Wimbo Na. 65
“Hii Ndiyo Njia”
1. Njia ya amani,
Uliyoipata.
Uliyofundishwa,
Njia ya zamani.
Njia ambayo Yesu
Alifundisha.
Njia ya amani
Njia ya Yehova.
(KORASI)
Njia hii; njia ya uzima
’Sigeuke, wala kupotoka.
Mungu wetu atuagiza:
‘Pita hapa; ’Sitazame nyuma.’
2. Njia ya upendo,
Usikengeuke.
Sauti ya Mungu,
Inatuongoza.
Upendo na wema;
Anatuonyesha.
Njia ya upendo;
Inatuchochea.
(KORASI)
Njia hii; njia ya uzima
’Sigeuke, wala kupotoka.
Mungu wetu atuagiza:
‘Pita hapa; ’Sitazame nyuma.’
3. Njia ya Uzima,
’Sitazame nyuma.
Mungu katupa:
Njia bora zaidi,
Njia ya amani,
Njia ya upendo,
Njia ya uzima.
Asante Yehova.
(KORASI)
Njia hii; njia ya uzima
’Sigeuke, wala kupotoka.
Mungu wetu atuagiza:
‘Pita hapa; ’Sitazame nyuma.’
(Ona pia Zab. 32:8; 139:24; Met. 6:23.)