-
BibliaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Au unaweza kusema: ‘Watu wengi wanatumia tafsiri hiyo ya Biblia, nami nina moja katika maktaba yangu.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Je, unajua kwamba mwanzoni Biblia iliandikwa katika Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki? . . . Je, unaweza kusoma lugha hizo? . . . Kwa hiyo, tunafurahi kwamba Biblia imetafsiriwa katika Kiswahili.’ (2) ‘Chati hii (“Orodha ya Vitabu vya Biblia,” katika NW) inaonyesha kwamba Mwanzo, kitabu cha kwanza cha Biblia, kilimalizika mwaka wa 1513 K.W.K. Je, unajua kwamba, baada ya Mwanzo kuandikwa, miaka 3,400 hivi ilipita kabla Biblia nzima kutafsiriwa katika Kiswahili?’ (3) ‘Tangu wakati huo, Kiswahili kimekuwa na mabadiliko mengi. Tumeona hivyo katika muda wa maisha yetu wenyewe, sivyo? . . . Basi tunathamini tafsiri za kisasa zinazoeleza kwa uangalifu zile kweli za awali katika lugha tunayosema leo.’
‘Ninyi mna Biblia yenu wenyewe’
Ona kichwa “Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.”
-
-
DamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Damu
Maana: Umajimaji wa ajabu sana unaozunguka katika mishipa ya wanadamu na katika wanyama walio na chembe nyingi, ukipeleka chakula na oksijeni, ukiondoa takataka, na kutimiza sehemu kubwa katika kuulinda mwili usiambukizwe magonjwa. Damu inahusika sana katika kuendeleza uhai hivi kwamba Biblia inasema “nafsi ya mwili iko katika damu.” (Law. 17:11) Akiwa Chanzo cha uhai, Yehova ametoa maagizo hususa kuhusu matumizi ya damu.
Wakristo wanaamriwa ‘wajiepushe na damu’
Mdo. 15:28, 29: “Roho takatifu na sisi wenyewe [baraza linaloongoza la kutaniko la Kikristo] tumependelea tusiwaongezee ninyi mzigo zaidi, ila mambo haya ya lazima, kuendelea kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu na damu na vitu vilivyonyongwa [au, kuuawa pasipo kutolewa damu] na uasherati. Mkijiepusha kwa uangalifu na mambo haya, mtafanikiwa. Afya njema kwenu!” (Katika andiko hilo, kula damu kunalinganishwa na ibada ya sanamu na uasherati, mambo ambayo hatupaswi kuyafanya.)
Nyama ya wanyama inaweza kuliwa, lakini si damu
Mwa. 9:3, 4: “Kila mnyama anayetembea ambaye yuko hai anaweza kuwa chakula chenu. Kama nilivyowapa mimea ya majani, nawapeni hao wote. Isipokuwa tu nyama pamoja na nafsi yake—damu yake—msile.”
Mnyama yeyote anayeliwa anapaswa kutolewa damu vizuri. Mnyama ambaye amenyongwa, amekufa katika mtego au kupatikana akiwa amekufa hafai kuliwa. (Mdo. 15:19, 20; linganisha na Mambo ya Walawi 17:13-16.) Vivyo hivyo, chakula chochote kilichoongezwa damu au hata visehemu vya damu hakipaswi kuliwa.
Mungu amekubali damu itumiwe katika dhabihu tu
Law. 17:11, 12: “Nafsi ya mwili iko katika damu, nami mwenyewe nimeiweka juu ya madhabahu ili ninyi mfanye upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu, kwa sababu damu ndiyo hufanya upatanisho kupitia nafsi iliyo ndani yake. Ndiyo sababu nimewaambia wana wa Israeli: ‘Nafsi yoyote kati yenu isile damu na mkaaji mgeni yeyote anayekaa akiwa mgeni katikati yenu hapaswi kula damu.’” (Dhabihu zote hizo za wanyama zilizotolewa chini ya Sheria ya Musa zilifananisha ile dhabihu moja ya Yesu Kristo.)
Ebr. 9:11-14, 22: “Kristo alipokuja akiwa kuhani mkuu . . . aliingia, si kwa damu ya mbuzi na ya ng’ombe-dume wachanga, bali kwa damu yake mwenyewe, mara moja kwa wakati wote ndani ya mahali patakatifu na kupata ukombozi wa milele kwa ajili yetu. Kwa maana ikiwa damu ya mbuzi na ya ng’ombe-dume na majivu ya ndama-jike yaliyonyunyizwa juu ya wale ambao wametiwa unajisi hutakasa kufikia usafi wa mwili, je, si zaidi damu ya Kristo, ambaye kupitia roho inayodumu milele alijitoa mwenyewe bila dosari kwa Mungu, itazisafisha dhamiri zetu kutoka katika matendo yaliyokufa ili tutoe utumishi mtakatifu kwa Mungu aliye hai? . . . Damu isipomwagwa hakuna msamaha unaotokea.”
Efe. 1:7: “Kwa njia yake [Yesu Kristo] tuna kuachiliwa huru kwa njia ya fidia kupitia damu ya huyo, ndiyo, msamaha wa makosa yetu, kulingana na utajiri wa fadhili zake zisizostahiliwa.”
Wale waliodai kuwa Wakristo katika karne za kwanza-kwanza W.K. walielewaje amri za Biblia kuhusu damu?
Tertuliano (karibu 160-230 W.K.): “Acheni matendo yenu yasiyo ya asili yaaibishwe mbele ya Wakristo. Sisi hata hatuna damu ya wanyama kwenye chakula chetu, kwa maana hiki ni chakula cha kawaida. . . . Kwenye kesi za Wakristo ninyi [Waroma wapagani] huwapa soseji zenye damu. Bila shaka, ninyi mnasadiki kwamba kitu kilekile mnachotumia kujaribu kuwafanya waondoke kwenye njia iliyo sawa, kitu hicho ni kinyume cha sheria yao. Basi, mkiwa na hakika watachukizwa na damu ya mnyama, mnawezaje kuamini kwamba wataitamani sana damu ya binadamu?”—Tertullian, Apologetical Works, and Minucius Felix, Octavius (New York, 1950), kilichotafsiriwa na Emily Daly, uku. 33.
Minucius Felix (karne ya tatu W.K.): “Sisi tunaiepuka kabisa damu ya binadamu, na hata katika chakula chetu hatutumii damu ya wanyama wanaoliwa.”—The Ante-Nicene Fathers (Grand Rapids, Mich.; 1956), kilichohaririwa na A. Roberts na J. Donaldson, buku la 4, uku. 192.
Kutia Damu Mishipani
Je, amri hiyo ya Biblia inatia ndani damu ya binadamu?
Ndiyo. Andiko la Matendo 15:29, linasema “kuendelea kujiepusha na . . . damu.” Halisemi tu kujiepusha na damu ya wanyama. (Linganisha na Mambo ya Walawi 17:10, andiko lililokataza kula “namna yoyote ya damu.”)
Je, kweli kutiwa damu mishipani ni sawa na kula damu?
Katika hospitali, mgonjwa anaposhindwa kula kupitia kinywa chake, analishwa kupitia mishipa. Je, mtu ambaye hajawahi kutia damu kinywani mwake lakini anakubali
-