya kitaifa bali pia wameuelekeza kwa makabila na watu na vikundi vya kikabila vilivyo katika nchi hizo. Ili kufikia watu hawa, Mashahidi huchapisha fasihi ya Biblia katika lugha zaidi ya 300. Hilo lahusisha kuzoeza na kudumisha vikundi vya watafsiri wanaostahili, kuandaa vifaa vya kompyuta vinavyoweza kushughulikia lugha hizi zote, na vilevile kufanya kazi yenyewe ya kuchapisha. Kwa miaka mitano tu iliyopita, lugha 36, zinazosemwa na watu wapatao 98,000,000, zimeongezwa kwenye orodha hiyo. Kwa kuongezea, Mashahidi hujitahidi kuwazuru watu hao mmoja-mmoja ili kuwasaidia kuelewa Neno la Mungu.—Mathayo 28:19, 20.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki