-
Mnyama-Mwitu Mwenye Vichwa Saba Anayetajwa Katika Ufunuo Sura ya 13 Anawakilisha Nini?Maswali ya Biblia Yajibiwa
-
-
Biblia inasema kwamba jina au namba ya mnyama-mwitu huyo—666—ni “namba ya mwanadamu.” (Ufunuo 13:17, 18) Maneno hayo yanaonyesha kwamba mnyama anayetajwa katika Ufunuo sura ya 13 ana asili ya kibinadamu, wala si ya roho au roho mwovu.
-
-
Nambari 666 Inamaanisha Nini?Maswali ya Biblia Yajibiwa
-
-
Nambari 666 Inamaanisha Nini?
Jibu la Biblia
Kulingana na kitabu cha mwisho cha Biblia, 666 ndiyo nambari, au jina, la yule mnyama-mwitu aliye na vichwa saba na pembe kumi anayepanda kutoka katika bahari. (Ufunuo 13:1, 17, 18) Mnyama-mwitu huyo anawakilisha mfumo wa kisiasa wa ulimwenguni pote, ambao unatawala juu ya “kila kabila na watu na lugha na taifa.” (Ufunuo 13:7) Jina 666 linaonyesha kwamba kwa maoni ya Mungu mfumo wa kisiasa umeshindwa kabisa. Linaonyeshaje hivyo?
Si kibandiko tu. Kwa kawaida Mungu anapompa mtu au kitu jina linakuwa na maana fulani. Kwa mfano, jina Abramu linamaanisha “Baba Ametukuzwa (Amekwezwa).” Mungu alimpa mwanamume huyo jina Abrahamu linalomaanisha “Baba ya Umati (Halaiki),” wakati ambapo Mungu aliahidi kumfanya Abrahamu “kuwa baba ya umati wa mataifa.” (Mwanzo 17:5) Vivyo hivyo, Mungu alimpa huyo mnyama-mwitu jina 666 kuwa ishara ya sifa zinazomtambulisha.
Nambari sita inaashiria kutokamilika. Mara nyingi, namba hutumiwa kama ishara katika Biblia. Nambari saba huwakilisha ukamili au ukamilifu. Kwa kuwa nambari sita imepungua kwa nambari moja kutoka saba, inaweza kumaanisha kitu ambacho si kamili au kilicho na kasoro machoni pa Mungu, na inaweza kuhusianishwa na maadui wa Mungu.—1 Mambo ya Nyakati 20:6; Danieli 3:1.
Mara tatu ili kutia mkazo. Nyakati nyingine Biblia hukazia jambo kwa kulitaja mara tatu. (Ufunuo 4:8; 8:13) Kwa hiyo jina 666 linakazia kwa msisitizo kwamba Mungu huiona mifumo ya kisiasa inayoongozwa na wanadamu kuwa imeshindwa kabisa. Wanadamu wameshindwa kuleta amani na usalama wa kudumu—mambo ambayo yanaweza kuletwa tu na Ufalme wa Mungu.
-