-
Kupambana na Hayawani Wawili Wakali SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
25. (a) Yohana anaelezaje habari za hayawani-mwitu mwingine ambaye yuaja juu kwenye mandhari ya ulimwengu? (b) Ni nini kinachoonyeshwa na pembe mbili za hayawani-mwitu mpya na kutokea kwake katika dunia?
25 Lakini sasa hayawani-mwitu mwingine yuaja juu kwenye mandhari ya ulimwengu. Yohana aripoti: “Na mimi nikaona hayawani-mwitu mwingine akipanda kutoka katika dunia, na alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akaanza kusema kama drakoni. Na anatumia mamlaka yote ya hayawani-mwitu wa kwanza katika mwono wake. Na hufanya dunia na wale wanaokaa ndani yayo waabudu hayawani-mwitu wa kwanza, ambaye dharuba-kifo yake iliponeshwa. Na yeye hufanya ishara kubwa, hivi kwamba amepaswa hata kufanya moto uje chini duniani kutoka katika mbingu katika mwono wa aina ya binadamu.” (Ufunuo 13:11-13, NW) Hayawani-mwitu huyu ana pembe mbili, kuonyesha ushirika wa serikali mbili za kisiasa. Na anaelezwa kuwa anatoka katika dunia, si kutoka katika bahari. Hivyo, anakuja kutoka mfumo wa mambo wa kidunia wa Shetani ambao tayari umeimarishwa. Ni lazima awe serikali ya ulimwengu, ambayo tayari ipo, inayochukua daraka la maana wakati wa siku ya Bwana.
-
-
Kupambana na Hayawani Wawili Wakali SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
27. (a) Ni mwelekeo gani wa hayawani-mwitu mwenye pembe mbili unaoonyeshwa na uhakika wa kwamba yeye anafanya moto ushuke chini kutoka mbinguni? (b) Watu wengi wanaonaje kifani cha ki-siku-hizi cha huyo hayawani-mwitu mwenye pembe mbili?
27 Huyu hayawani-mwitu mwenye pembe mbili hufanya ishara kubwa, hata kufanya moto ushuke kutoka katika mbingu. (Linga Mathayo 7:21-23.) Hii ishara ya pili hukumbusha sisi juu ya Eliya, nabii wa Mungu wa kale ambaye alijitia katika ushindani na manabii wa Baali. Yeye alipoitisha moto ushuke kutoka katika mbingu kwa kufaulu katika jina la Yehova, ulithibitisha kupita shaka lolote kwamba yeye alikuwa nabii wa kweli na kwamba wale manabii wa Baali walikuwa bandia. (1 Wafalme 18:21-40) Kama hao manabii wa Baali, huyo hayawani-mwitu mwenye pembe mbili huhisi kwamba yeye ana vitambulisho vya kuwa nabii. (Ufunuo 13:14, 15; 19:20) Kwani, yeye hudai kwamba amezima kani za uovu katika vita viwili vya ulimwengu, na alishinda ule unaoitwa eti ukomunisti unaokana kuwako kwa mungu! Kweli kweli, wengi, hukiona kifani cha ki-siku-hizi cha hayawani-mwitu mwenye pembe mbili kuwa mlinda uhuru na kibubujiko cha vitu vizuri vya kimwili.
-