Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je! Ulimwengu Waweza Kuungana?
    Amkeni!—1993 | Desemba 22
    • muungano yaonekana kuwa mbali kuliko wakati mwingine wowote. Mashindano ya kitaifa na kikabila yatisha kuwapo kwa mwanadamu kuliko wakati mwingine wowote. Hata hivyo, miongoni mwa giza hili la tufeni, mwanga wa tumaini wang’aa pe. Wakati wa kiangazi cha 1993, kikundi cha watu kutoka vikundi vya kikabila vyenye kupigana walionyesha muungano sawa ambao umewaruhusu kushinda ugomvi wa kikabila na kufanya kazi pamoja kwa upendo na umoja.

      Jambo lililo kinyume ni kwamba muungano huo waletwa na jambo hasa linalogawanya ainabinadamu—dini. Gazeti Time liliripoti: “Ukichunguza ukabila wowote wenye ugomvi, au utaifa, kwa kawaida utapata chini yake kiini cha kidini . . . Chuki za kidini huwa za kikatili na zisizo na huruma na zisizo na mpaka.”[20] Juu ya mambo hayohayo, India Today lilisema: “Dini imekuwa jina ambalo uhalifu mwingi mkatili umetendwa. . . . Hiyo hutokeza jeuri kubwa ajabu na ni nguvu yenye kuangamiza sana.”[21]

      Kwelikweli, kwa kawaida dini imekuwa sehemu ya tatizo hilo, si utatuzi. Lakini kikundi hiki kimoja cha kidini kilichotajwa juu—kikundi chenye watu wengi—kimeonyesha kwamba dini yaweza kuunganisha watu, si kugawanya. Ni nani walio katika kikundi hiki? Na kwa nini wamefurahia mafanikio makubwa ajabu ilhali wengine wameshindwa? Ili kupata jibu twakukaribisha usome makala zifuatazo. Kufanya hivyo kwaweza kukupa mtazamo mpya wa wakati ujao wa ainabinadamu.

  • Muungano Unaostaajabisha Ulimwengu
    Amkeni!—1993 | Desemba 22
    • Muungano Unaostaajabisha Ulimwengu

      ULIMWENGU ulishtushwa na kuanguka ghafula kwa Ukomunisti na hivi karibuni zaidi kuongezeka daima kwa jeuri ya kikabila. Hata hivyo, kwa wakati uleule, mamilioni katika Ulaya ya Mashariki wamestaajabishwa na utendaji wa kikundi chenye muungano, na chenye shangwe ambacho kimeshinda chuki za kirangi na utaifa—Mashahidi wa Yehova.

      Mashahidi wa Yehova wamefanikiwa katika kusitawisha ibada yenye muungano hata vita ilipokuwa ikifoka kuwazunguka. Katika 1991, wakati umati wa kimataifa wa Mashahidi 14,684 ulipokutana katika Zagreb, Croatia, polisi mmoja alisema hivi: “Itakuwa vema kuonyesha vyombo vya habari jambo linalotendeka katika uwanja huu, papa hapa, ambapo twaona Waserbia, Wacroati, Waslovenia, Wamontenegro, na wengine wakiketi kando ya mmoja na mwenzake kwa amani.”[1]

      Mwaka huohuo mtangazaji wa habari kwenye mkusanyiko katika Siberia aliona Warusi wakimkumbatia mtu aliyekuwa ametoka kubatizwa wa uzao wa Buryat. Akijua kwamba urafiki wa aina hiyo ni adimu kati ya watu walio tofauti, yeye akasema hivi: “Mliweza kushindaje vizuizi hivyo vya utaifa?”[2]

      Kiangazi hiki mikusanyiko 45 ilifanywa na Mashahidi wa Yehova katika Ulaya Mashariki na Esia, ule wa Moscow na ule wa Kiev wa kimataifa. Wote waliohudhuria mikusanyiko 45 walikuwa zaidi ya 368,000—zaidi ya 112,000 katika ile iliyokuwa Muungano wa Sovieti na karibu 11,000 katika majiji manne ya ile iliyokuwa Yugoslavia.

      Kujapokuwa mapigano katika ujirani wao, karibu Mashahidi 215 waliweza kufika kwenye mkusanyiko katika Belgrade, Serbia, Agosti 19 hadi 22. Ulihudhuriwa na watu 3,241. Ripota mmoja aliandika hivi: “Vikundi karibu na Sarajevo yenyewe viliweza kuhudhuria. Vilikodi basi, na watu 56 wakaja. Hao walitoka Lukavica, Pale, Ilidža, na Vogošća. Watu watano pia walitoka Benkovac. Jambo jingine kubwa pia ni kwamba watu 23 kati ya 174 ambao walibatizwa kwenye mkusanyiko huo walikuwa wametoka katika maeneo hayo yenye mzozo.”[3]

      Katika Moscow na Kiev

      Katika Julai 28, 1993, ukurasa wa mbele wa The New York Times ulikuwa na picha kubwa ya Mashahidi wa Yehova katika Moscow, yenye maelezo haya mafupi: “Kufunguliwa huru kwa dini katika Urusi kulileta waongofu katika Stediamu ya Locomotive ya Moscow kwa ajili ya ubatizo mkubwa wakiwa Mashahidi wa Yehova.”[4]

      Gazeti Times liliripoti hivi: “Washiriki waliokuwa na nyuso zenye machozi wakumbatia wapya wenye kulowa maji. Kinyume na tabia ya kawaida katika Locomotive, hakuna mtu anayevuta sigareti, hakuna anayetukana, hakuna aliyelewa.”[4a] Kwa siku nne Mashahidi kutoka Urusi na kutoka nchi nyingine zaidi ya 30 waliijaza stediamu wakatoshea vizuri, kilele cha hudhurio kikiwa 23,743.

      Mkusanyiko mkubwa hata zaidi wa kimataifa wa Mashahidi wa Yehova ulifanywa katika Kiev, jiji kuu la Ukrainia. Kulikuwa na kilele cha hudhurio la 64,714 walikusanyika katika Stediamu ya Republican, mojawapo iliyo kubwa zaidi katika Ulaya ya Mashariki. Ukurasa wa mbele wa Evening Kiev uliripoti: “Mashahidi wa Yehova . . . wameungana si kwa beji za buluu tu zikiwa zimeandikwa ‘Ufundishaji wa Kimungu’ juu yazo bali kwa imani ya kweli.”[5]

      Jinsi Muungano Unavyopatikana

      Jinsi muungano huo unavyowezekana ulitolewa kielezi na Shahidi mzee-mzee wa Ukrainia katika mkusanyiko wa Kiev. Yeye alielekeza mbinguni na kusema, “Yehova.” Kisha, akinyoosha mikono yake ili afanyize duara, aliinua kidole kimoja. Ujumbe wake ulikuwa dhahiri: ‘Sisi sote tu kitu kimoja, tukiunganika kupitia ufundishaji wa kimungu wa Yehova Mungu.’[6]

      Jambo lenye kupendeza, Encyclopædia Britannica iliripoti juu ya Mashahidi wa Yehova katika ile iliyokuwa Muungano wa Sovieti, ikionyesha sababu ya Mashahidi kuungana. Ilieleza hivi: “Wao wanajua mafundisho yao [ya msingi wa Biblia], ni waongofu wenye bidii na hupanga maisha yao yote kulingana na itikadi zao za kidini.”[7] Kwa hiyo, ilifaa kama nini, kwamba kichwa cha mikusanyiko ya Mashahidi wa Yehova ya kiangazi hiki kilikuwa “Ufundishaji wa Kimungu”!

      Yesu Kristo, aliyetetea ufundishaji wa kimungu, alielekeza kwenye kanuni moja ya maana aliposali hivi kuhusu wafuasi wake: “Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.” Naam, msimamo wa Mashahidi wa Yehova wa kutokuwemo unawaunganisha wao, kama vile Yesu alivyoomba aliposali hivi: “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu.”—Yohana 17:16-21.

      Jambo lililoonwa la mjumbe kutoka Uhispania latoa kielezi cha jinsi kutokuwa sehemu ya ulimwengu kunavyounganisha watu wa Mungu. Katika safari ya kuelekea mkusanyikoni Moscow, yeye alikaa kando ya mtu aliyetoka Afghanistan ambaye alieleza kwamba hata watu wa dini moja walikuwa wanauana katika vita ya wenyewe kwa wenyewe katika nchi hiyo. “Dini yako inaunga mkono chama kipi cha kisiasa?” Kisha yeye akauliza. “Hakuna,” ndugu huyo akajibu.[8] Kwa kuwa Mashahidi wa Yehova hawaungi mkono upande wowote kisiasa, hawahusiki katika vita vya kikabila, ambavyo hugonganisha watu dhidi ya wengine.

      Wajumbe kutoka ile iliyokuwa jamhuri ya Sovieti ya Kazakhstan walijionea wenyewe jinsi vita yaweza kuogopesha. Gari moshi lao lilijikuta katikati ya mifyatuko ya risasi kati ya vikosi vyenye kupigana. Walikuwa na furaha kama nini kufika salama katika Kiev na kufurahia upendo na muungano miongoni mwa vikundi vingi vya kikabila vya mataifa mengi katika stediamu![9]

      Idadi ya wajumbe Wajerumani na Warusi hasa walithamini lile ufundishaji wa kimungu umewafanyia. Wakiwa wanaume wachanga kizazi kimoja kilichopita, walikuwa wakijaribu kuuana wakati wa Vita ya Ulimwengu ya 2. Lakini wakati wa mkusanyiko wa Kiev, waliunganishwa katika ibada ya kweli, kama inavyoonekana kwenye ukurasa wa 7.[10]

      Watazamaji Walistaajabishwa

      Moscow, jiji lenye watu milioni tisa hivi, lilikuwa na fursa ndogo wakati uliopita ya kufaha-miana na Mashahidi wa Yehova.[11] Ni kweli, wengi walikuwa wamesikia juu ya mnyanyaso na kufungwa kwao chini ya Ukomunisti. Pia, kufikia kiangazi cha mwaka huu, makutaniko 18 yalikuwa yameundwa katika Moscow na 13 katika Kiev ili kutumiwa na idadi za watu zinazokua wanaohudhuria mikutano ya Mashahidi. Lakini sasa wenyeji waliona makumi ya maelfu ya wajumbe waliovalia beji mahali pa mkusanyiko na kotekote majijini mwao! Watazamaji wengi walistaajabu.

      Mkuu wa zima-moto wa Moscow alisema: “Mkusanyiko huu wavutia sana. Inapendeza kwamba watu wengi sana wa mataifa mbalimbali wanaweza kuwasiliana kwa lugha moja. Nashangazwa na usafi na utaratibu wa watu wenu. Nimekuwa nikifanya kazi katika stediamu hii kwa miaka 20 na sijapata kuona chochote kama hiki.”[12]

      Mtembeza-watalii mmoja alisema hivi: “Kwa kawaida ninapotembeza kikundi, kugawanyika kwacho huonekana mara tu kinapoondoka kwenye uwanja wa ndege. Sivyo ilivyo na Mashahidi wa Yehova.”[13] Mgeni kwenye mkusanyiko katika Kiev alimaka hivi: “Nyinyi mmeungana kwelikweli. Jinsi ilivyo tofauti kama nini na namna mambo yalivyo nje ya kuta za stediamu!”[14]

      Mkusanyiko wa Moscow ulipoanza Alhamisi, Julai 22, wafanyakazi kadhaa waliokuwa wamesimama juu ya mahali pa ujenzi mkubwa ulio karibu na hapo walionekana wakisimamisha kazi yao kwa muda. Walivutiwa na sauti za watu zaidi ya 23,000 zilizopaazwa katika wimbo. Wangeshangazwa hata zaidi ikiwa wangejua kwamba nyimbo hizo zilikuwa zinaimbwa kwa lugha zaidi ya kumi na mbili. Hata Mashahidi viziwi wasioweza kuimba kwa sauti zao “waliimba” kwa mikono yao katika lugha ya ishara.[15]

      Mahali penye kupendwa pa kukusanyikia jioni palikuwa Red Square iliyo kubwa ya Moscow, nje tu ya kuta za Kremlin. Jioni ya kabla ya mkusanyiko kuanza (hakukuwa na giza hadi baada ya saa nne), mamia ya Mashahidi wengi kutoka rangi mbalimbali walikuwa hapo wakikumbatiana kwa furaha. Ilitukia kwamba ripota mmoja kutoka Moscow Times alisimama hapo na kuwa mwenye udadisi. “Ninyi mwawakilisha nani?” akauliza. Alipoambiwa, alisema hivi: “Sijapata kamwe kuona mchanganyiko wenye furaha wa watu wenye malezi tofauti-tofauti katika Red Square. Kwa kawaida kikundi kama hiki huwa hapa kuandamana au kupinga jambo fulani.”[16]

      Wakazi wa Moscow na vilevile Kiev walivutiwa kwelikweli na maelfu ya wajumbe waliovalia beji wakisalimiana, kukumbatiana kwa msisimko na kujaribu kuwasiliana wao kwa wao. Mwanabiashara mmoja kutoka Iran aliyekuwa akitembelea Kiev alimkaribia Shahidi aliyetoka United States na kusema: “Mna jambo lenye kupendeza ajabu. Nimekuwa nikiwachunguza ninyi watu siku chache zilizopita. Nataka baadhi ya fasihi zenu za Kiingereza nizisome.” Yeye alieleza kwamba ikiwa hangeondoka asubuhi iliyofuata kwenda Iran, angehudhuria mkusanyiko.[17]

      Kotekote katika Moscow na Kiev—hasa kwenye barabara, na sehemu za umma, na katika reli za chini ya ardhi—wajumbe wa mkusanyiko walifikia watu kuwatolea trakti na broshua za Biblia. Kila jioni Mashahidi walionekana wakisimama karibu na Kaburi la Lenin katika Red Square wakizungumza kwa upole na kugawanya trakti. Utoaji huo ulikubaliwa kwa kawaida, mara nyingi kwa tabasamu changamfu. Kama utoaji ulifanywa katika gari-moshi la chini ya ardhi, kwa ujumla mtu alianza kusoma mara hiyo. Halikuwa jambo lisilo la kawaida kuona watu watano au sita ndani ya gari wakisoma trakti za Biblia.[18]

      Baada ya kusoma ujumbe, kwa kawaida abiria wa magari-moshi ya chini ya ardhi walionyesha uthamini. “Hatujapata fursa ya kujifunza mambo kama haya,” akaeleza mtu mwenye umri wa makamo kwa Kiingereza kisicho sanifu. “Asanteni sana.” Katika kisa kingine, kijana mmoja na mama yake walivutiwa na ujumbe hivi kwamba walishuka kutoka kwenye gari-moshi la chini ya ardhi katika kituo cha yule mjumbe wa mkusanyiko ili kuendelea na mazungumzo.[18a]

      Kiev ilijawa na wajumbe Mashahidi zaidi ya 50,000 ambao walikuwa wamekuja kutoka nchi zaidi ya 30, wote ambao walikuwa wamehitaji mahali pa kulala. Walio wengi walikaa katika hoteli, makao ya faragha, na shule, lakini karibu 1,800 walipatiwa mahali katika mashua sita. Mtunza-nyumba mmoja katika mojapo mashua hizo aliwaachia Mashahidi taarifa. Alisema hivi: “Naona ni kama mmetoka kwenye sayari nyingine. Mna uzuri na muungano sana ambao huleta baraka. Yawezekana kwamba ninyi ni wana wa Mungu. Nafikiri juu ya hili nyakati zote.”[19]

      Ilifaa kama nini kwamba Mashahidi wa Yehova waliweza kuwa na mikusanyiko mikubwa na kwamba wakuu wa serikali na watu wengine pia waliweza kuona sifa nzuri hivyo za Kikristo na mwenendo unaomtukuza Mungu! Wakuu wa serikali wa mahali hapo ambao walifanya kazi pamoja na Mashahidi hawakuwa na la kusema ila kuwasifu kwa utendaji wao, uungwana wao, na ushirikiano mzuri pamoja na wenye kuongoza stediamu na idara nyinginezo za jiji.

      “Stediamu haijasafishwa vizuri jinsi hii kwa miaka 13,” akasema ofisa mmoja katika Kiev.[20] Polisi mmoja huko alimaka hivi: “Watu wa pekee kama nini! Ni kama kuwa katika ulimwengu mpya. Siwezi kuelewa ni kwa nini mlinyanyaswa.”[21]

      Mambo Makuu ya Mkusanyiko

      Kwa Mashahidi katika Moscow na Kiev, jambo kuu labda lilikuwa hudhurio la maelfu ya wajumbe kutoka nchi nyinginezo, kutia na washiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova. Ile shangwe ya kuwa pamoja tu, katika ibada yenye muungano iliyo ya amani kukiwa na watu wa mataifa mbalimbali, ilipita ufafanuzi. Msemaji mwenye kumalizia katika Moscow na katika Kiev aliposema kwamba shukrani zetu kuu zamwendea Yehova Mungu, aliyefanya mkusanyiko huo uwezekane, wahudhuriaji walisimama na kupiga makofi kwa dakika kadhaa hadi msemaji alipoendeleza hotuba yake.

      Mambo mengine makuu ya mikusanyiko yalikuwa hotuba zilizotolewa kwa Kiingereza na washiriki wa Baraza Linaloongoza na ripoti fupi-fupi zilizotolewa kila siku na wajumbe kutoka mabara mbalimbali. Utoaji wote huo wa Kiingereza ulitafsiriwa sawia katika lugha nyingi. Katika Kiev, kwa kielelezo, katika lugha 16![22a] Kwa hiyo kwa kuketi katika kata hizo zilizogawiwa kikundi cha lugha mahsusi, wajumbe waliweza kusikia sehemu ya programu hiyo katika lugha yao wenyewe.

      Bado jambo jingine kuu la mkusanyiko lilikuwa kutolewa katika Kirusi na Kiukrania kwa ile broshua mpya Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai? Kitolewaji kilichothaminiwa zaidi kilikuwa kitabu cha Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika Kirusi, ambacho chatumiwa kuwatayarisha Mashahidi wa Yehova watoe kweli za Biblia kwa matokeo. Pia kilichotolewa katika Kirusi kilikuwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, utoaji sahihi wa tarehe za matukio za historia ya Biblia hasa kwa vijana. Tayari na-kala zaidi ya milioni 36 za kitabu hiki zimechapishwa katika lugha zaidi ya 80.[23]

      Ubatizo wa wanafunzi wengi wapya ulikuwa kweli jambo jingine kuu la mkusanyiko. Ukweli wa kwamba wengi waliobatizwa walikuwa vijana haukukosa kuonekana. Katika mkutano wa habari katika Kiev, mleta habari mmoja wa gazeti Osvita aliuliza: “Yenye kutokeza katika mkusanyiko wenu ni idadi kubwa ya vijana. Wao wana fadhili, wapendeza, na wenye tabia nzuri. Mwafanyaje hivyo? Je! mna sera ya pekee kwa vijana? Mimi hufanya kazi na vijana, na nitapendezwa zaidi kujua.”[24]

      Ijapokuwa wakfu kwa Mungu lazima utegemee ujuzi, si hisiamoyo, ubatizo wenyewe bado ni tukio la kihisiamoyo, wenye kugusa moyo. Katika Moscow umati ulisimama na kupiga makofi wakati wataka kubatizwa 1,489 walipoanza kusogea kuelekea vidimbwi vitatu vya ubatizo hadi wote wakabatizwa, zaidi ya saa nzima baadaye.[25]

      Katika Kiev, ambapo kulikuwa na watu 64,000, vidimbwi sita viliwekwa kwa ajili ya ubatizo kwenye mwisho mmoja wa stediamu. Kukiwa na wabatizaji sita au zaidi katika kila kidimbwi, kiasi kinacholingana na idadi ya kutosha kutaniko kilizamishwa kila dakika mbili. Bado, ubatizo uliendelea kwa zaidi ya muda wa saa mbili! Katika “Mapenzi ya Kimungu” Kusanyiko la Kimataifa la 1958 katika New York, 7,136 walibatizwa. Lakini katika Kiev, Mashahidi wa Yehova wapya 7,402 kutoka Ukrainia na jamhuri nyingine zilizokuwa Muungano wa Sovieti waliweka rekodi mpya ya ubatizo mkubwa zaidi wa Kikristo. Hao walikuwa watu wenye kuongea Kirusi peke yake kutoka maeneo ambayo hadi hivi majuzi Mashahidi wa Yehova walikuwa wamepigwa marufuku, kwa miongo mingi!

      Jambo moja kuu la mkusanyiko katika Belgrade lilikuwa kuwapo kwa wajumbe kutoka maeneo ya vita, yenye kuzingiwa. “Mara nyingi wajumbe hawa walionyesha shukrani nyingi kwa pendeleo waliloonyeshwa ili wapate kuja mkusanyikoni,” mfanyakazi wa mkusanyiko akaripoti. “Hata hivyo, ni sisi wengine ambao tuliweza kukutana nao kushuhudia upendo na bidii yao kwa kweli ya Biblia.”[26]

      Katika Mikusanyiko ya “Ufundishaji wa Kimungu,” barua yenye kugusa moyo iliyoandikwa kipupwe kilichopita kutoka Sarajevo ilisomwa. “Hali-joto ni karibu digirii 15 sentigredi chini ya sufuri,” mwandikaji akasema. “Niko pamoja na mke na wana wangu wawili na hatuna umeme wala kuni za kutosha . . . Milio ya bunduki mimina-risasi na milipuko yaweza kusikika. Lakini mioyoni mwetu tuna utulivu na joto kwa sababu ya kweli na kwa sababu ya uhusiano wetu mzuri na Yehova. . . . Tunawasihi mwendelee kusali kwa Yehova ili atusaidie tuendelee bila kuchoka na kuvumilia maogofyo haya yote, tukiwa imara katika imani. Tunasali kwa ajili yenu!”[27]

      Kuna Tofuati Gani?

      Wakiangaliwa kwa kulinganishwa na ukosefu wa muungano miongoni mwa dini za ulimwengu, Mashahidi kwa wazi ni tofauti kabisa. Lakini kwa kweli, wanaweza kufanyiza tofauti gani? Kuhusu mkusanyiko wa Mashahidi miaka iliyopita, tahariri ilisema: “Ni kweli kwamba kusema kwamba kama ulimwengu ulikuwa unaishi kulingana na kanuni [za Biblia] za Mashahidi wa Yehova kungekuwa na mwisho wa umwagaji-damu na chuki, na upendo ungetawala kama mfalme.”[28]

      Hata hivyo, ainabinadamu walio wengi hawafuati kamwe ufundishaji wa kimungu. Katika karne ya kwanza, hata walikataa kumsikiliza Mwana wa Mungu, Yesu Kristo. Kwa hiyo, je, ni kutazamia mengi mno kwamba siku moja tutaona ulimwengu uliounganika? Jambo kama hilo lawezekanaje?

      [Sanduku katika ukurasa wa 12]

      MIKUSANYIKO KATIKA ULAYA YA MASHARIKI NA ESIA

      Nchi Kilele cha Hudhurio Waliobatizwa

      Albania (mkusanyiko 1) 598 39[1]

      Bulgaria (mkusanyiko 1) 704 45[2]

      Jamhuri ya Cheki (mikusanyiko 2) 20,025 620[2]

      Ile Iliyokuwa Muungano wa Sovieti [5]

      Estonia (mikusanyiko 2) 4,732 383[7]

      Urusi (mikusanyiko 3) 32,582 2,454[6]

      Ukrainia (mikusanyiko 2) 69,333 7,797[6]

      Kyrgyzstan (mkusanyiko 1) 5,678 604

      Ile Iliyokuwa Yugoslavia [2]

      Croatia (mkusanyiko 1) 5,003 157

      Makedonia (mkusanyiko 1) 642 27

      Serbia (mkusanyiko 1) 3,241 174

      Slovenia (mkusanyiko 1) 1,961 69

      Hungari (mikusanyiko 5) 22,191 798[2]

      Polandi (mikusanyiko 13) 152,371 4,352

      Romania (mikusanyiko 9) 36,615 2,375[2]

      Slovakia (mikusanyiko 2) 13,215 473[2]

      JUMLA: 368,891 20,367

      [Picha katika ukurasa wa 7]

      Zaidi ya watu 64,000 walikusanyika katika Stediamu ya Republican, Kiev

      [Picha katika ukurasa wa 7]

      Maadui wa Vita ya Ulimwengu ya 2 kutoka Ujerumani na Ukrainia waunganishwa na kweli ya Biblia

      [Picha katika ukurasa wa 8, 9]

      Waabudu zaidi ya 23,000 waliounganika katika Stediamu ya Locomotive, Moscow

      Watu 7,402 walibatizwa katika Kiev, na 1,489 katika Moscow

      Wajumbe wa kigeni walileta tani nyingi za chakula kwa wale walio na uhitaji

      Juu na katikati: Vikundi vingi vya kikabila vilikutana kwa muungano wenye amani Chini: Kutoa ushahidi katika Red Square

      [Picha katika ukurasa wa 10]

      Wajumbe wa mkusanyiko walifurahi kupokea kitabu cha “Hadithi za Biblia,” “Kiongozi cha Shule,” pamoja na broshua mpya katika lugha yao

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki