Wimbo Na. 54
Lazima Tuwe na Imani
Makala Iliyochapishwa
1. Kale Yehova Mungu kasema,
Kupitia manabii.
Leo kupitia Mwana wake,
Anasema: ‘Tubuni!’
(KORASI)
Je, tuna imani kweli?
Ni lazima tuijenge.
Je, ni ya matendo kweli?
Imani iokoayo nafsi.
2. Amri ya Yesu Kristo twatii,
Ufalme tunatangaza.
Kweli iwe wazi tukiwa na
Uhuru wa kusema.
(Korasi)
3. Tuna imani nayo ni ngao;
Kamwe hatutaogopa.
Japo tuna wengi maadui,
Wokovu u karibu.
(KORASI)
Je, tuna imani kweli?
Ni lazima tuijenge.
Je, ni ya matendo kweli?
Imani iokoayo nafsi.
Je, tuna imani kweli?
Ni lazima tuijenge.
Je, ni ya matendo kweli?
Imani iokoayo nafsi.
(Ona pia Rom. 10:10; Efe. 3:12; Ebr. 11:6; 1 Yoh. 5:4.)