Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Taarifa za Mteremo” Kutoka Kwenye Apokalipsi
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Desemba 1
    • 3. Huduma ya waziwazi ya Mashahidi wa Yehova yalingana na utume gani?

      3 Kwa kuwa Mashahidi wa Yehova ni watangazaji wa taarifa hizi za mteremo, kwa kweli wao ni wasemaji wa mjumbe wa kimbingu wa mfano ambaye utume wake unatajwa pia katika Ufunuo. “Nikaona malaika mwingine akiruka katika mbingu ya kati, naye alikuwa na habari njema idumuyo milele ili aitangaze kuwa taarifa za mteremo kwa wale wakaao juu ya dunia, na kwa kila taifa na kabila na lugha na watu.” (Ufunuo 14:6) Hiyo “habari njema idumuyo milele” yatia ndani tangazo la kwamba “ufalme [au, utawala] wa ulimwengu” umekuwa “ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake” na kwamba “wakati [wa Yehova] uliowekwa rasmi” umefika wa “kuwaleta kwenye uangamizi wale wanaoiangamiza dunia.” (Ufunuo 11:15, 17, 18) Je, kweli hiyo si habari njema?

  • “Taarifa za Mteremo” Kutoka Kwenye Apokalipsi
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Desemba 1
    • 6. Ono lililoandikwa katika sura ya 4 husaidia watu kuelewa nini?

      6 Sura ya 4 yaandaa ono lenye kutia kicho la kiti cha ufalme cha kimbingu cha Yehova Mungu. Yatuonyesha utukufu wa kuwapo kwa Yehova na pia mpangilio wa utawala wa kimbingu ambao atatumia. Watawala ambao wamevikwa taji, ambao viti vyao vya ufalme vimezunguka kiti kikuu cha ufalme cha ulimwengu, wamsujudu Yehova na kutangaza: “Wewe wastahili, Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako na vikaumbwa.”—Ufunuo 4:11.

      7. (a) Malaika anawaambia wakaao duniani wafanye nini? (b) Ni nini sehemu muhimu ya kazi yetu ya kufundisha watu?

      7 Je, jambo hilo lina maana yoyote kwa watu leo? Ndiyo, bila shaka. Ikiwa wanataka kuishi chini ya Ufalme wa Milenia, ni lazima watii mambo ambayo ‘malaika anayeruka katika mbingu ya kati’ atangaza: “Hofuni Mungu na kumpa utukufu, kwa sababu saa ya hukumu yake imewasili.” (Ufunuo 14:6, 7) Mojawapo ya makusudi makuu ya kazi ya kufundisha watu Biblia inayofanywa na Mashahidi wa Yehova ni kuwasaidia “wale wakaao juu ya dunia” wamjue Yehova na kumwabudu, watambue kwamba yeye ndiye Muumba, na kunyenyekea kwa hiari enzi yake kuu yenye uadilifu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki