Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yubile ya Yehova—Wakati Wetu Kufurahi Sana
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 1
    • Yubile ya Yehova—Wakati Wetu Kufurahi Sana

      “Na ninyi ni lazima mtakase mwaka wa hamsini na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakaaji wayo wote. Utakuwa Yubile kwa ajili ya ninyi . . . Umepasa uwe jambo fulani takatifu kwa ninyi . . . Ndipo kwa hakika ninyi mtakaa juu ya nchi katika usalama.”—WALAWI 25:10-12, 18, NW.

      1. Ni maandishi gani yaliyo juu ya Kengele ya Uhuru, na maneno hayo yametolewa wapi?

      KO KOTE unakoishi, huenda wewe ukawa umepata kusikia habari juu ya Kengele ya Uhuru inayojulikana sana iliyo katika Philadelphia, Pennsylvania, U.S.A. The World Book Encyclopedia kinasema kwamba kengele hiyo “Ilipigwa Julai 8, 1776, pamoja na kengele nyingine za kanisa kutangaza kupitishwa kwa Tangazo Rasmi la Kujitegemea. Maneno yaliyoandikwa juu ya kengele hiyo, ‘Tangazeni Uhuru katika sehemu zote za nchi kwa wakaaji wote waliomo,’ yametolewa katika Biblia (Walawi 25:10).”

      2. Wewe unahisi namna gani juu ya taraja la kupata uhuru, lakini ni matatizo gani ambayo huenda yakatokea kuhusu uhuru huo?

      2 Uhuru unaendelea kuwa na nguvu nyingi za kuvuta watu, sivyo? Inaelekea wewe ungefurahi sana kuwa na taraja la kupata uhuru wa kweli—wa kutoka katika mawazo ya uwongo, mkazo au uonevu wa kisiasa, matokeo yenye kudhoofisha mwili ya uzee na ugonjwa, yenye kutokeza kifo. Ikiwa ndivyo, una sababu nzuri ya kufurahi sana, na karibuni utakuwa na sababu kubwa zaidi. ‘Hiyo inaweza kuwaje?’ huenda wewe ukauliza, kwa sababu hakuna serikali mpaka sasa ambayo imeandaa uhuru kamili, wala wanasayansi wala madaktari hawawezi kuzuia uzee, ugonjwa, na kifo kinachotokea hatimaye. Lakini, tunarudia, upo msingi wa kufurahi sana juu ya uhuru wa kweli. Ili kuelewa ni jinsi gani, fikiria habari fulani za maana za kule nyuma zinazoweza kukuhusu wewe—sasa na katika wakati ujao.

      3. Yubile ilikuwa nini, na ni jambo gani lililotukia wakati huo?

      3 Kifungu kilichotajwa juu kinatumia neno “Yubile.” Yubile kilikuwa kipindi cha kushika Sabato cha mwaka mmoja kwa nchi ya Israeli. Kilifuata mfululizo wa miaka saba-saba ya Sabato za ukulima ambayo ilijumlika kuwa muda wa miaka 49. Mwaka wa 50, ile Yubile, ulikuwa ndio upeo wa mfululizo wa miadhimisho ya Sabato kwa nchi ambayo Yehova alikuwa amewapa watu wake, ikitimiza ahadi aliyopewa Abrahamu baba yao ya zamani, “rafiki ya Yehova.” (Yakobo 2:23; Isaya 41:8, NW) Katika siku ya Yubile, uhuru ulitangazwa katika sehemu zote za nchi. Jambo hilo lilimaanisha uhuru kwa Waisraeli wote waliokuwa wamejiuza katika utumwa kwa sababu ya deni. Jambo jingine la Yubile lilikuwa kwamba mali zote za urithi wa mashamba zilizokuwa zimeuzwa (inaelekea kwa sababu ya uchumi wa watu kuharibika) zilirudishwa kwao.—Walawi 25:1-54.

      4. Yubile ilitangazwa wakati gani, na jinsi gani?

      4 Tukiwa na habari hizo za msingi, unaweza kuthamini ni kwa sababu gani Yubile ulikuwa mwaka wa uhuru wenye kusherehekewa. Ulitangazwa kwa kupiga mbiu katika Siku ya Upatanisho.a Ni kama vile Musa alivyoandika katika Walawi 25:9, 10, NW: “Na wewe ni lazima uililishe mbiu ya mlio mkubwa katika mwezi wa saba katika siku ya kumi ya mwezi; katika siku ya upatanisho ninyi watu mnapaswa kuililisha. Na nyini ni lazima mtakase mwaka wa hamsini na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakaaji wayo wote. Utakuwa Yubile kwa ajili ya ninyi, na lazima mrudi kila mmoja kwenye mali yake na kila mmoja kwa jamaa yake.” Katika 1473 K.W.K, Yoshua aliongoza Waisraeli akawavusha Mto Yordani na kuwaingiza katika Nchi ya Ahadi, ambamo walipaswa kuishika Yubile.

      Uhuru wa Kwanza-kwanza Watangazwa

      5. Ni mambo gani ya ukombozi na Yubile tutakayofikiria?

      5 Mambo yaliyotangulia kutajwa yanaweza kuonekana kama historia ya kale isiyohusu sana maisha zetu, hasa ikiwa sisi si wa ukoo wa Kiyahudi. Ijapokuwa hivyo, Yesu Kristo alitupa sisi sababu inayofaa kutazamia Yubile kubwa zaidi. Jambo hilo ndilo linalofanyiza msingi wa kufurahi sana kwetu juu ya uhuru. Ili tuthamini ni kwa sababu gani, tunahitaji kuona jinsi Yesu alivyofanya kwa njia mbili uandalizi kwa ajili ya uhuru katika karne ya kwanza. Halafu tutafikiria jinsi njia hizo zinavyolingana na mauhuru mawili katika wakati wa maisha yetu, lakini mauhuru ya kadiri kubwa zaidi na yenye kutupa sababu kubwa zaidi ya kufurahi sana.

      6, 7. (a) Andiko la Isaya 61:1-7 lilitabiri matukio gani mazuri ajabu? (b) Yesu alionyeshaje kwamba unabii wa Isaya ulikuwa unatimizwa wakati huo?

      6 Ingawa halisemi moja kwa moja juu ya mwaka wa kale wa Yubile, rejezo moja la kiunabii kuhusu namna moja inayokuja ya uhuru lilifanywa kwenye Isaya 61:1-7, NW: “Roho ya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova iko juu yangu, kwa sababu ya kwamba Yehova amenipaka mafuta kuambia wapole habari njema. Yeye amenituma kuganga-ganga waliovunjika moyo, kutangazia uhuru wale waliochukuliwa mateka na hata kutangazia wafungwa wafunguliwe wazi macho; kuutangaza mwaka wa nia njema upande wa Yehova na siku ya kisasi kwa upande wa Mungu wetu; kufariji wote wanaoomboleza . . . Kufurahi sana mpaka wakati usiojulikana ndiko kutakuwa fungu lao.” Lakini ni jinsi gani na wakati gani unabii huo ungetimizwa?

      7 Baada ya mwadhimisho wa sikukuu ya Kupitwa katika mwaka 30 W.K., Yesu Kristo aliingia ndani ya sinagogi siku ya Sabato. Akiwa humo akasoma sehemu ya unabii wa Isaya na kuitumia kuhusu yeye mwenyewe. Luka 4:16-21, NW linasema, kwa sehemu: “Yeye akalifungua kunjo na kupata mahali palipoandikwa: ‘Roho ya Yehova iko juu yangu, yeye alinituma niende nikahubiri kuachiliwa kwa mateka na kupata nafuu ya kuona kwa walio vipofu, kuwaondosha waliopondeka kwa kuwaachilia, kuhubiri mwaka unaokubalika wa Yehova, . . . Halafu yeye akaanza kuwaambia: ‘Leo andiko hili ambalo mmesikia sasa hivi limetimizwa.’”

      8. (a) Ni ukombozi gani wa kwanza-kwanza ambao Yesu aliandaa? (b) Jambo hilo linaonyeshwaje katika Yohana 9:1-34?

      8 Habari njema ambazo Yesu alitangaza ziliwaandalia uhuru wa kiroho Wayahudi waliozikubali. Kwa kufunguliwa macho yao wazi waone mambo yaliyomaanishwa na matakwa hasa na ibada ya kweli, waliwekwa huru watoke katika mawazo mengi yenye makosa. (Mathayo 5:21-48) Uhuru huo ulikuwa na thamani kubwa kuliko maponyo ya kimwili ambayo Yesu alifanya. Kwa sababu hiyo, ingawa Yesu aliyafungua macho ya mwanamume aliyezaliwa akiwa kipofu, mwanamume huyo alipata faida ya kudumu zaidi kutokana na kubaini kwamba Yesu alikuwa nabii kutoka kwa Mungu. Uhuru mpya wa mwanamume huyo ulitofautiana na hali ile ya viongozi wa kidini ambao walikuwa wametumikishwa kwenye mapokeo yao na imani zenye makosa. (Yohana 9:1-34; Kumbukumbu 18:18; Mathayo 15:1-20) Hata hivyo huo ulikuwa uhuru wa kwanza-kwanza tu au wa utangulizi Hata katika karne ya kwanza, Yesu angepaswa kusaidia kwa namna nyingine ya uhuru uliolingana na Yubile katika Israeli ya kale. Kwa sababu gani n jambo la akili kukata shauri hivyo?

      9. Hata kwa wale waliokombolewa kiroho, ni namna gani ya utumwa iliyobaki?

      9 Yesu alimwambia hivi mwanamume huyo aliyekuwa kipofu: “Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.” Halafu akawaambia Mafarisayo: “Kama mngekuwa vipofu, msingekuwa na dhambi; lakini sasa mwasema, Twaona; basi dhambi yenu inakaa.’ (Yohana 9:35-41) Ndiyo, dhambi inayoongoza kwenye kifo ilikuwa bado tatizo kubwa, hata kama ilivyo sasa. (Warumi 5:12) Hata Wayahudi, kutia na mitume waliofaidika na uhuru ule wa kwanza kwanza, uhuru wa kiroho ambao Yesu aliandaa, walibaki wakiwa wanadamu wasiokamilika. Waliendelea kuwa watu mwa kwa dhambi na kwa kifo chenye kutokezwa nayo. Je! Yesu angelibadili jambo hilo? Angeweza? Na ikiwa ndivyo, wakati gani?

      10. Yesu aliahidi kwamba angeandaa uhuru gani w ziada?

      10 Mapema kabla ya hapo Yesu alikuwa akisema: “Ninyi mkibaki katika neno langu ninyi ni wafuasi wangu kweli kweli, na ninyi mtaujua ukweli, na ukweli utawaweka ninyi huru.” Wasikilizaji wake Wayahudi wakamjibu: “Sisi ni wazaliwa wa Abrahamu na hatujapata kamwe kuwa watumwa kwa mtu ye yote. Imekuwaje wewe wasema, ‘Ninyi mtakuwa huru.’?” Yesu akajibu: “Kwa kweli kabisa: mimi nawaambia ninyi, Kila mtendaji dhambi ni mtumwa wa dhambi. Tena, mtumwa haba ki kati ya watu wa nyumbani milele; mwana anabaki milele.” (Yohana 8:31-36, NW) Basi uzaliwa wa kimwili kutokana na Abrahamu haungeweza kuweka Wayahudi huru na utu mwa kwa dhambi. Yesu alitoa tangazo hilo la kihistoria kuhusu uhuru ili avute fikira kwenye jambo fulani lililokuwa likija na ambalo lingekuwa kubwa kuliko mambo ambayo Waisraeli walijionea katika Yubile yo yote.

      Yubile ya Kikristo Yaanza

      11. Kwa sababu gani kupendezwa kwetu na Yubile ya Kikristo kunakaza fikira juu ya mwaka wa 33 W.K.?

      11 Wayahudi hawakuona kwamba Yubile ya agano la Torati la Musa ilikuwa kifananishi cha Yubile kubwa zaidi. (Wakolosai 2:17; Waefeso 2:14, 15) Yubile hiyo kwa Wakristo inatia ndani “ukweli” unaoweza kuweka wanadamu huru—ukweli ambao unahusiana hasa na “Mwana,” yaani Yesu Kristo. (Yohana 1:17) Ni wakati gani ilipoanza kusherehekewa Yubile hiyo kubwa zaidi ambayo ingeweza kuleta uhuru hata wa kutolewa katika dhambi na matokeo yake? Ilianza katika masika ya 33 W.K., siku ya Pentekoste. Hiyo ilikuwa siku kumi baada ya kupaa kwa Yesu mbinguni akaonyeshe mbele za Yehova Mungu ustahili wa dhabihu yake.—Waebrania 9:24-28.

      12, 13. Ni jambo gani lililotukia baada ya kifo cha Yesu ambalo lililetea wafuasi wake tukio lisilo na kifani?

      12 Kabla ya Yesu, hakuna kiumbe mwanadamu aliyekuwa amefufuliwa kutoka kwa wafu aendelee kuishi milele. (Warumi 6:9-11) Bali, wote walilala usingizi katika kifo na wangeendelea kulala mpaka wakati ufike wa kufufuliwa kwa jamaa ya kibinadamu. Kwa ufufuo wake kupitia uwezo wa Mungu, Yesu Kristo akawa kile ambacho Maandiko yaliyoongozwa na Mungu yanamwita, “matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo.” — 1 Wakorintho 15:20, NW.

      13 Siku 50 baada ya ufufuo wake, kulikuwa na ushuhuda wa kwamba Yesu Kristo aliyefufuliwa alikuwa amepaa akaingia ndani ya mbingu. Na alikuwa ameingia ndani ya kuwapo kwa Yehova Mungu akiwa na thamani ya dhabihu yake kamilifu ya kibinadamu na kuitumia kwa ajili ya wanadamu. Jambo hilo lilitukia siku ya Pentekoste 33 W.K. Kwa kutii maagizo kutoka kwa Yesu, wafuasi karibu 120 walikutana pamoja katika Yerusalemu. Ndipo Yesu alipomimina roho takatifu juu ya wafuasi hao, kwa utimizo wa Yoeli 2:28, 29. Ndimi kama kwamba za moto zilikaa-kaa juu ya vichwa vyao, nao wakaanza kusema lugha zilizo ngeni kwao. (Matendo 2:16-21, 33) Huo ulikuwa uthibitisho wa kwamba Yesu Kristo aliyefufuliwa alikuwa amepaa akaingia katika mbingu na akawa ameingia ndani ya kuwapo kwa Mungu akiwa na thamani ya dhabihu kamilifu ya kibinadamu ili aitumie kwa ajili ya wanadamu.

      14. (a) Hali ya wafuasi wa Kristo ilikuwa nini kwa habari ya maagano? (b) Agano jipya lilihusu baraka gani ya kutokeza?

      14 Matokeo yalikuwa nini kwa wafuasi hao? Jambo moja ni kwamba, wao waliwekwa huru watoke katika agano la Torati la Musa, ambalo Mungu alikuwa amefanya pamoja na taifa la Israeli la asili lakini ambalo sasa alikuwa amefuta, akalipigilia misumari kwenye mti wa mateso ya Yesu. (Wakolosai 2:13, 14; Wagalatia 3:13) Mahali pa agano hilo palichukuliwa na agano jipya, si lenye kufanywa pamoja na taifa la Israeli la asili, bali pamoja na “taifa” jipya la Israeli wa kiroho. (Waebrania 8:6-13; Wagalatia 6:16) Agano jipya hilo, lililotabiriwa kwenye Yeremia 31:31-34, lilipangwa kupitia mpatanishi mkubwa kuliko Musa nabii wa kale. Kwa sababu ya kupendezwa kujua mambo ya uhuru, inatupasa hasa tuangalie jambo moja la agano jipya. Mtume Paulo alivuta fikira kwenye jambo hilo, akiandika hivi: “Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, . . . Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa. Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi.”—Waebrania 10:16-18.

      15. Kwa sababu gani tunaweza kusema kwamba katika Pentekoste 33 W.K. Yubile ya Kikristo ilianza kwa wapakwa-mafuta? (Warumi 6:6, 16-18)

      15 Yesu alikuwa akielekeza kwenye uhuru huo wa kutolewa katika dhambi aliposema hivi: “Mwana akiwaweka ninyi huru, ninyi mtakuwa huru kikweli.” (Yohana 8:36, NW) Wazia hilo—uhuru wa kutolewa katika dhambi uliofanywa uwezekane juu ya msingi wa dhabihu ya Kristo! Kuanzia siku ya Pentekoste, Mungu aliwatangaza wenye kuamini kuwa waadilifu ndipo akawachukua wawe wana wa kiroho wa kulelewa wenye taraja la kutawala pamoja na Kristo mbinguni. Paulo anaeleza hivi: “Kwa maana ninyi hamkupokea roho ya utumwa yenye kusababisha woga tena, bali ninyi mlipokea roho ya kuchukuliwa mlelewe mkiwa wana, . . . Basi, ikiwa sisi tu watoto, sisi tu warithi pia: warithi kweli kweli wa Mungu, lakini warithi washirika pamoja na Kristo.” (Warumi 8:15-17, NW) Bila shaka, Yubile ya Kikristo ilikuwa imeanza kwa Wakristo wapakwa-mafuta.

      16. Ni baraka na mataraja gani ya ziada yaliyohusika kwa wale wenye kuadhimisha Yubile ya Kikristo?

      16 Hivyo siku hiyo ya Pentekoste katika mwaka 33 W.K., taifa jipya la Israeli wa kiroho lilitokea. Waliojumlika kuwa taifa hilo walikuwa wanadamu ambao dhambi zao zilikuwa zimesamehewa juu ya msingi wa damu ya dhabihu ya Kristo. (Warumi 5:1, 2; Waefeso 1:7) Ni nani kati yetu ambaye angeweza kukana kwamba washiriki hao wa kwanza Waisraeli wa kiroho walioingizwa ndani ya agano jipya hawakupata ukombozi mzuri ajabu wakawa huru kwa kusamehewa dhambi zao? Walifanywa na Mungu wakawa “mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, [wapate] kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita [watoke] gizani [wakaingie] katika nuru yake ajabu.” (1 Petro 2:9) Ni kweli kwamba miili yao ya nyama ilikuwa ingali isiyo kamilifu nao wangekufa baada ya muda fulani. Hata hivyo, sasa Mungu alikuwa amewatangaza waadilifu na akawachukua wawe wana wa kiroho wa kulelewa, kifo chao cha kimwili kilikuwa ‘kuachiliwa’ kulikoruhusu ufufuo wao waende kwenye “ufalme wa kimbingu wa Kristo.” —2 Timotheo 4:6, 18, NW.

      17, 18. Kwa sababu gani ukombozi wa Yubile ya Kikristo ulikuwa wenye thamani kubwa kuliko uhuru wa utangulizi ambao Yesu alitangaza?

      17 Hatua ya kwanza-kwanza au ya utangulizi ya kuweka huru Wayahudi wenye kuamini watoke katika mawazo na mazoea yenye makosa ilikuwa na thamani kubwa. Ijapokuwa hivyo, tumeona kwamba Yesu alichukua hatua inayopita ukombozi huo wa kuwekwa huru kiroho. Kuanzia Pentekoste 33 W.K. na kuendelea, yeye alikomboa wanadamu wenye kuamini akawaweka huru kutoka “sheria ya dhambi na kifo.” (Warumi 8:1, 2, NW) Hivyo ndivyo ilivyoanza Yubile ya Kikristo kwa Wakristo wapakwa-mafuta. Huo kikweli ulikuwa ukombozi wenye thamani kubwa zaidi wa kuwekwa huru, kwa maana ulitia ndani taraja la kupata uzima mbinguni wakiwa warithi washirika pamoja na Kristo.

      18 Kufikia hapo tumefikiria pande mbili za uhuru wa Kikristo katika karne ya kwanza, ambazo haziwezi kukanwa kuwa zilikuwa msingi wa kufurahi sana. Na waamini wa karne ya kwanza walifurahi sana. (Matendo 13:44-52; 16:34; 1 Wakorintho 13:6; Wafilipi 4:4) Ndivyo ilivyokuwa hasa kuhusu ushiriki wao katika Yubile ya Kikristo, iliyowafungulia njia ya kupokea baraka za milele katika mbingu. — 1 Petro 1:3-6; 4:13, 14.

      19. Ni maulizo gani yanayobaki kwa Wakristo ambao hawakuzaliwa kwa roho, na ni jambo gani linaloonyesha kwamba wao watakuwa na sehemu katika ukombozi utakaoandaliwa na Mungu?

      19 Ingawa hivyo, ni nafasi gani inayowafaa Wakristo wa kweli walio wengi leo ndani ya mpango huu, kwa kuwa hawakutangazwa kuwa waadilifu na hawakupakwa mafuta kwa roho takatifu? Kuna sababu ya Kimaandiko ya kutafuta ukombozi wa kiasi kikubwa wa kuwekwa huru kwao wakiwa sehemu ya Yubile ya Kikristo. Kumbuka Matendo 3:20, 21: “[Yesu] ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu wake tokea mwanzo wa ulimwengu.” (Linganisha Matendo 17:31.) Kakika maana ile ile, Yohana, mtume mpakwa-mafuta aliyekuwa tayari akifurahia Yubile ya Kikristo, aliandika hivi juu ya Yesu Kristo: “Naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.” (1 Yohana 2:2) Je! hiyo inamaanisha kwamba wale Wakristo wengi washikamanifu leo ambao hawana tumaini la kimbingu wanaweza kufurahia sana uhuru wa Kikristo? Je! kufurahi huko ni kwa wakati ujao tu, au tayari tuna sababu ya kufurahi sana? Tunaweza kugundua jambo hilo kwa kuchunguza zile pande za ukombozi wa Kikristo na Yubile ambazo zina maana pekee kwa waabudu wa kweli leo.

      [Maelezo ya Chini]

      a Siku ya Upatanisho iliyokuwa mwadhimisho mkubwa wa kila mwaka ilifanywa katika tarehe ya 10 ya Tishri, mwezi uliokuwa katika kalenda ya Kiebrania, unaolingana na kipindi chetu cha kati ya Septemba na Oktoba.

      Mawazo Yako ni Nini?

      ◻ Faida za Yubile zilikuwa ni nini katika Israeli wa kale?

      ◻ Yesu alitangazaje ukombozi fulani wa kwanza-kwanza, na ulihusu nini?

      ◻ Ni wakati gani Yubile ya Kikristo ilipoanza, na ni msingi gani wa kukata shauri hilo?

      ◻ Kwa sababu gani tuna sababu ya kutazamia ukombozi unaohusu mamilioni ya Wakristo ambao si wapakwa-mafuta wa roho?

  • Yubile ya Kikristo Yafikia Upeo Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 1
    • Yubile ya Kikristo Yafikia Upeo Katika Mileani

      1. Wayahudi katika Jamhuri ya Israeli hawajafanya jitihada ya kuanzisha tena kitu gani, na kwa sababu gani?

      HATA katika Jamhuri ya Israeli (iliyoanzishwa katika 1948), Wayahudi walio wengi wanaojifikiria kuwa wako chini ya Torati la Musa hawajaanzisha tena kusherehekea mwaka wa Yubile. Na kungekuwa na vitatanishi vingi kama wangejaribu. Matatizo mengi sana ya uchumi yangetokea, kwa maana haki za umaskini zinahusika. Jamhuri ya Israeli siyo yenye nchi yote iliyokaliwa na makabila yale 12 ya kale. Pia hakuna hekalu lenye kuhani mkuu wa kabila la Lawi, kwa kuwa vitambulishi vya makabila ya watu vilipotezwa.

      2. Ni jinsi gani Wakristo wengine tayari wamekwisha kuanza kusherehekea Yubile iliyotolewa na kivuli ile ile ya Israeli wa kale?

      2 Ingawa hivyo, jambo hilo linatuacha sisi wapi kwa habari ya baraka za sherehe ya Yubile? Tunakumbuka kwamba Yubile ya kale ilikuwa mwaka wa uhuru wenye shangwe—Waisraeli waliokuwa wamejiuza kuingia utumwani waliwekwa huru na wakarudishiwa mashamba yao ya urithi. (Walawi 25:8-54) Katika makala iliyotangulia tuliona kwamba mpango huo ulikoma pamoja na agano la torati la Musa katika 33 W.K. (Warumi 7:4, 6; 10:4) Ndipo lilipoanzishwa kutenda agano jipya ambalo kwalo Mungu angeweza kusamehe dhambi za waamini, awapake mafuta kwa roho takatifu, na kuwachukua wawe wana wa kulelewa ambao wangepelekwa mbinguni. (Waebrania 10:15-18) Hata hivyo wale wenye kufaidika kwa njia hiyo kutokana na mpango huo wa agano jipya ni “kundi dogo” la watu 144,000 ‘ambao wamenunuliwa katika dunia.’ Kwa hiyo mamilioni ya Wakristo wengine washikamanifu wanaweza kupataje ukombozi ambao Yubile ilikuwa kivuli chao? —Luka 12:32; Ufunuo 14:1-4.

      Dhabihu kwa Ajili ya Wote!

      3. Dhabihu ya Yesu ni yenye matokeo na udumifu wa kadiri gani?

      3 Katika nyakati zilizotangulia Ukristo faida za Siku ya Upatanisho ya kila mwaka zilidumu kwa mwaka mmoja tu. Faida za dhabihu ya ukombozi wa Bwana Yesu Kristo ni za kuendelea, za daima. Hivyo Yesu, Kuhani Mkuu mfananishwa, si lazima awe mwanadamu tena, na ajidhabihu, ndipo arudi mbinguni, akaonyeshe thamani ya dhabihu hiyo mwaka baada ya mwaka katika Patakatifu Zaidi Sana pa Yehova Mungu. Ni kama vile Maandiko yanavyosema: “Kristo, sasa kwa kuwa yeye ameinuliwa kutoka kwa wafu, hafi tena; kifo si bwana mkubwa juu yake tena.”—Warumi 6:9; Waebrania 9:28, NW.

      4, 5. (a) Ni nini yamekuwa matokeo ya matumizi ya dhabihu ya Yesu kuanzia Pentekoste 33 W.K.? (b) Tuna kionyesho gani cha kwamba dhabihu yake itatumiwa kwa upana zaidi?.

      4 Kwa sababu hiyo, katika miaka iliyofuata Pentekoste ya 33 W.K., waamini wameanza kusherehekea Yubile ya Kikristo wakiisha kuwa wafuasi waliozaliwa kwa roho wa Bwana Yesu aliyetukuzwa. Wakiisha ‘kuwekwa huru watoke katika sheria ya dhambi na kifo,’ wao wamefurahia uhuru wenye kuwatia nguvu. (Warumi 8:1, 2, NW) Wameutangaza pia ujumbe wa Kikristo ili watu wengine zaidi waweze kusamehewa dhambi zao, wapakwe mafuta, na wawe wana wa kiroho v Mungu. Ingawa hivyo, hiyo inamaanisha kwamba ikiwa mtu si wa kikundi hicho ambacho ni cha watu 144,000 tu, hawezi kupata ukombozi wenye kufurahisha sasa?

      5 Yaliyo ya maana katika habari hii ni m, neno ya mtume Paulo kwenye Warumi 8:19-21: “Viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili [vikiwa vyenye dhambi na visivyoweza kuondolea mbali dhambi kabisa].” Ndipo Paulo alipokazia kwamba kuna “tumaini; kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru w utukufu wa watoto wa Mungu.” Basi, uhuru huo si kwa wale tu wanaokuwa “watoto wa Mungu” mbinguni. Maneno yaliyozoeleka kwenye Yohana 3:16 yanathibitisha jambo hilo. Na, kama ilivyotajwa, mtume Yohana mpakwa-mafuta alisema kwamba Kristo alikufa “kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.’—1 Yohana 2:2.

      1919—Ukombozi wa Kwanza-kwanza

      6, 7. Tangu 1919 ni ukombozi wa namna gani umetangazwa, na kwa sababu gani hasa tangu wakati huo?

      6 Katika nyakati za kisasa wapakwa-mafuta wanaosherehekea Yubile ya Kikristo wamekuwa wakitangaza habari njema zinazokomboa, hasa tangu 1919 W.K. ‘Kwa sababu gani kuanzia wakati huo?’ huenda wewe uke taka kujua ikiwa umezaliwa majuzi zaidi. Acheni tuone, huku tukizingatia kwamba jambo hili linahusu kufurahia kwako ukombozi.

      7 Kwa miongo ya miaka kabla ya tarehe hiyo wapakwa-mafuta wa Yehova walichapisha kweli za Kibiblia, kama vile katika mfululizo unaojulikana sana wa vichapo Studies in the Scriptures (1886-1917). Waligawa pia kati ya watu vijitabu na trakti nyingi zenye kuwaarifu mambo. Wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza upinzani ulitokea, kujaribu na kupepeta, na kupungua mwendo kwa utendaji wao mbalimbali. Lakini katika 1919, mabaki wapakwa-mafuta walijitokeza wakiwa na bidii iliyofanywa upya ili kutangaza kweli za Biblia. Kama vile Yesu angeweza kusema katika 30 W.K. kwamba yeye alipakwa mafuta awahubirie ‘wafungwa kufunguliwa kwao na vipofu kupata kuona tena,’ ndivyo wapakwa-mafuta hao wa kisasa wangeweza kufanya. Baada ya mkusanyiko wa kusisimua katika Septemba 1-7, 1919,a wao walisonga mbele kwa nguvu nyingi wakizitangaza kweli zilizokomboa watu wasiohesabika.—Luka 4:18.

      8, 9. Ni katika maana gani watu wengi wamewekwa huru, na ni misaada gani imetumiwa katika kutangaza ukombozi huo?

      8 Kwa mfano, fikiria msaada ule wa kujifunzia Biblia The Harp of God (1921), uliotokeza kweli za muhimu kama kwamba zilikuwa nyuzi kumi katika kinubi. Kitabu hicho kilikiri kwamba “watu wengi wameogopeshwa wasijifunze Biblia” na fundisho lile la kwamba “adhabu kwa waovu . . . ni mateso ya milele au kuteswa-teswa katika mahali panapowaka moto na kiberiti usiozimika.” Wasomaji wa nakala zile karibu 6,000,000 za kitabu hicho walijifunza kwamba fundisho hilo ‘halingeweza kuwa kweli kwa angalau sababu nne mbalimbali na zenye kutokeza sana: (1) kwa sababu halipatani na kufikiri kuzuri; (2) kwa sababu linahitilafiana sana na haki; (3) kwa sababu ni kinyume cha kanuni ya upendo; na (4) kwa sababu lote kabisa halipatani na maandiko.” Unaweza kuwazia jinsi jambo hilo lilivyokomboa watu waliokuwa wamekua katika woga wa mateso ya milele katika mahali penye moto au ya maumivu makali sana katika purgatori!

      9 Ndiyo, mahubiri yenye bidii ya ukweli wa Biblia yaliyofanywa na wapakwa-mafuta hao yaliwaweka huru kila upande wa dunia watu waliokuwa wamefanywa kuwa watumwa wa mafundisho ya uwongo, mambo ya ushirikina, na mazoea yasiyo ya kimaandiko (kama vile kuabudu wazee wa ukoo waliokufa, kuogopa mizuka au roho waovu, na kunyonywa kifedha na viongozi wa kidini). Vichwa vyenyewe vya misaada fulani ya kujifunza Biblia vinaonyesha jinsi ilivyokuwa na nguvu nyingi za kuvuta mamilioni ya watu wakombolewe.b Hivyo maneno ya Yesu yamethibitika kuwa kweli, wakati aliposema kwamba wafuasi wake ‘wangefanya kazi kubwa kuliko’ alizofanya yeye. (Yohana 14:12) Kwa kulinganishwa na kazi ile ya utangulizi ya ukombozi wa kiroho ambayo Yesu alifanya kwa kuhubiri ‘kufunguliwa kwa wafungwa,’ watumishi wa kisasa wa Mungu wamefanya kiasi kikubwa zaidi—wakifikia mamilioni mengi ya watu kila upande wa dunia.

      10. Kwa sababu gani tunaweza kutazamia kwamba ukombozi wa ziada na ulio mkubwa zaidi utaonwa na watu?

      10 Ijapokuwa hivyo, kumbuka kwamba katika karne ya kwanza ukomboaji mwingine zaidi ulianza katika Pentekoste 33 W.K. Huko Yubile ya Kikristo ilianza kwa ajili ya “kundi dogo” ambao wangesamehewa dhambi zao, na jambo hilo liwaongoze kuwa “wana wa Mungu” mbinguni. Namna gani katika wakati wetu? Je! mamilioni ya Wakristo wengine wenye kujitoa wangefunguliwa watoke katika kifungo cha dhambi na hivyo washerehekee Yubile kuu? Ndiyo, na mtume Petro alionyesha hivyo aliposema juu ya “zamani za kufanya upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu [wa kale].”—Matendo 3:21.

      Yubile kwa Mamilioni

      11. Walawi sura ya 25 inadokezaje kwamba tunaweza kutafuta ukombozi unaopanuka kufikia wengi zaidi ya Israeli wa kiroho tu?

      11 Inastahili kuangaliwa kwamba katika Walawi sura ya 25, Waisraeli walikumbushwa mara mbili kwamba kwa maoni ya Yehova wao walikuwa “watumwa” wake aliokuwa amewakomboa kutoka Misri. (Mistari 42 na 55, NW) Sura hiyo ya Yubile inataja pia “walowezi” na ‘wakaaji wa kigeni kati yao.’ Watu hao leo wana ulinganifu na “mkutano mkubwa” wanaoshiriki pamoja na Waisraeli wa kiroho katika kuzitangaza habari njema za Kikristo.

      12. Tangu 1935 ni tukio gani lenye kufurahisha ambalo limekuwa likiendelea?

      12 Tangu 1935 “mchungaji mwema” Yesu Kristo amewaingiza wale wanaotaka kuwa: “kondoo wengine” ndani ya ushirika wenye utendaji pamoja na mabaki wapakwa-mafuta Ilikuwa lazima ‘awalete’ hao, nao walipaswa kuwa “kundi moja” chini ya “mchungaji mmoja.” (Yohana 10:16) Sasa “kondoo wengine” ni mamilioni. Ikiwa wewe ni wa umati huo wenye furaha, tayari unahesabiwa kuwa mwadilifu ukiwa rafiki ya Mungu. na ukiwa sehemu ya uumbaji wa kibinadamu unaotazamia ‘kuwekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu’ wakati wa “zamani [zinazokuja] za kufanywa upya vitu vyote” duniani. Hilo si tumaini lililowekwa pasipofaa.—Warumi 8:19-21; Matendo 3:20, 21.

      13. Ni baraka gani hasa tunayopasa kuangalia kuwa inatukia baada ya dhiki kubwa?

      13 Baada ya mtume Yohana kuona 144,001 wanaofurahia Yubile ya Kikristo ambao tu maini lao ni kuwa mbinguni, alieleza juu ya “mkutano mkubwa,” akisema: “Hao ndio ambao wanatoka katika dhiki kubwa, na wao wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo. Hiyo ndiyo sababu wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu nao wanamtolea utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake.”—Ufunuo 7:14, 15, NW.

      14, 15. Kwa sababu gani wale wa “mkutano mkubwa” wana sababu ya pekee kufurahi sana sasa?

      14 Hata sasa, kabla ya ile dhiki kubwa, hao wanajizoeza imani katika damu iliyomwagwa ya Kristo, na hivyo wanafaidika na kifo chake cha dhabihu. Wanafurahi sana pia juu ya kukombolewa kutoka katika Babuloni Mkuu, juu ya kuwa na dhamiri njema mbele za Yehova Mungu, na katika pendeleo lao la kushiriki katika utimizo wa Mathayo 24:14 kwa kuzihubiri habari njema za Ufalme kabla mwisho haujaja.

      15 Ijapokuwa hivyo, namna gani taraja la mkutano mkubwa la kukombolewa kutoka katika dhambi na kutokukamilika walikozaliwa nako? Je! wakati huo uko karibu? Kuna sababu nzuri ya kushikilia kwamba bado wangali pamoja nasi wengine wa kizazi cha wanadamu ambacho Yesu Kristo alitabiri hakingepita mpaka mambo yote yaliyotabiriwa yatimizwe. (Mathayo 24:34) Kwa sababu hiyo, mwisho mkuu wa “umalizio wa mfumo wa mambo” bila shaka uko karibu sana.—Mathayo 24:3.

      Vipeo vya Yubile ya Kikristo

      16. Sisi tunasimama wapi katika kutimilizwa kwa kusudi la Mungu, na ni jambo gani lililo mbele?

      16 “Vita ya siku ile kuu ya Mungu mwenyezi” inakuja mbio mbio, na mabaki ya “kundi dogo,” na pia ule “mkutano—mkubwa” wa waandamani waaminifu na washikamanifu watashika ukamilifu kuelekea Yehova Mungu na wanatazamia kupata ulinzi wa kimungu. Wao wanatazamia kwa hamu nyingi Yehova ashinde kabisa majeshi yote ya adui, ili yeye Kuu ya Ulimwengu Wote. Hicho kitakuwa kipeo cha ajabu kitakachofanya wafurahie uhuru wa Kikristo!—Ufunuo 16:14; 19:19-21; Habakuki 2:3.

      17. Ni jinsi gani bado mamilioni ya watu watapokea ukombozi katika Yubile kuu na yenye utukufu?

      17 Ndipo utakapofuata juu ya dunia utawala wa Mfalme Yesu Kristo aliye mshindi, huku enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote ikiwa imethibitishwa kwa mara nyingine tena, na Yesu Kristo akiwa ndiye mwenye uongozaji kamili wa dunia akiwa Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Ndipo yeye atakapotumia moja kwa moja ustahili wa dhabihu yake kwa mamilioni ya wanadamu, kutia ndani watakaofufuliwa, wanaojizoeza imani na wanaokubali kwa nia msamaha wa dhambi ambao Mungu ataandaa kupitia Kristo. Ushuhuda wa jambo hilo utaonyeshwa kwa Mungu kufuta “kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena.” (Ufunuo 21:3, 4) Ikiwa huo si ukomboaji wa kweli, kuna mwingine gani?

      18. Kwa njia inayoweza kulinganishwa na jambo moja la Yubile ya kale, ni nini litakalotukia kuhusu dunia katika mfumo mpya?

      18 Zaidi ya hivyo, dunia haitaongozwa tena, ichafuliwe tena, wala iharibiwe tena na watu mmoja mmoja wenye pupa, mashirika, na serikali za kibinadamu. (Ufunuo 11:18) Bali, itarudishwa kwa waabudu wa kweli. Wao watakabidhiwa ile kazi yenye kufurahisha ya kushiriki katika utimizo halisi wa unabii wa Isaya: “Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake. Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine, . . . Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na [Yehova].” (Isaya 65:21-25) Kufikia mwisho wa Utawala wa Mileani vidalili vyote vya dhambi na kutokamilika kulikorithiwa vitakuwa vimefutiliwa mbali na washikamanifu wa Mungu duniani watakuwa wakisherehekea upeo kamili utakaokuwa kikomo cha Yubile. Kwa hiyo ukombozi uliotolewa kivuli na ile Yubile utakuwa umetimilika.—Waefeso 1:10, NW.

      Baada ya Upeo wa Kimileani wa Yubile

      19, 20. Shetani na mashetani watajaribuje kukatiza baraka zenye kutokana na Yubile ya Mileani, lakini matokeo yatakuwa nini?

      19 Andiko la Ufunuo 20:1-3 linatabiri kwamba Shetani Ibilisi, mtawala wa vikosi vya mashetani, atakuwa ameondoshwa uwanjani kwa muda wa ile miaka elfu ya utawala wa Kristo juu ya wanadamu. Mwishoni mwa ile Mileani, wakati Ibilisi na mashetani wake watakaporuhusiwa kwa muda mfupi wajitokeze, roho hao waovu wataiona dunia, si ikiwa katika hali walimoiacha ikiwa, bali ikiwa paradiso ya duniani pote yenye uzuri usioelezeka. Wataiona dunia ikiwa imekaliwa na ule “mkutano mkubwa” wenye uaminifu na mabilioni ya wafu wa kibinadamu watakaokuwa wamefufuliwa ambao Yesu Kristo alifia akiwa dhabihu ya ukombozi. Kufikia mwishoni mwa Mileani ile Yubile ya Kikristo itakuwa imetimiza kusudi layo la kufungua wanadamu kwa ukamili katika matokeo ya dhambi. (Warumi 8:21) Lingekuwa tendo la kiibilisi na lenye aibu sana kama nini mtu ye yote akijaribu kuharibu hali hiyo nzuri sana! Lakini kwa ruhusa ya Mungu Mwenye Nguvu Zote, Ibilisi atafanya jaribio la mwisho la kutenda hivyo, naye atapiga kwa dharuba akiwa na uchungu wenye kasirani. Kwa sababu hiyo imeandikwa hivi kwenye Ufunuo 20:7-10, 14.

      20 “Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake; naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari. Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala. Na yule Shetani, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto.

      21. Baada ya Yubile ya Kikristo kukoma pamoja na Mileani, ni itikio gani lenye kufanywa na wana wa Mungu wa kimbingu litakalokumbusha maneno ya Ayubu 38:7.

      21 Uhuru wa kweli, utakaokuwa umetokezwa na mpango wa Yubile, utaendelea kufurahiwa kila mahali; viumbe wote watakuwa huru na watakuwa wakiheshimu yule ambaye pekee yake ndiye mwenye lile jina Yehova. (Zaburi 83:18) Ndivyo itakavyokuwa Yehova anapoendelea kutekeleza makusudi yake katika ulimwengu wote mzima. Wakati wa kuumbwa kwa dunia, kabla wanadamu hawajawekwa juu yayo, ‘nyota za asubuhi ziliimba pamoja, na wana wote wa Mungu walipiga kelele kwa furaha’ wakishangilia kwa kuona urembo huo. (Ayubu 38:7) Watafanya hivyo hata zaidi kwa kuona dunia ikiongezeka wanaume na wanawake ambao wameonyesha n kuthibitisha wakfu wao wote kabisa na ukamilifu wao kwa Mungu Mwenye Nguvu Zote.

      22. Mwelekeo wetu unapasa kuwa nini, kupatana n himizo linalopatikana kwenye Zaburi 150:1-6?

      22 Mambo yote yakiwa yanafikiriwa kulingana na mng’aro wa kustaajabisha unaoangazwa juu ya Maandiko, sisi hatuna la kufanya isipokuwa kutokeza shangwe ya Yubile kwa hiari pamoja na mbingu na kusema, Haleluya! Hili ndilo himizo kwetu ambalo kwalo kitabu cha Zaburi kinamalizika: “Haleluya. Sifuni Mungu katika patakatifu Pake sifuni Yeye katika anga, ngome Yake. Sifuni Yeye kwa vitendo Vyake vyenye nguvu; sifuni Yeye kwa ukuu Wake unaozidi. Sifuni Yeye kwa mipulizo ya mbiu; sifuni Yeye kwa kinubi na zeze. Sifuni Yeye kwa kigoma na dansi; sifuni Yeye kwa udi na filimbi. Sifuni Yeye kwa matoazi yenye kuvuma; sifuni Yeye kwa matoazi yenye kugongana kwa sauti kubwa. Acheni vyote vipumuavyo vimsifu Bwana. Haleluya.”—Zaburi 150:1-6 Tanakh Bible (1985), Sosaiti ya Amerika ya Uchapishaji wa Kiyahudi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki