Vimefanywa Vitabu vya Kutumiwa
Nchi ndogo yenye milima-milima ya Lesotho ina mipaka yake yote ndani ya Afrika ya Kusini. Wakuu wa Shule katika eneo la Maseru, mji mkuu, walihojiwa na kila mmoja wao akapewa vitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako, Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha na Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Kwa sababu ya hilo, shule moja ilichukua vitabu Ujana 50, na katika shule nyingine kitabu Hadithi za Biblia kilifanywa kitabu rasmi. Madarasa saba, yenye wanafunzi 260, yakaanza kutumia kitabu hicho.
Tunasadiki kwamba wewe na jamaa yenu mtafaidika pia kwa maagizo mazuri yaliyomo katika vichapo hivyo. Kila kimoja kimefungwa kwa jalada gumu; kitabu Ujana na kitabu Jamaa kila kimoja kina kurasa 192. Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia kina kurasa 256, kurasa zake zikiwa na ukubwa sawa na wa gazeti hili, na kimejaa picha kubwa zaidi ya 125, nyingi zikiwa na rangi zenye kupendeza. Pokea vichapo hivyo vitatu kwa Kshs 48,00 (Tshs 80.00) tu.
Tafadhali mnipelekee Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, Kupata Faida Zote za Ujana Wako na Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Ninyi mtanilipia malipo ya kuvipeleka kwa posta. Mimi nimewapelekea Kshs 48.00 (Tshs 80.00).