-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2014 | Novemba 15
-
-
Andiko la Ufunuo 11:3 linasema kwamba mashahidi wawili wangetoa unabii kwa siku 1,260. Kisha, simulizi hilo linasema kwamba mnyama-mwitu ‘angewashinda na kuwaua.’ Lakini baada ya “siku tatu na nusu,” mashahidi hao wawili wangerudishwa kwenye uhai, na hilo lingewashangaza watu wote waliokuwa wakiwatazama.—Ufu. 11:7, 11.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2014 | Novemba 15
-
-
Marejeo hayo yanahusianaje na Ufunuo sura ya 11 na Zekaria 4:1-3, na 14? Kila simulizi linawarejelea watiwa-mafuta wa Mungu waliokuwa wakiongoza katika wakati huo mgumu wa majaribu. Basi Ufalme wa Mungu ulipoanza kutawala mbinguni mwaka wa 1914, ndugu watiwa-mafuta waliokuwa wakiongoza wakati huo walitimiza andiko la Ufunuo sura ya 11 kwa kuhubiri kwa miaka mitatu na nusu wakiwa wamevikwa “nguo za magunia.”
-