-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
12. (a) Katika Zaburi, Yehova aliahidi nini kiunabii kwa habari za Yesu? (b) Ni nini kinachofananishwa na huyo mwanamke kuzaa mwana “ambaye anapaswa kuchunga mataifa yote kwa ufito wa chuma”?
12 Sasa, je! usemi huo unasikika kuwa wenye kuzoeleka? Ndiyo, Yehova aliahidi kiunabii kwa mintarafu ya Yesu: “Wewe utavunja wao kwa fimbo ya kifalme ya chuma, kana kwamba ni chombo cha mfinyanzi wewe utaponda wao vipande vipande.” (Zaburi 2:9, NW) Pia unabii ulitolewa kwa habari yake hivi: “Ufito wa imara yako Yehova atapeleka kutoka Sayuni, akisema: ‘Enda ukishinda katikati ya maadui wako.’” (Zaburi 110:2, NW) Kwa hiyo, uzawa ulioonwa na Yohana unahusu sana Yesu Kristo. La, si kuzaliwa kwa Yesu na bikira huko nyuma kabla ya karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu; wala haungeweza kuwa ukirejezea kuinuliwa kwa Yesu tena kwenye uhai wa roho katika 33 W.K. Zaidi ya hilo, si uhamaji. Badala ya hivyo, ni uzawa wa Ufalme wa Mungu katika 1914 ukiwa uhalisi, Yesu akiwa—sasa katika mbingu kwa karibu karne 20—ameketishwa katika kiti cha ufalme akiwa Mfalme.—Ufunuo 12:10.
13. Ni nini kinachofananishwa na huyo mtoto wa kiume ‘kudakwa mbali hadi kwa Mungu na kwenye kiti cha ufalme chake’?
13 Yehova hangeweza kamwe kuruhusu Shetani ameze mke Wake au mwana Wake aliyezaliwa hivi sasa! Wakati wa uzawa, mtoto huyo wa kiume ‘anadakwa mbali kwa Mungu na hadi kwenye kiti cha ufalme chake.’ Yeye anakuja hivyo chini ya himaya ya Yehova, ambaye ataangalia kikamili huu Ufalme uliozaliwa hivi sasa, chombo Chake cha kutakasia jina Lake takatifu. Wakati ule ule, huyo mwanamke anakimbilia mahali alipotayarishiwa na Mungu jangwani. Tutapata habari zaidi juu ya hilo baadaye! Kwa habari ya Shetani, sasa jukwaa limetayarishwa kwa ajili ya tukio lenye maana kubwa ambalo litafanya isiwezekane kabisa kwake kutisha tena hata kidogo Ufalme ulio katika mbingu. Ni tukio gani hilo?
Vita Katika Mbingu
14. (a) Kama Yohana anavyolieleza, ni tukio gani linalofanya Shetani asiweze tena kutisha Ufalme? (b) Shetani na roho waovu wake wamezuiliwa mahali gani?
14 Yohana anatuambia: “Na vita ikafyatuka katika mbingu: Mikaeli na malaika zake wakapigana na drakoni, na drakoni na malaika zake akapigana lakini hakushinda, wala mahali hapakupatikana kwa ajili yao tena katika mbingu. Hivyo chini yule drakoni mkubwa akavurumishwa, nyoka wa awali kabisa, mmoja ambaye huitwa Ibilisi na Shetani, ambaye anaongoza vibaya dunia nzima yote inayokaliwa; yeye akavurumishwa chini kwenye dunia, na malaika zake wakavurumishwa chini pamoja na yeye.” (Ufunuo 12:7-9, NW) Kwa hiyo likiwa tukio la kidrama katika kuleta siri takatifu ya Mungu kwenye tamati, Shetani anatolewa, anaondoshwa nje ya mbingu, na roho waovu wake wanatupwa chini kwenye dunia pamoja naye. Mmoja ambaye ameongoza vibaya dunia nzima yote inayokaliwa kwa kadiri ya kuwa mungu wayo mwishowe anazuiwa kwenye ujirani wa sayari hii, ambako uasi wake ulianzia awali.—2 Wakorintho 4:3, 4.
15, 16. (a) Mikaeli ni nani, na sisi tunajuaje? (b) Ni kwa nini inafaa kwamba Mikaeli ndiye anayepaswa kuvurumisha Shetani kutoka katika mbingu?
15 Ni nani wanaotimiza ushindi huu mkubwa katika jina la Yehova? Biblia inasema ni Mikaeli na malaika zake. Lakini Mikaeli ni nani? Jina “Mikaeli” lamaanisha “Ni Nani Aliye Kama Mungu?” Kwa hiyo lazima Mikaeli awe anapendezwa na kutetea enzi kuu ya Yehova kwa kuthibitisha kwamba hakuna wa kulinganishwa na Yeye. Katika Yuda 9 yeye anaitwa “Mikaeli, malaika mkuu.” Kwa kupendeza, jina la cheo “malaika mkuu” limetumiwa mahali pengine katika Biblia kuhusiana na mtu mmoja tu: Yesu Kristo.b Paulo husema kwa habari yake hivi: “Bwana mwenyewe atashuka kutoka katika mbingu akiwa na mwito wenye kuamuru pamoja, na sauti ya malaika mkuu na pamoja na tarumbeta ya Mungu.” (1 Wathesalonike 4:16, NW) Jina la cheo “malaika mkuu” lamaanisha “mkuu wa malaika.” Kwa hiyo haishangazi kwamba Ufunuo husema juu ya “Mikaeli na malaika zake.” Mahali pengine ambapo Biblia hutaja malaika wakitii mtumishi mwadilifu wa Mungu hurejezea Yesu. Hivyo, Paulo husema juu ya “ufunuo wa Bwana Yesu Kristo kutoka katika mbingu pamoja na malaika zake wenye nguvu.”—2 Wathesalonike 1:7, NW; ona pia Mathayo 24:30, 31; 25:31.
16 Haya na maandiko mengine yanatuongoza kwenye mkataa usioepukika kwamba Mikaeli si mwingine ila Bwana Yesu Kristo katika cheo chake cha kimbingu. Sasa, katika siku ya Bwana, yeye hasemi tu kwa Shetani tena: “Yehova na akemee wewe.” Kwa kuwa huu ni wakati wa kuhukumu, Yesu, akiwa Mikaeli, huvurumisha chini mwovu huyu Shetani na malaika zake waovu kutoka katika mbingu. (Yuda 9, NW; Ufunuo 1:10) Inafaa kabisa kabisa kwamba yampasa Yeye awe ndiye Mmoja wa kufanya hivyo, kwa kuwa yeye ndiye Mfalme aliyetawazwa hivi sasa. Pia Yesu ndiye ile Mbegu, iliyoahidiwa huko nyuma katika Edeni, ambaye mwishowe kabisa atapondaponda kichwa cha huyo nyoka, hivyo amwondolee mbali kabisa asiwepo kwa wakati wote. (Mwanzo 3:15) Kwa kuondosha Shetani nje ya mbingu, Yesu amechukua hatua kuelekea kupondwapondwa huko kwa mwisho kabisa.
“Mwe na Nderemo, Nyinyi Mbingu”
17, 18. (a) Yohana anaripoti tendo-mwitikio gani kwa habari ya anguko la Shetani kutoka katika mbingu? (b) Ni jipi linaloelekea kuwa chimbuko la sauti kubwa anayosikia Yohana?
17 Yohana anaripoti tendo-mwitikio kwa anguko hili kubwa mno la Shetani: “Na mimi nikasikia sauti kubwa katika mbingu ikisema: ‘Sasa kumetukia wokovu na nguvu na ufalme wa Mungu wetu na mamlaka ya Kristo wake, kwa sababu mshtaki wa ndugu zetu amevurumishwa chini, ambaye huwashtaki mchana na usiku mbele za Mungu wetu! Na wao walishinda yeye kwa sababu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa sababu ya neno la kushuhudu kwao, na wao hawakupenda nafsi zao hata usoni mwa kifo. Kwa minajili hii mwe na nderemo, nyinyi mbingu na nyinyi ambao hukaa ndani yazo!’”—Ufunuo 12:10-12a, NW.
18 Ni ya nani sauti kubwa hiyo ambayo Yohana anasikia? Biblia haisemi. Lakini kilio kama hicho kinachoripotiwa kwenye Ufunuo 11:17 kilikuja kutoka kwa wazee 24 waliofufuliwa wakiwa katika vyeo vyao vya kimbingu, ambako sasa wao wanaweza kuwakilisha watakatifu 144,000. (Ufunuo 11:18) Na kwa kuwa watumishi wapakwa-mafuta wa Mungu wanaonyanyaswa ambao wangali duniani wanasemwa hapa kuwa “ndugu zetu,” taarifa hiyo ingeweza kwa uzuri kutoka kwa chimbuko lile lile. Hapana shaka kwamba hawa waaminifu wanaweza kuunga sauti zao, kwa kuwa ufufuo wao ungefuata upesi baada ya Shetani na magenge yake ya roho waovu kuwa wametupwa nje ya mbingu.
19. (a) Kumalizwa kwa siri takatifu ya Mungu kunafungulia Yesu njia afanye nini? (b) Ni nini kinachoonyeshwa na Shetani kuitwa “mshtaki wa ndugu zetu”?
19 Kumalizwa kwa siri takatifu ya Mungu kunahitaji Yesu achukue mamlaka katika Ufalme wa Yehova. Hivyo njia inafunguliwa kwa ajili ya Mungu kutimiza kusudi lake kubwa la kukomboa aina ya binadamu jaminifu. Yesu analeta wokovu si kwa wanafunzi wake pekee wenye kuhofu Mungu walio duniani sasa bali pia kwa yale mamilioni yasiyohesabika ya wafu ambao wako katika kumbumbu la Mungu. (Luka 21:27, 28) Kumwita Shetani “mshtaki wa ndugu zetu” kunaonyesha kwamba, hata ingawa mashtaka yake dhidi ya Ayubu yalithibitishwa kuwa bandia, yeye alifuliza moja kwa moja kutilia shaka ukamilifu wa watumishi wa kidunia wa Mungu. Kwa wazi, yeye alirudia kwa pindi nyingi lile shtaka la kwamba mtu atatoa vyote alivyo navyo kwa kubadilishana na nafsi yake. Lo! jinsi Shetani ameshindwa kwa kusikitisha!—Ayubu 1:9-11; 2:4, 5.
20. Wakristo waaminifu wamemshindaje Shetani?
20 Wakristo wapakwa-mafuta, wanaohesabiwa kuwa waadilifu “kwa sababu ya damu ya Mwana-Kondoo,” wanaendelea kutoa ushuhuda kwa Mungu na kwa Yesu Kristo ijapokuwa minyanyaso. Kwa zaidi ya miaka 120, hii jamii ya Yohana imekuwa ikielekeza kwenye lile suala kubwa linalohusiana na kukoma kwa majira ya Mataifa katika 1914. (Luka 21:24) Na sasa umati mkubwa unatumikia kishikamanifu kando yao. Hakuna wowote wa hawa ‘wanahofu wale wanaoua mwili lakini hawawezi kuua nafsi,’ kama vile maono ya maisha halisi ya Mashahidi wa Yehova katika wakati wetu yameonyesha tena na tena. Kwa neno la kinywa na kwa mwenendo unaofaa wa Kikristo, wao wameshinda Shetani, wakithibitisha bila ugeugeu kwamba yeye ni mwongo. (Mathayo 10:28; Mithali 27:11; Ufunuo 7:9, NW) Wanapofufuliwa kwenda katika mbingu, ni lazima Wakristo wapakwa-mafuta wawe na furaha kama nini, kwa kuwa Shetani hayuko juu kule ili kushtaki ndugu zao! Kweli kweli, ni wakati wa wingi wote wa malaika, kuitikia kwa shangwe mwito: “Mwe na nderemo, nyinyi mbingu na nyinyi ambao hukaa ndani yazo!”
Ole wa Ushindani!
21. Shetani ameleteaje dunia na bahari ole?
21 Akiudhika kwa sababu ya ole wa tatu, sasa Shetani ananuia kusumbua aina ya binadamu kwa namna yake mwenyewe ya ole. Ni: “Ole kwa ajili ya dunia na kwa ajili ya bahari, kwa sababu Ibilisi amekuja chini kwa nyinyi, akiwa na kasirani kubwa, akijua yeye ana kipindi kifupi cha wakati.” (Ufunuo 12:12b, NW) Kutupwa kwa Shetani nje ya mbingu bila shaka kunamaanisha ole kwa dunia halisi, ambayo inaangamizwa na binadamu wenye ubinafsi walio chini ya udhibiti wake. (Kumbukumbu 32:5) Hata zaidi hivyo, sera ya Shetani ‘tawala au angamiza’ huleta ole kwa dunia ya ufananisho, muundo wa jamii ya kibinadamu, pamoja na bahari ya ufananisho, lile tungamo lenye msukosuko la aina ya binadamu yenyewe. Wakati wa vita viwili vya ulimwengu, hasira-kisasi ya Shetani ilionyeshwa kwa hasira-kisasi ya mataifa yaliyotiishwa chini yake, na milipuko ya hasira kali ya roho waovu kama hiyo inaendelea hadi leo hii—ingawa si kwa muda mrefu zaidi! (Marko 13:7, 8) Lakini hata mbinu za Ibilisi ziwe zenye kuogofya namna gani, hazitaweza kamwe kukaribia tokeo lenye ole ambalo ole wa tatu—tendo kupitia Ufalme wa Mungu—litafanyiza juu ya tengenezo lionekalo la Shetani!
22, 23. (a) Yohana husema ni nini kinachokuwa baada ya drakoni kuwa amevurumishwa chini kwenye dunia? (b) Inawezekanaje kwa drakoni kunyanyasa “mwanamke ambaye alizaa mtoto wa kiume”?
22 Tangu kutupwa nje kwa Shetani kwenye msiba mkubwa, ndugu za Kristo ambao wangali duniani wamevumilia ukatili wa hasira-kisasi yake. Yohana huripoti hivi: “Sasa wakati drakoni alipoona kwamba amevurumishwa chini kwenye dunia, alinyanyasa mwanamke ambaye alizaa mtoto wa kiume. Lakini mabawa mawili ya tai akapewa mwanamke, ili yeye apate kuruka kwenda katika jangwa kwenye mahali pake; huko ndiko yeye analishwa kwa wakati na nyakati na nusu wakati mbali na uso wa nyoka.”—Ufunuo 12:13, 14, NW.
23 Hapa njozi inachukua wazo lililotolewa katika mstari wa 6, ambao unatuambia kwamba baada ya uzawa wa mtoto wake, mwanamke akimbia kwenda katika jangwa, mbali na drakoni. Huenda sisi tukataka kujua jinsi huyo drakoni anavyoweza kunyanyasa mwanamke, kwa kuwa yeye yuko katika mbingu na drakoni huyo sasa ametupwa chini kwenye dunia. Basi, kumbuka kwamba huyo mwanamke ana watoto hapa duniani, mbegu yake. Baadaye katika njozi hii, sisi tunaarifiwa kwamba Shetani anaonyesha hasira-kali yake kuelekea huyo mwanamke kwa kunyanyasa mbegu yake. (Ufunuo 12:17) Yale yanayoipata mbegu ya mwanamke hapa duniani yaweza kuonwa kuwa yakipata huyo mwanamke mwenyewe. (Linga Mathayo 25:40.) Na hesabu yenye kukua ya waandamani wa hiyo mbegu duniani ingepatwa pia na minyanyaso hiyo.
Taifa Jipya
24. Ni nini kilichopata Wanafunzi wa Biblia kilichofanana na kukombolewa kwa Waisraeli kutoka Misri?
24 Vita ya ulimwengu ya kwanza ilipokuwa ikipiganwa, ndugu waaminifu wa Yesu waliendelea na kushuhudu kwao kadiri walivyoweza. Hiyo ilifanywa usoni mwa upinzani ulioongezewa mkazo kutoka Shetani na vibaraka wake wakali. Mwishowe, kushuhudu peupe kwa Wanafunzi wa Biblia karibu kulisimamishwa. (Ufunuo 11:7-10) Hiyo ilikuwa wakati walipopatwa na kituko kama kile cha Waisraeli katika Misri ambao pia walivumilia chini ya uonevu mkubwa. Ikawa ndipo Yehova alipowaleta upesi, kama kwa mabawa ya tai, kwenye usalama katika jangwa la Sinai. (Kutoka 19:1-4) Hali kadhalika, baada ya mnyanyaso mkali wa 1918-19, Yehova alikomboa mashahidi wake, wenye kuwakilisha mwanamke wake, akawaingiza ndani ya hali ya kiroho iliyokuwa salama kwao kama jangwa lilivyokuwa kwa Waisraeli. Hiyo ilikuja ikiwa jibu la sala zao.—Linga Zaburi 55:6-9.
25. (a) Ni nini alichotokeza Yehova katika 1919, kama alivyotokeza Waisraeli wakiwa taifa jangwani? (b) Ni nani wanaojumlika kuwa taifa hili, nao wameletwa ndani ya nini?
25 Huko jangwani, Yehova aliwatokeza Waisraeli wakiwa taifa, akiwaandalia kiroho na kimwili. Hali moja na hiyo, kuanzia 1919, Yehova aliitokeza mbegu ya mwanamke ikiwa taifa la kiroho. Hili lisifikiriwe kuwa ule Ufalme wa Kimesiya ambao umekuwa ukitawala kutoka katika mbingu tangu 1914. Badala ya hivyo, washiriki wa hili taifa jipya ni baki la mashahidi wapakwa-mafuta walio duniani, walioletwa ndani ya hali ya kiroho tukufu katika 1919. Wakiwa sasa wanaandaliwa “kipimo cha ugavi wa chakula chao kwa wakati unaofaa,” hao waliimarishwa kwa ajili ya kazi iliyokuwa mbele.—Luka 12:42, NW; Isaya 66:8.
26. (a) Kile kipindi cha wakati kinachotajwa kwenye Ufunuo 12:6, 14 ni cha urefu gani? (b) Ni nini lililokuwa kusudi la kipindi hicho cha nyakati tatu na nusu, kilianza lini na kilikwisha lini?
26 Pumziko la muda hili la mbegu ya mwanamke wa Mungu lilidumu kwa muda gani? Ufunuo 12:6 husema siku 1,260. Ufunuo 12:14 hukiita kipindi hicho wakati, nyakati, na nusu wakati; kwa maneno mengine, nyakati tatu na nusu. Kwa kweli, semi zote mbili husimamia miaka mitatu na nusu, ikiendelea katika Kizio cha Kaskazini kutoka masika ya 1919 kufika vuli ya 1922. Hiki kilikuwa kipindi cha ponyo lenye kuburudisha na kujipanga tena kitengenezo kwa jamii ya Yohana iliyorudishwa.
27. (a) Kulingana na ripoti ya Yohana, yule drakoni alifanya nini baada ya 1922? (b) Ni nini lililokuwa kusudi la Shetani kutapika nje furiko la mnyanyaso dhidi ya Mashahidi?
27 Yule drakoni hakuchoka! “Na drakoni akatapika maji kama mto kutoka kinywa chake baada ya mwanamke, ili kufanya yeye azamishwe na mto.” (Ufunuo 12:15, NW) Ni nini kinachomaanishwa na “maji kama mto,” au “furiko la maji”? (The New English Bible) Mfalme Daudi wa kale alisema juu ya waovu ambao walimpinga kuwa “mafuriko-bubujiko ya watu wasiofaa kitu [“vijito vya wasio na thamani,” Young]. (Zaburi 18:4, 5, 16, 17, NW) Hali kadhalika, anachofungulia Shetani ni kunyanyaswa na wasio na thamani au “watu wasiofaa kitu.” Baada ya 1922 Shetani alitapika furiko la mnyanyaso dhidi ya Mashahidi. (Mathayo 24:9-13) Hilo lilikuja kutia ndani jeuri ya kimwili, “kutunga matata kwa amri,” vifungo, na hata kunyongwa kwa kutundikwa, kupigwa risasi, na kukatwa kichwa. (Zaburi 94:20, NW) Shetani aliyetwezwa, akiwa amenyimwa ruhusa ya kumfikia moja kwa moja mwanamke wa Mungu, alianza kushambulia kwa hasira-kisasi ile mbegu yake inayobaki duniani na kuwaangamiza, ama moja kwa moja ama kwa kusababisha wapoteze kibali cha Mungu kwa kuvunja ukamilifu wao. Lakini azimio lao lilithibitika kuwa kama lile la Ayubu: “Mpaka mimi niishe mimi sitaondolea mbali ukamilifu wangu kutoka kwangu mwenyewe!”—Ayubu 27:5, NW.
28. Furiko la mnyanyaso lilifikiaje kilele wakati wa Vita ya Ulimwengu 2?
28 Furiko hili la ukatili la mnyanyaso lilifikia kilele wakati wa Vita ya Ulimwengu 2. Katika Ulaya Mashahidi wapatao 12,000 walitiwa katika kambi za mateso za Nazi, na 2,000 hivi wakafa. Chini ya mabwana wa vita waliotawala Italia, Japani, Korea, na Taiwani, Mashahidi waaminifu walipata kutendewa kikatili vivyo hivyo. Hata katika yale mabara yanayoitwa eti ya kidemokrasi, Mashahidi walishambuliwa na vikundi vya Aksio Katoliki, wakapakwa lami na kuvikwa manyoya, na wakafukuzwa kutoka mji. Makusanyiko ya Wakristo yalivunjwa na watoto wa Mashahidi wakafukuzwa shuleni.
29. (a) Yohana anaelezaje habari ya muawana ukiwasili kutoka chimbuko lisilotazamiwa? (b) “Dunia ikaja kusaidia mwanamke” jinsi gani? (c) Yule drakoni alieendelea kufanya nini?
29 Muawana uliwasili kutoka chimbuko lisilotazamiwa: “Lakini dunia ikaja kusaidia mwanamke, na dunia ikafungua kinywa chayo na ikameza kabisa mto ambao yule drakoni alitapika kutoka kinywa chake. Na drakoni akajaa hasira-kisasi kuelekea mwanamke, na akatoka kwenda kufanya vita na wabakio wa mbegu yake, ambao hushika amri za Mungu na wana kazi ya kutoa ushahidi kwa Yesu.” (Ufunuo 12:16, 17, NW) “Dunia”—elementi zilizo ndani ya mfumo wa mambo wa Shetani mwenyewe—ikaanza kumeza ule “mto,” au “furiko.” Wakati wa miaka ya 1940 Mashahidi walianza kupata mfululizo wa maamuzi yenye kupendeleka katika Mahakama Kuu Zaidi Sana ya United States, na kutoka mamlaka zenye kutawala katika mabara fulani, ambayo yalitetea uhuru wa ibada. Mwishowe, Mataifa-Mafungamani yakameza kabisa hiyo kani kubwa gandamizi ya Kinazi-Fashisti, kwa kuauni Mashahidi ambao walikuwa wameteseka chini ya tawala katili za kidikteta. Minyanyaso haikukoma kabisa, kwa kuwa yule drakoni ameendelea mpaka leo hii, naye huendeleza vita dhidi ya wale ambao “wana kazi ya kutoa ushahidi kwa Yesu.” Katika mabara mengi, Mashahidi washikamanifu wangali wamo gerezani, na baadhi yao wangali wanakufa kwa sababu ya ukamilifu wao. Lakini katika mengine ya mabara haya, wakati kwa wakati wenye mamlaka hulegeza mbano wao, na Mashahidi hufurahia kipimo kikubwa zaidi cha uhuru.c Hivyo, katika utimizo wa unabii, dunia huendelea kumeza mto wa mnyanyaso.
30. (a) Dunia imeandaa muawana wa kutosha kwa ajili ya kitu gani kitukie? (b) Ukamilifu wa watu wa Mungu hutokeza nini?
30 Katika njia hii, dunia imeandaa muawana wa kutosha kuruhusu kazi ya Mungu iendelee kwenye mabara 235 hivi na kuzaa wahubiri wa habari njema waaminifu zaidi ya milioni sita. Pamoja na wabakio wa mbegu ya mwanamke, umati mkubwa wa kimataifa wa waumini wapya unashika amri za Mungu kwa habari ya kujitenga na ulimwengu, adili safi, na upendo kwa akina ndugu, na wao wanashuhudia Ufalme wa Kimesiya. Ukamilifu wao unajibu shtaka lenye suto la Shetani, hivi kwamba onyo la kifo linavumishwa kwa ajili ya Shetani na mfumo wake wa mambo.—Mithali 27:11.
-
-
Kupambana na Hayawani Wawili Wakali SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 28
Kupambana na Hayawani Wawili Wakali Sana
Njozi ya 8—Ufunuo 13:1-18
Habari: Hayawani-mwitu mwenye vichwa saba, hayawani-mwitu mwenye vichwa viwili, na mfano wa hayawani-mwitu
Wakati wa utimizo: Kutoka siku ya Nimrodi hadi dhiki kubwa
1, 2. (a) Yohana anasema nini juu ya drakoni? (b) Yohana kwa lugha ya ufananisho, huelezaje habari ya tengenezo lionekanalo linalotumiwa na drakoni?
YULE drakoni mkubwa ametupwa chini kwenye dunia! Funzo letu juu ya Ufunuo limedhihirisha kwamba Nyoka au wafuasi wake roho waovu hawataruhusiwa tena kamwe warudi ndani ya mbingu. Lakini hatujamaliza habari ya “mmoja ambaye huitwa Ibilisi na Shetani, ambaye anaongoza vibaya dunia nzima yote inayokaliwa.” Simulizi linafuata kutambulisha kirefu njia anayotumia Shetani kupiga vita dhidi ya ‘mwanamke na mbegu yake.’ (Ufunuo 12:9, 17, NW) Yohana anasema hivi juu ya drakoni huyo wa kinyoka: “Na huyo akasimama tuli juu ya mchanga wa bahari.” (Ufunuo 13:1a, NW) Kwa hiyo acheni sisi tutue na kuchunguza njia ya utendaji ya huyo drakoni.
2 Mbingu takatifu hazisumbuliwi tena na kuwapo kwa Shetani na roho waovu wake. Hao roho waovu wamekwisha fukuzwa nje ya mbingu na kufungiwa kwenye ujirani wa dunia. Hapana shaka hii ndiyo sababu ya ukuzi mkubwa mno wa mazoea ya uwasiliano na roho nyakati hizi. Nyoka mwenye hila angali anadumisha tengenezo la roho lenye ufisadi. Lakini je! yeye pia anatumia tengenezo linaloonekana ili kuongoza vibaya aina ya binadamu? Yohana hutuambia hivi: “Na mimi nikaona hayawani-mwitu akipanda kutoka bahari, mwenye pembe kumi na vichwa saba, na juu ya pembe zake mataji kumi, lakini juu ya vichwa vyake majina yenye kufuru. Sasa hayawani-mwitu ambaye mimi niliona alikuwa kama chui,
-