Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nidhamu Inayoweza Kuzaa Tunda Lenye Kuamanika
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Aprili 15
    • wamejitenga na ushirika wa kundi kwa makusudi, Wakristo wanakuwa na himaya ya kutopatwa na maoni ya uchambuzi, ya kukosa uthamini, au hata ya uasi-imani.​—Waebrania 12:15, 16.

      Namna Gani Juu ya Watu wa Ukoo?

      11, 12. (a) Ni nini lililokuwa tokeo juu ya watu wa ukoo wa Kiisraeli wakati mtenda kosa alipokatiliwa nje? (b) Toa kielezi cha manufaa za utii.

      11 Kwa uhakika Mungu anatambua kwamba mara nyingi kutekeleza sheria zake za uadilifu juu ya kukatilia nje watenda makosa kunahusisha ndani watu wa ukoo na kuwaathiri. Kama ilivyotajwa juu, wakati mtenda kosa Mwisraeli alipouawa, hakuna ushirika zaidi wa kijamaa uliokuwa unawezekana. Kwa hakika, ikiwa mwana alikuwa mlevi na mlafi, wazazi wake walipaswa kumleta kwa ajili ya hukumu, na ikiwa yeye alikuwa asiyetubu, wazazi hao walipaswa kushiriki katika kule kumuua kwa haki, ‘kuondolea mbali kilicho kibaya kutoka kati ya Israeli.’ (Kumbukumbu 21:18-21, NW) Wewe unaweza kuthamini kwamba jambo hilo halingekuwa rahisi kwao. Wazia, pia, jinsi wale ndugu, dada, au babu na nyanya za mtenda kosa walivyohisi. Hata hivyo, kuweka kwao ushikamanifu kwa Mungu wao mwadilifu mbele ya shauku ya kijamaa kungeweza kuwaokolea uhai.

      12 Kumbuka kile kisa cha Kora, ambaye alikuwa kiongozi katika uasi dhidi ya uongozi wa Mungu kupitia Musa. Katika haki yake kamilifu, Yehova aliona kwamba ilikuwa lazima Kora afe. Lakini washikamanifu wote walishauriwa hivi: “Nawasihi, ondokeni penye hema za hawa watu waovu, wala msiguse kitu chao cho chote, msiangamizwe katika dhambi” yao. Watu wa ukoo ambao hawakutaka kukubali onyo la Mungu walikufa pamoja na waasi hao. Lakini watu fulani wa ukoo wa Kora walichagua kwa hekima kuwa washikamanifu kwa Yehova, jambo ambalo liliokoa uhai wao na kuongoza kwenye baraka za wakati ujao.​—Hesabu 16:16-33; 26:9-11; 2 Nyakati 20:19.

      13. Wakristo washikamanifu wataitikia jinsi gani kama mshiriki wa jamaa ya pale pale anajitenga na ushirika?

      13 Kukatilia nje kutoka kundi la Kikristo hakuhusishi ndani kifo cha mara hiyo, kwa hiyo vifungo vya kijamaa vinaendelea. Hivyo, mwanamume aliyeoa ambaye ametengwa au anajitenga na ushirika huenda bado akaishi nyumbani pamoja na mke wake Mkristo na watoto waaminifu. Staha kwa hukumu za Mungu na hatua ile ya kundi itasukuma yule mke na watoto kung’amua kwamba kwa mwendo wake, mwanamume huyo alileta mwisho wa ule ukamatano wa kiroho uliokuwa kati yao. Hata hivyo, kwa kuwa kutengwa kwake na ushirika hakukomeshi vifungo vyao vya damu au uhusiano wa ndoa, shauku na shughuli za kikawaida za jamaa zinaendelea.

      14. Ni shauri gani la kimungu linalopasa kuwa na mavutano juu ya uwasiliano wetu na mtu wa ukoo aliyetengwa na ushirika ambaye yuko nje ya jamaa yetu ya pale pale?

      14 Hali hii ni tofauti ikiwa yule ambaye ametengwa au amejitenga na ushirika ni mtu wa ukoo anayeishi nje ya jamaa ile ya pale pale, Labda ingewezekana kuzuia karibu mawasiliano yote pamoja na mtu huyo wa ukoo. Hata kama kuna mambo fulani ya kijamaa yanayotaka mawasiliano, kwa uhakika yanapasa kuwekwa katika kadiri ndogo kabisa, kupatana na ile kanuni ya kimungu: “Ninyi mwache kabisa kuchangamana katika ushirika pamoja na ye yote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa [au mwenye hatia ya dhambi nyingine nzito sana], . . . hata msiwe mnakula pamoja na mtu huyu.”​—1 Wakorintho 5;11, NW.

      15. Ni jinsi gani watu wa ukoo wanavyoweza kuongoza mavutano ya hisia za moyoni katika visa kama hivyo? (Zaburi 15:1-5; Marko 10:29, 30)

      15 Inaeleweka kwamba huenda hilo likawa jambo gumu kwa sababu ya hisia za moyoni na vifungo vya kijamaa, kama vile upendo wa akina babu na nyanya kwa wajukuu wao. Hata hivyo. huo ni mtihani wa ushikamanifu kuelekea Mungu, kama vile ilivyotajwa na yule dada aliyenukuliwa katika ukurasa 26. Ye yote ambaye anahisi sikitiko kubwa na umizo ambalo limesababishwa hivyo na yule mtu wa ukoo aliyetengwa na ushirika anaweza kutiwa moyo na kielelezo kilichowekwa na watu fulani wa ukoo wa Kora.​—Zaburi 84:10-12.b

      Ule Uamuzi wa Mahakama

      16-18. Ni uamuzi gani ambao ulifikiwa katika ile kesi ya mahakama iliyotajwa mapema zaidi, na mahakama ilitoa maoni gani ya ziada juu ya kesi hiyo?

      16 Huenda wewe ukapenda kujua tokeo la ile kesi ya mahakama iliyohusu mwanamke mmoja ambaye aliudhika kwa sababu waliokuwa wazoeani wake hapo kwanza hawakutaka kuongea naye baada ya yeye kuchagua kuikataa imani, akijitenga na ushirika wa kundi.

      17 Kabla ya kesi ile kwenda kusikilizwa, mahakamani fulani kuu ya wilaya ilitoa kwa muhtasari hukumu iliyokuwa dhidi ya mwanamke huyo. Hukumu hiyo ilitegemea wazo la kwamba mahakama hazijiingizi katika mambo ya nidhamu ya kikanisa. Ndipo mwanamke huyo akaomba rufani. Uamuzi uliotolewa kwa mkubaliano wa ujumla wa mahakama kubwa ya rufanic ulitegemea kuhusishwa kwa upana zaidi kwa haki za Sheria Iliyosahihishwa (ya Katiba ya United States): “Kwa sababu zoea la kuepuka watu ni sehemu ya imani ya Mashahidi wa Yehova, sisi tunapata kwamba ule uandalizi wa Katiba ya United States wa ‘kuendesha mambo kwa uhuru‘ . . . unazuia [mwanamke huyo] asikae miongoni mwao. Washtakiwa wana pendeleo lenye himaya ya katiba la kujitia katika lile zoea la kuepuka watu. Kulingana na hilo, sisi tunathibitisha ule” uamuzi wa mapema zaidi wa mahakama ya wilaya.

      18 Maoni ya mahakama ya rufani yaliendelea kusema: “Kuepuka watu ni zoea ambamo Mashahidi wa Yehova wanajitia kwa kufuatana na fasiri yao ya maandishi ya kibiblia, na sisi hatuko huru kufasiri upya maandishi hayo . . . Washtakiwa wana haki ya kuendesha itikadi zao za kidini kwa uhuru . . . Kwa ujumla mahakama hazipekui-pekui kwa ukaribu uhusiano ulio miongoni mwa washiriki (au waliokuwa washiriki) wa kanisa. Makanisa yanapewa kadiri kubwa ya hiari ya kufanya mambo wakati yanapofikiliza nidhamu juu ya washiriki au waliokuwa washiriki. Sisi tunakubaliana na maoni ya Hakimu Mkubwa Jackson [aliyekuwa hakimu wa Mahakama Kubwa Zaidi ya United States] kwamba ‘utendaji mbalimbali [wa] kidini unaohusu wale tu walio washiriki wa ile imani unafanywa kwa uhuru wa hiari na ndivyo unavyopasa kuwa—kuwa wa uhuru wa hiari kabisa kabisa.’ . . . Washiriki wa lile Kanisa [ambalo mwanamke huyo] aliamua kuacha wamekata shauri kwamba wao hawataki tena kushirikiana na yeye. Sisi tunashikilia kwamba wao wana uhuru wa hiari kufanya uchaguzi huo.”

      19, 20. Kwa sababu gani mtu anayekatiliwa nje kutoka kundi hayumo katika hali ya kulipwa hasara zake mahakamani?

      19 Mahakama ya rufani ilikiri kwamba hata ikiwa mwanamke huyo alihisi taabu nyingi ya moyoni kwa sababu waliokuwa wazoeani wake walichagua kutoongea naye, “kumruhusu yeye alipwe hasara za majeraha yasiyoelezeka au ya hisia za moyoni kungewekea Mashahidi wa Yehova mpaka ulio kinyume cha katiba ili wasitumie uhuru wa hiari kuendesha mambo ya dini . . . Uthibitishio ambao katiba inatoa wa kuendesha mambo ya dini kwa uhuru unataka kwamba jamii iachilie namna ya madhara ambayo [mwanamke huyo] alipatwa nayo kwa sababu inastahili sana kuwa hivyo ili kukinga haki ya utofautiano wa kidini ambayo raia wote wanafurahia.” Katika maana fulani, uamuzi huu umepata uzito hata zaidi tangu utolewe. Jinsi gani? Baadaye mwanamke huyo alifanya ombi rasmi kwamba mahakama iliyo ya juu zaidi katika bara hiyo isikilize kesi hiyo na ikiwezekana ibadili uamuzi uliofanywa dhidi yake. Lakini katika Novemba 1987, Mahakama Kuu Zaidi ya United States ilikataa kufanya hivyo.

      20 Kwa sababu hiyo, kesi hii ya maana sana ilionyesha kwamba mtu aliyetengwa au aliyejitenga na ushirika hawezi kufanyiwa malipo ya hasara na Mashahidi wa Yehova katika mahakama ya kisheria kwa sababu ya kuepukwa.d Kwa kuwa kundi lilikuwa likiitikia na kutumia ile mielekezo mikamilifu ambayo sisi sote tunaweza kusoma katika Neno la Mungu, mtu huyo anahisi potezo lililoletwa na vitendo vyake mwenyewe.

      Nidhamu—Wengi Wananufaika

      21. Kwa sababu gani usawaziko unahitajiwa katika maoni yanayohusu kutenga na ushirika?

      21 Baada ya kusikia juu ya kutenga na ushirika, watu fulani wa nje wanakuwa na mwinamio wa kusikitikia mtenda kosa ambaye hawezi kuongea tena na washiriki wa kundi la Kikristo. Lakini je! sikitikio hilo halikuwekwa mahali pasipofaa? Fikiria manufaa inayowezekana kupokewa na mtenda kosa na wengine.

      22, 23. Toa kielezi juu ya umaana na thamani ya kutii Mungu katika maoni yetu kuhusu watu waliotengwa na ushirika?

      22 Mathalani, katika ukurasa 26 sisi tuliona elezo la Lynette juu ya uchaguzi wake ‘kujikatilia nje kabisa kutoka ushirika wote’ pamoja na Margaret dada yake aliyetengwa na ushirika. Yeye na watu wa ukoo wake walio Wakristo ‘walikuwa na itikadi kwamba njia ya Yehova ndiyo bora zaidi.’ Na ndivyo ilivyo kweli kweli!

      23 Baadaye dada ya Lynette alimwambia hivi: ‘Kama wewe ungaliona kutenga na ushirika kama jambo la hivi hivi tu, mimi najua kwamba nisingalichukua hatua za kuelekea kurudishwa upesi kama nilivyofanya. Kukatiliwa nje kabisa kutoka kwenye wapendwa na kutoka uwasiliano wa karibu pamoja na kundi kuliumba tamaa yenye nguvu ya kutubu. Mimi niling’amua sawasawa jinsi mwendo wangu ulivyokuwa wenye kosa na jinsi lilivyokuwa jambo zito kugeuzia Yehova kisogo changu.’

      24. Itikio la dada mmoja kuhusu kutenga na ushirika liliathiri yeye na wengine jinsi gani?

      24 Katika kisa kingine, wazazi wa Laurie walitengwa na ushirika. Hata hivyo mwanamke huyo anasema: ‘Ushirika wangu pamoja nao haukukoma kamwe bali uliongezeka. Kadiri wakati ulivyopita, mimi nikawa zaidi na zaidi asiye mtendaji. Nilifika hata kwenye hatua ya kutohudhuria mikutano.’ Ndipo yeye aliposoma habari katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) wa Septemba 1 na 15, 1981, (Kiswahili ni Desemba 15, 1981, na Januari 1, 1982), ambazo zilikazia kutegemeza lile shauri la 1 Wakorintho 5:11-13 na 2 Yohana 9-11. “Ilikuwa kana kwamba balbu ya taa ilikuwa imewashwa ndani yangu,” yeye anaandika. ‘Mimi nilijua ningelazimika kufanya mabadiliko fulani. Sasa mimi naelewa vizuri zaidi ule umaana wa Mathayo 10:34-36. Uamuzi wangu haukuwa rahisi kukubaliwa na jamaa yetu, kwa maana mwana wangu, mwenye umri wa miaka 5, ndiye mvulana peke yake, na wao wanampenda sana.’ Inatumainiwa kwamba kupoteza ushirika huo kutagusa mioyo ya wazazi, kama kulivyogusa moyo wa Margaret. Hata hivyo, ile nidhamu iliyohusika ilisaidia Laurie: ‘Mimi nimerudi kule nje katika huduma ya shambani. Ndoa yangu na jamaa ni yenye nguvu zaidi kwa sababu ya badiliko langu, na ndivyo nilivyo mimi.’

      25. Ni maoni gani ambayo mtu aliyerudishwa alikuwa nayo kuhusu nidhamu ya Mungu?

      25 Au fikiria hisia za mmoja ambaye alitengwa na ushirika na baadaye akarudishwa. Sandi aliandika: ‘Mimi ningependa kuwapigia ninyi asante kwa zile makala zenye kujaa sana msaada na maagizo [zilizotajwa juu] kuhusu karipio na kutenga na ushirika. Mimi nafurahi kwamba Yehova anapenda watu wake vya kutosha kuhakikisha kwamba tengenezo lake linaendelezwa likiwa safi. Jambo ambalo huenda likaonekana kama la ukatili kwa watu wa nje linahitajiwa kabisa na kwa kweli ni jambo la upendo kufanya. Mimi nimejawa na shukrani kwamba Baba yetu wa kimbingu ni Mungu mwenye upendo na mwenye kusamehe.

      26. Ni tunda gani la uadilifu ambalo linaweza kutokana na kukubali nidhamu? (Zaburi 94:10, 12)

      26 Kwa hiyo Mungu wetu ambaye anataka kwamba mtenda kosa asiyetubu aondoshwe ndani ya kundi anaonyesha kwa upendo pia kwamba ikiwa yule mtenda dhambi anatubu, yeye anaweza kurudishwa katika kundi. (Mtu aliyejitenga na ushirika anaweza vivyo hivyo kuomba awe tena sehemu ya kundi.) Baada ya hapo yeye anaweza kufarijiwa na Wakristo ambao watahakikisha upendo wao kwake. (2 Wakorintho 2:5-11; 7:8-13) Kwa kweli, ni sawa na vile Paulo alivyoandika: “Hakuna nidhamu ambayo inaonekana kwa wakati uliopo kuwa yenye shangwe, bali yenye kihoro; hata hivyo baadaye kwa wale ambao wamezoezwa nayo inazaa tunda lenye kuamanika, yaani, uadilifu.”​—Waebrania 12:11, NW.

  • Je! Wewe Unakumbuka?
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Aprili 15
    • Je! Wewe Unakumbuka?

      Je! wewe umefurahia kusoma matoleo ya hivi majuzi ya Mnara wa Mlinzi? Basi, ona kama unaweza kujibu maswali yanayofuata:

      ◻ Ni nini kichwa cha uenezaji-evanjeli wa Kibiblia siku hizi?

      Kiini cha ujumbe wa mwenezaji-evanjeli leo ni zile habari njema za Ufalme wa Mungu ulio mikononi mwa Mtawala wake mwekwa-rasmi, Yesu Kristo. Hiyo inatia ndani kweli zote alizonena Yesu na ambazo wanafunzi wake waliandika katika kumbukumbu.(Mathayo24:14; 28:19,20)—1/1, ukurasa 4.

      ◻ Kwa sababu gani inahitajiwa kabisa kuendeleza kuhubiri zile habari njema katika maeneo ambamo tokeo ni dogo au hamna lo lote?

      Kupitia Kristo Yesu, Yehova ameamuru kwamba ‘habari njema zihubiriwe katika dunia yote inayokaliwa.’ (Mathayo 24:14, NW) Wakati watu wanapokataa kusikiliza, hiyo inatupa sisi nafasi ya kuonyesha urefu wa kina cha upendo wetu na bidii ya kujitolea Yehova kwa kufanya yanayofaa kwa udumifu. Pia, upendo wetu unatusukuma tuonye jirani zetu juu ya mambo yaliyoko wakati ujao kwa ajili ya aina ya binadamu. (1 Yohana 5:3; 2 Timotheo 4:2) -1/1, ukurasa 26.

      ◻ Ni manufaa gani ambazo huduma ya wakati wote inaletea wahubiri wengi wa Ufalme?

      Inawasaidia kusitawisha kwa ukamili zaidi lile tunda la roho, kuonyesha upendo mwingi zaidi kwa watu, kuwa wenye matokeo zaidi katika huduma, na kumwitibari Yehova kwa kadiri kubwa zaidi. Kwa sababu hiyo, wao wanashangilia kuwa na uhusiano wa karibu zaidi pamoja na Yehova.—1/15, ukurasa 26.

      ◻ Waandikaji wote wa Biblia walielekeza kwenye mwelekezo na kusudi gani la Mungu wajapokuwa na tofauti za kutokeza habari zao?

      Wote walionyesha mambo ambayo Yehova Mungu atatenda kufanya aina ya binadamu iwe yenye furaha, na pia mambo ambayo ni lazima wanadamu mmoja mmoja wafanye ili wapokee kibali cha Mungu.​—2/1, ukurasa 7.

      ◻ Ni nini baadhi ya thawabu na manufaa zinazotokana na kuwa mfuataji haki?

      Hali ya kuitibariana na kutumainiana kwa uhakika inasitawishwa, ikiongoza kwenye mielekeo na mahusiano yenye afya. Ufuataji haki unachangia pia dhamiri safi, na unampa mtu amani ya akili, hivi kwamba yeye anaweza kuelekeana na wengine bila hofu ya kuaibika. (Waebrania 9:14; 1 Timotheo 1:19) —2/15, ukurasa 7.

      ◻ Ni sala za nani ambazo Mungu aliye mweza yote anasikia na kujibu?

      Yehova anasikia sala zinazotolewa kumwelekea yeye kupitia mfereji unaofaa, Yesu Kristo; katika njia inayofaa; na kwa mwelekeo unaofaa wa akili na moyo. Mungu anajibu sala kama hizo kulingana na mapenzi yake ya kimungu na kwenye wakati wake uliochaguliwa. —3/15, ukurasa 7.

      ◻ Ni tukio gani la maana lililotukia katika mwaka wa 20 wa utawala wa Mfalme Artazakse (455 K.W.K.)?

      Nehemia alipewa ruhusa arudi akajenge upya Yerusalemu na kuta zao. Amri hii ilikuwa ndio mwanzo wa yale “majuma sabini’’ ya miaka ya unabii wa Danieli, yakielekeza kwenye mtokeo wa Yesu akiwa “Mesiya Kiongozi” katika wakati barabara, katika 29 W.K. (Danieli 9:24, 25; Nehemia 1:1; 2:1-9, NW) —3/15, kurasa 28,29.

      ◻ Ni njia gani iliyo bora zaidi ya kushughulikia matatizo ya kijamaa?

      Ni kwa upendo, kwa maana Biblia inashauri hivi, “Acheni mambo yenu yote yatukie kwa upendo.” Pia, “Upendo hufunika wingi wa dhambi.”(1 Wakorintho 16:14; 1 Petro 4:8, NW) Huu unapasa kuwa upendo wenye kina kirefu ambao una nia ya kuachilia makosa ya kutokamilika ya washiriki wengine wa jamaa ambayo kama sivyo yanaudhi mtu na kukwaruza hisia zake.​—4/1, kurasa 6, 7.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki