-
Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye TamatiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
6. Hutukia nini wakati bakuli la tatu linapomiminwa, na ni maneno gani yanayosikiwa kutoka kwa malaika na kutoka madhabahu?
6 Bakuli la tatu la kasirani ya Mungu kama mpigo wa tatu wa tarumbeta, huathiri machimbuko ya maji matamu. “Na wa tatu akamimina bakuli lake ndani ya mito na vibubujiko vya maji. Na hiyo ikawa damu. Na mimi nikasikia malaika aliye na amri juu ya maji akisema: ‘Wewe, Mmoja ambaye yuko na ambaye alikuwako, Mshikamanifu, u mwadilifu, kwa sababu wewe umekata maamuzi haya, kwa sababu wao walimimina damu ya watakatifu na ya manabii, na wewe umewapa damu wanywe. Wao hustahili hiyo.’ Na mimi nikasikia madhabahu ikisema: ‘Ndiyo, Yehova Mungu, Mweza Yote, ya kweli na ya uadilifu ni maamuzi yako ya hukumu.’”—Ufunuo 16:4-7, NW.
-
-
Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye TamatiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
10. “Malaika aliye na amri juu ya maji” anajulisha nini, na ni ushahidi gani ambao “madhabahu” inaongezea?
10 “Malaika aliye na amri juu ya maji,” yaani, malaika amiminaye bakuli hili juu ya maji, anatukuza Yehova kuwa ndiye Hakimu wa Ulimwengu Wote Mzima, ambaye maamuzi yake ya uadilifu ni kamili. Kwa hiyo, yeye anasema juu ya hukumu hii: “Wao hustahili hiyo.” Pasipo shaka, huyo malaika alijionea mwenyewe umwagaji-damu mwingi na ukatili uliochochewa na mafundisho bandia na falsafa za ulimwengu huu mbovu kwa muda wa maelfu mengi ya miaka. Kwa sababu hiyo, yeye anajua kwamba uamuzi wa hukumu wa Yehova ni wa haki. Hata “madhabahu” ya Mungu inasema kwa mpaazo. Kwenye Ufunuo 6:9, 10, nafsi za wale ambao waliuawa kiimani husemwa kuwa kwenye msingi wa madhabahu hiyo. Kwa hiyo “madhabahu” inaongeza ushahidi wenye nguvu nyingi kwa habari ya haki na uadilifu wa maamuzi ya Yehova.a Hakika, inawafaa wale ambao wamemwaga na kutumia vibaya damu wenyewe wanyweshwe damu kinguvu, kama ufananisho wa Yehova kuwahukumia kifo.
-