-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
23. (a) Inakuwaje kwa mashahidi wawili baada ya siku tatu na nusu, na tokeo ni nini kwa maadui wao? (b) Ni lini Ufunuo 11:11, 12 na unabii wa Ezekieli kuhusu Yehova akipulizia bonde la mifupa mikavu ulipopata utimizo wa ki-siku-hizi?
23 Vichapo vya umma vilijiunga na viongozi wa kidini katika kuharibu sifa ya watu wa Mungu, nyusipepa moja ikisema: “Tamati ya The Finished Mystery imetolewa.” Ingawa hivyo, hilo lilikuwa mbali sana na ukweli! Wale mashahidi wawili hawakubaki wakiwa wafu. Tunasoma: “Na baada ya siku tatu na nusu roho ya uhai kutoka kwa Mungu iliingia ndani yao, na wao wakasimama kwa nyayo zao, na hofu kubwa ikaanguka juu ya wale waliokuwa wakiona wao. Na wao wakasikia sauti kubwa kutoka mbingu ikisema kwao: ‘Njooni juu huku.’ Na wao wakaenda juu ndani ya mbingu kwa wingu na maadui wao wakaona wao.” (Ufunuo 11:11, 12, NW) Hivyo, wao walikuwa na ono kama lile la mifupa mikavu katika bonde ambalo Ezekieli alitembelea katika njozi. Yehova alipuliza juu ya hiyo mifupa mikavu, nayo ikawa hai, ikiandaa picha ya uzawa mpya wa taifa la Israeli baada ya miaka 70 ya utekwa katika Babuloni. (Ezekieli 37:1-14) Unabii huo muwili, katika Ezekieli na katika Ufunuo, ulikuwa na utimizo wao wa ki-siku-hizi wenye kutazamisha katika 1919, wakati Yehova aliporudisha mashahidi wake ‘waliokufa’ kwenye uhai wenye kusisimua.
-
-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
25. (a) Ni lini mashahidi wawili walipoambiwa, “Njooni juu huku,” na hilo lilitukiaje? (b) Urudisho wa mashahidi wawili ulikuwa na tokeo gani lenye kushtua jiji kubwa?
25 Jumuiya ya Wakristo ilijaribu tena na tena kurudia ushindi wayo wenye shangwe wa 1918. Ilianza kutumia watu wenye ghasia, kutunga hila kisheria, vifungo vya gereza, hata kunyongwa—lakini wapi! Baada ya 1919 ilikuwa haiwezi kufikia milki ya kiroho ya mashahidi wawili. Katika mwaka huo Yehova alikuwa amesema kwao: “Njooni juu huku,” nao walikuwa wamepanda kwenye hali ya kiroho iliyoinuliwa ambayo maadui wao wangeweza kuwaona lakini hawangeweza kuwagusa. Yohana anaeleza habari ya vile jiji kubwa liliathiriwa na tokeo lenye kushtua la kurudishwa kwao: “Na katika saa hiyo likatukia tetemeko la dunia kubwa, na asilikumi ya jiji ikaanguka; na watu elfu saba wakauawa na hilo tetemeko la dunia, na wanaobaki wakashikwa na kikuli na wakampa Mungu wa mbingu utukufu.” (Ufunuo 11:13, NW) Kulikuwako vurugu kubwa kikweli katika milki ya dini. Ardhi ilionekana inajongeza chini ya viongozi wa makanisa yaliyoimarishwa wakati hiki kikundi cha Wakristo kilichohuishwa kilipoanza kufanya kazi. Asilikumi moja ya jiji lao, kitamathali watu 7,000, waliathiriwa sana sana hivi kwamba wanasemekana kuwa waliuawa.
-