-
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
17. (a) Ni swali gani linalozushwa na mmoja wa wazee 24, na uhakika wa kwamba mzee angeweza kupata mahali pa jibu unadokeza nini? (b) Swali la mzee lilijibiwa lini?
17 Tangu wakati wa mtume Yohana na kundelea mpaka ndani ya siku ya Bwana, Wakristo wapakwa-mafuta walitatizika wakitaka kujua utambulisho wa umati mkubwa. Basi, inafaa kwamba, mmoja wa wazee 24, akiwakilisha wapakwa-mafuta ambao tayari wako katika mbingu, achochee kufikiri kwa Yohana kwa kuzusha swali hususa: “Na katika kuitikia mmoja wa wazee akasema kwangu mimi: ‘Hawa ambao wamevalia majoho meupe, wao ni akina nani na wao walitoka wapi?’ Kwa hiyo mara hiyo mimi nikasema kwa yeye: ‘Bwana yangu, wewe ndiwe mmoja ambaye anajua.’” (Ufunuo 7:13, 14a, NW) Ndiyo, huyo mzee angeweza kupata mahali pa jibu na kumpa Yohana. Hiyo inadokeza kwamba waliofufuliwa wa kikundi cha wazee 24 huenda wakawa wanahusika katika kuwasilisha kweli za kimungu leo. Kwa upande wao, wale wa jamii ya Yohana waliomo duniani walipata kujua utambulisho wa umati mkubwa kwa kutazama kwa ukaribu sana alichokuwa akifanya Yehova katikati yao. Wao walikuwa wenye uharaka wa kuthamini mmeto wenye kutia kiwi wa nuru ya kimungu ambao ulipamba anga la kitheokrasi katika 1935, wakati barabara wa Yehova.
-
-
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
22. Ni habari gani zaidi anayopokea Yohana kuhusu umati mkubwa?
22 Kupitia mfereji wa kimungu Yohana anapokea habari zaidi kuhusu huu umati mkubwa: “Na yeye [mzee] akasema kwangu mimi: ‘Hawa ndio wale ambao huja kutoka dhiki kubwa, na wamefua majoho yao na wameyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo. Hiyo ndiyo sababu wao wako mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu; na wao wanatolea yeye utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake; na Mmoja anayeketi juu ya kiti cha ufalme atatanda hema yake juu yao.’”—Ufunuo 7:14b, 15, NW.
23. Ni nini iliyo dhiki kubwa ambayo umati mkubwa “huja kutoka” hiyo?
23 Katika pindi ya mapema zaidi, Yesu alikuwa amesema kwamba kuwapo kwake katika utukufu wa Ufalme kungefikia upeo katika “dhiki kubwa kama ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa, la, wala haitatukia tena.” (Mathayo 24:21, 22, NW) Katika utimizo wa unabii huo, wale malaika wataachilia pepo nne za dunia zikumbe mfumo wa ulimwengu wa Shetani. Cha kwanza kwenda kitakuwa ni Babuloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini bandia. Kisha, kwenye upeo wa dhiki hiyo, Yesu ataokoa mabaki duniani ya 144,000, pamoja na umati mkubwa wenye watu wengi sana.—Ufunuo 7:1; 18:2.
24. Watu mmoja mmoja wa umati mkubwa wanastahilije kwa ajili ya kuokoka?
24 Watu mmoja mmoja wa umati mkubwa wanastahilije kwa ajili ya kuokoka? Yule mzee anamwambia Yohana kwamba “wamefua majoho yao na wameyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” Kwa maneno mengine, wao wamezoea imani katika Yesu akiwa Mkombozi wao, wamejiweka wakfu kwa Yehova, nao wameonyesha wakfu wao kwa ubatizo wa maji, na ‘wanashika dhamiri njema’ kwa mwenendo wao mnyoofu. (1 Petro 3:16, 21; Mathayo 20:28, NW) Hivyo, wao ni safi na waadilifu katika macho ya Yehova. Na wanajiweka wenyewe “bila doa kutoka ulimwengu.”—Yakobo 1:27, NW.
-