-
“Mwana-Mfalme wa Amani” Akabili Har–MagedoniUsalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
-
-
Mataifa Yanakusanywa Kwenye Har–Magedoni
15. (a) Basi, Har–Magedoni ni mahali pa namna gani? (b) Ni Nini kimojapo cha vyanzo vya maenezi ya kisiasa yenye uchafu yanayowakusanya mataifa kwenye vita katika Har–Magedoni?
15 Kwa hiyo Megido palikuwa mahali ambapo vita vya kukata maneno vilipiganwa. Hivyo, kwa kufaa, Har–Magedoni ungekuwa ni uwanja wa vita ambao katika huo mataifa yote ya ulimwengu wa leo yangepiga miguu kuuelekea chini ya majeshi yenye kuchochea yanayosimuliwa kwenye Ufunuo 16:13, 14. Zile “semi zilizoongozwa na mashetani,” (NW) zinazokusanya mataifa ndiyo yale maenezi ya kisiasa ambayo yanatolewa leo kama mkoromo wa vyura, yenye uchafu kama vile chura alivyo mchafu kulingana na maoni ya Biblia. Kimojapo cha vyanzo vya maenezi ya kisiasa hayo yenye uchafu ni lile “joka kubwa jekundu.” Ufunuo 12:1-9 unatambulisha “yule joka” kuwa Shetani yule Ibilisi.
-
-
“Mwana-Mfalme wa Amani” Akabili Har–MagedoniUsalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
-
-
17. Ni nini matokeo ya maenezi ya kisiasa yanayofanana na vyura yanayotoka kwa yule “mnyama”?
17 Mfumo huo wa ulimwengu wa utawala wa kisiasa una maenezi yao ya kisiasa ya kuutofautisha. Nayo maenezi ya kisiasa hayo, yenye mkoromo kama wa vyura, ni usemi ulioongozwa na roho unaotumika pamoja na ule usemi ulioongozwa na roho wa “yule joka” ili kukusanya “wafalme,” au watawala wa kisiasa wa ulimwengu, kwenye “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” itakayopiganwa kwenye Har–Magedoni.
18. (a) Jina Har–Magedoni linaonyesha nini? (b) Mlima ungefananisha nini?
18 Hivyo Har–Magedoni huonyesha hali ya ulimwengu inayohusu vita ya kukata maneno. Inaonyesha ile hali ya upeo wa mambo ya ulimwengu ambayo kwa sababu hiyo watawala wa ulimwengu kwa umoja wanapinga mapenzi ya Mungu, hivi kwamba Mungu analazimika kutenda kwa majeshi yenye kupinga kulingana na kusudi lake. Kwa hiyo wakati ujao utaamuliwa kulingana na matokeo ya mkabiliano huo. Kwenye Megido yenyewe, mahali pale pa kijiografia, hapakuwa na mlima. Lakini, mlima ungefananisha mahali pa kukusanyika penye kutokeza sana ambapo pangeweza kuonekana kwa urahisi kutoka mbali na majeshi yote ya kivita yenye kukusanyika hapo.
19, 20. Jenerali wa majeshi ya Yehova ya kimbingu atatumia mpango gani wa werevu wa vita kwenye Har–Magedoni, na kwa matokeo gani?
19 Kwa miaka kadha Yesu Kristo aliye Jenerali wa majeshi yenye kupiga vita ya Yehova, amekuwa akitazama kukusanyika kwa watawala wa ulimwengu pamoja na majeshi yao yenye kupiga vita kwenye Har–Magedoni. Walakini, yeye hakujaribu kumchagua mfalme ye yote mmoja na majeshi yake ya kivita awapige wakiwa peke yao na hivyo amalize majeshi ya adui kidogokidogo. Tofauti na hilo, yeye anawaruhusu wakati wa kutosha wajikusanye pamoja na kuunganisha majeshi yao yawe jeshi la kivita kubwa zaidi liwezekanalo. Kusudi lake la ujasiri ni kupigana nao wote kwa wakati mmoja!
-