-
Kupambana na Hayawani Wawili Wakali SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
25. (a) Yohana anaelezaje habari za hayawani-mwitu mwingine ambaye yuaja juu kwenye mandhari ya ulimwengu? (b) Ni nini kinachoonyeshwa na pembe mbili za hayawani-mwitu mpya na kutokea kwake katika dunia?
25 Lakini sasa hayawani-mwitu mwingine yuaja juu kwenye mandhari ya ulimwengu. Yohana aripoti: “Na mimi nikaona hayawani-mwitu mwingine akipanda kutoka katika dunia, na alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akaanza kusema kama drakoni. Na anatumia mamlaka yote ya hayawani-mwitu wa kwanza katika mwono wake. Na hufanya dunia na wale wanaokaa ndani yayo waabudu hayawani-mwitu wa kwanza, ambaye dharuba-kifo yake iliponeshwa. Na yeye hufanya ishara kubwa, hivi kwamba amepaswa hata kufanya moto uje chini duniani kutoka katika mbingu katika mwono wa aina ya binadamu.” (Ufunuo 13:11-13, NW) Hayawani-mwitu huyu ana pembe mbili, kuonyesha ushirika wa serikali mbili za kisiasa. Na anaelezwa kuwa anatoka katika dunia, si kutoka katika bahari. Hivyo, anakuja kutoka mfumo wa mambo wa kidunia wa Shetani ambao tayari umeimarishwa. Ni lazima awe serikali ya ulimwengu, ambayo tayari ipo, inayochukua daraka la maana wakati wa siku ya Bwana.
26. (a) Hayawani-mwitu mwenye pembe mbili ni nini, naye anahusianaje na yule hayawani-mwitu wa awali kabisa? (b) Ni katika maana gani pembe za hayawani-mwitu mwenye pembe mbili ni kama za Mwana-kondoo naye yukoje “kama drakoni” anaposema? (c) Watukuzaji wa taifa wanaabudu nini kikweli, nao utukuzaji wa taifa umefananishwa na nini? (Ona kielezi cha chini.)
26 Anaweza kuwa nini? Ni Serikali ya Uliwengu, Uingereza-Amerika—kile kile kichwa cha saba cha hayawani-mwitu wa kwanza lakini katika daraka la pekee! Kumtenga katika njozi hiyo kuwa hayawani-mwitu tofauti hutusaidia sisi kuona kwa wazi zaidi jinsi anavyotenda kwa kujitegemea juu ya jukwaa la ulimwengu. Huyu hayawani-mwitu wa kitamathali mwenye pembe mbili ni mfanyizo wa serikali mbili za kisiasa zilizoko wakati ule ule mmoja ambazo zinajitegemea, lakini zinashirikiana pamoja. Pembe zake mbili “kama mwana-kondoo” hudokeza kwamba hujifanya kuwa mpole na asiyechokoza, akiwa na namna ya serikali iliyotiwa nuru ambayo ulimwengu wote wapaswa kuiendea. Lakini anasema “kama drakoni” kwa kuwa anatumia mbano na vitisho na jeuri ya moja kwa moja wakati wowote namna yake ya utawala isipokubaliwa. Hakutia moyo watu wanyenyekee Ufalme wa Mungu chini ya utawala wa Mwana-Kondoo wa Mungu bali, badala ya hivyo, ni kwa mapendezi ya Shetani, yule drakoni mkubwa. Ametetea migawanyiko ya utukuzaji wa taifa na chuki ambazo hujumlika kuwa ibada kwa hayawani-mwitu wa kwanza.c
-
-
Kupambana na Hayawani Wawili Wakali SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
c Waelezaji wameona kwamba utukuzo wa taifa, kwa kweli, ni dini. Kwa sababu hiyo, watu ambao ni watukuzaji wa taifa kwa kweli wao wanaabudu sehemu ya hayawani-mwitu inayowakilishwa na nchi ambayo katika hiyo wanaishi. Kwa habari ya utukuzaji wa taifa katika United States, sisi tunasoma hivi: “Utukuzaji wa taifa, ukionwa kuwa dini, una mengi yanayohusiana na mifumo mikubwa ya dini za wakati uliopita . . . Mtetea taifa wa kidini wa ki-siku-hizi anaona utegemeo wake ni mungu wake mwenyewe wa kitaifa. Yeye anahisi yuahitaji msaada Wake wenye nguvu. Katika Yeye hutambua mna chimbuko lake mwenyewe la ukamilifu na furaha. Yeye anajitiisha kwake Huyo, kwa maana halisi ya kidini. . . . Taifa linaonwa kuwa la milele, na kifo cha wana walo washikamanifu huongeza tu sifa na utukufu walo usiokufa.”—Carlton J. F. Hayes, kama alivyonukuliwa katika ukurasa 359 wa kitabu What Americans Believe and How They Worship, cha J. Paul Williams.
-