-
Malaika Ni Nani na Wanafanya Kazi Gani?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Shetani na roho wake waovu ni nani?
Baadhi ya malaika hawakuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova. Malaika wa kwanza aliyeasi ni yule “anayeitwa Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa.” (Ufunuo 12:9) Shetani alitamani kuwatawala viumbe wengine, basi aliwashawishi wanadamu wa kwanza wamwasi Yehova na baadaye aliwashawishi malaika wengine wajiunge naye katika uasi. Malaika hao waasi wanaitwa roho waovu. Yehova aliamua wafukuzwe kutoka mbinguni waje duniani, nao wataangamizwa.—Soma Ufunuo 12:9, 12.
3. Shetani na roho wake waovu wanatumia mbinu gani kuwapotosha wanadamu?
Shetani na roho waovu huwapotosha watu wengi kupitia zoea baya la kujaribu kuwasiliana na viumbe wa roho. Kwa mfano, baadhi ya watu hutafuta habari kutoka kwa wanajimu, wabashiri, na waganga wa kienyeji. Na wengine hutafuta matibabu yanayohusisha roho waovu. Pia, watu hudanganywa waamini kwamba wanaweza kuzungumza na watu waliokufa. Lakini Yehova anatuonya hivi: “Msiende kwa watu wanaowasiliana na roho, wala msitafute ushauri kutoka kwa wabashiri.” (Mambo ya Walawi 19:31) Anatupatia onyo hilo ili kutulinda dhidi ya Shetani na roho waovu. Wao ni maadui wa Mungu na wanataka kutusababishia madhara.
-
-
Malaika Ni Nani na Wanafanya Kazi Gani?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
6. Shinda vita dhidi ya Shetani na roho wake waovu
Shetani ndiye mtawala wa roho waovu. Lakini kiongozi wa malaika waaminifu anaitwa Mikaeli, ambalo ni jina lingine la Yesu. Mikaeli ana nguvu kadiri gani? Soma Ufunuo 12:7-9, kisha mzungumzie maswali haya:
Ni nani mwenye nguvu zaidi? Je, ni Mikaeli na malaika zake au ni Shetani na roho wake waovu?
Je, unafikiri wafuasi wa Yesu wanapaswa kumwogopa Shetani na roho wake waovu?
Unaweza kushinda vita dhidi ya Shetani na roho wake waovu. Soma Yakobo 4:7, kisha mzungumzie swali hili:
Unawezaje kujilinda dhidi ya Shetani na roho wake waovu?
-
-
Ufalme wa Mungu Umeanza Kutawala!Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Tangu mwaka wa 1914, hali zimekuwaje na watu wamekuwa wakitendaje?
Wanafunzi wa Yesu walimwuliza hivi: “Ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” (Mathayo 24:3) Yesu aliwajibu kwa kutabiri mambo mengi ambayo yangetokea wakati ambapo angeanza kutawala mbinguni akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu. Baadhi ya mambo aliyotaja ni vita, upungufu wa chakula, na matetemeko ya ardhi. (Soma Mathayo 24:7.) Pia, Biblia ilitabiri kwamba tabia za watu katika “siku za mwisho” zingefanya hali ziwe “ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1-5) Hali na tabia hizo zimeonekana waziwazi hasa tangu mwaka wa 1914.
3. Kwa nini hali zimekuwa mbaya sana tangu Ufalme wa Mungu ulipoanza kutawala?
Muda mfupi baada ya kuwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu, Yesu alipigana vita mbinguni dhidi ya Shetani na roho waovu. Shetani alishindwa katika vita hivyo. Biblia inasema: “[alitupwa] chini duniani, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye.” (Ufunuo 12:9, 10, 12) Shetani ana hasira kali kwa sababu anajua kwamba ataangamizwa. Kwa hiyo, anasababisha maumivu na kuteseka ulimwenguni pote. Ndiyo sababu hali ni mbaya sana ulimwenguni! Ufalme wa Mungu utaondoa matatizo hayo yote.
-
-
Ufalme wa Mungu Umeanza Kutawala!Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
5. Ulimwengu umebadilika tangu mwaka wa 1914
Yesu alitabiri kuhusu hali ambazo zingekuwa ulimwenguni wakati ambapo angeanza kutawala. Soma Luka 21:9-11, kisha mzungumzie swali hili:
Umesikia au kujionea nini kati ya mambo hayo yaliyotabiriwa?
Mtume Paulo alifafanua jinsi ambavyo watu wangetenda wakati wa siku za mwisho za utawala wa wanadamu. Soma 2 Timotheo 3:1-5, kisha mzungumzie swali hili:
Umejionea watu wakiwa na tabia gani kati ya tabia hizo?
-