-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
2. (a) Ni ishara gani kubwa ambayo Yohana aona? (b) Maana ya ishara kubwa ilifunuliwa wakati gani?
2 Sasa Yohana aona ishara kubwa—moja ambayo ni ya upendezi wenye kutokeza kwa watu wa Mungu. Inajulisha njozi ya kiunabii yenye kusisimua, ambayo maana yayo ilichapwa kwa mara ya kwanza katika toleo la Machi 1, 1925, la The Watch Tower katika makala iliyokuwa na kichwa “Uzawa wa Taifa” kisha tena katika 1926 katika kitabu Deliverance. Mmeto huu mwangavu wa uelewevu wa Biblia ulipata kuwa alama ya kihistoria katika mwendeleo wa kazi ya Yehova. Kwa hiyo acheni Yohana aeleze drama hii ianzapo kukunjuka: “Na ishara kubwa ilionekana katika mbingu, mwanamke amepambwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya nyayo zake, na juu ya kichwa chake palikuwa na taji la nyota kumi na mbili, na yeye alikuwa na mimba. Na yeye hupiga kilio kikuu katika uchungu mkali wake ili azae.”—Ufunuo 12:1, 2, NW.
-
-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
6. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba huyo mwanamke anayeonwa na Yohana amevaa joho-jua, ana mwezi chini ya nyayo zake, na ana taji la nyota? (b) Ni nini kinachofananishwa na maumivu ya kuzaa ya huyo mwanamke mwenye mimba?
6 Yohana huona mwanamke huyu akiwa amevaa joho-jua na akiwa na mwezi chini ya nyayo zake. Tunapoongeza taji la nyota, anazungukwa kabisa na nuru za kimbingu. Upendeleo wa Yehova hung’aa juu yake mchana na usiku. Lo! ni ufananisho wenye kufaa kama nini wa tengenezo zuri mno la kimbingu la Yehova! Pia yeye ana mimba, anavumilia maumivu ya kuzaa. Vilio vyake vya kutaka msaada wa kimungu huonyesha wakati wake wa kuzaa umekuja. Katika Biblia, mara nyingi maumivu ya kuzaa hufananisha kazi ngumu inayohitajiwa ili kutokeza tokeo la maana. (Linga Zaburi 90:2; Mithali 25:23; Isaya 66:7, 8.) Hapana shaka maumivu ya kuzaa ya aina hii yalilipata tengenezo la Yehova la kimbingu lilipojitayarishia uzawa huu wa kihistoria.
-