-
Kristo Azungumza na MakutanikoMnara wa Mlinzi—2003 | Mei 15
-
-
7, 8. Kutaniko la Efeso lilikuwa na tatizo gani kubwa, nasi tunawezaje kushughulika na hali kama hiyo?
7 Hata hivyo, Wakristo huko Efeso walikuwa na tatizo kubwa. “Nashika hili dhidi yako,” akasema Yesu, “kwamba umeacha upendo uliokuwa nao hapo kwanza.” Washiriki wa kutaniko walihitaji kuchochea tena upendo waliokuwa nao kwa Yehova hapo kwanza. (Marko 12:28-30; Waefeso 2:4; 5:1, 2) Sote tunapaswa kuwa waangalifu tusipoteze upendo tuliokuwa nao kwa Mungu hapo kwanza. (3 Yohana 3) Namna gani ikiwa tunatanguliza tamaa ya kuwa matajiri au kufuatia anasa maishani? (1 Timotheo 4:8; 6:9, 10) Badala ya kuwa na tamaa kama hizo, tunapaswa kuomba msaada wa Mungu kwa bidii ili kusitawisha upendo mwingi kwa Yehova na kushukuru kwa yale ambayo yeye na Mwana wake wametufanyia.—1 Yohana 4:10, 16.
-
-
Kristo Azungumza na MakutanikoMnara wa Mlinzi—2003 | Mei 15
-
-
11. Tunaweza kuwachocheaje wengine wampende Yehova?
11 Waefeso walikuwa wamepoteza upendo waliokuwa nao hapo kwanza, lakini namna gani hali kama hiyo ikianza kutokea kutanikoni? Kila mmoja wetu na awachochee wengine wampende Yehova kwa kuzungumzia njia zake za upendo. Tunaweza kuonyesha shukrani zetu kwa upendo ambao Mungu alionyesha kwa kutoa fidia kupitia Mwana wake mpendwa. (Yohana 3:16; Waroma 5:8) Inapofaa, tunaweza kutaja upendo wa Mungu tunapotoa maelezo ama tunapokuwa na migawo kwenye mikutano. Tunaweza kuonyesha kwamba tunampenda Yehova kwa kulisifu jina lake katika huduma ya Kikristo. (Zaburi 145:10-13) Naam, maneno na matendo yetu yanaweza kuchochea tena au kuimarisha sana upendo ambao kutaniko lilikuwa nao hapo kwanza.
-