-
Siku ya Hukumu Ni Nini?Biblia Inafundisha Nini Hasa?
-
-
kwamba wale watakaofufuliwa wataanza upya. Kwa hiyo, vitabu vya kukunjwa vinawakilisha matakwa mengine ya Mungu. Ili waishi milele, wale watakaookoka Har–Magedoni na wale watakaofufuliwa watahitaji kutii amri za Mungu kutia ndani matakwa yoyote mapya ambayo huenda Yehova akafunua katika ile miaka 1,000. Hivyo, watu watahukumiwa kulingana na yale watakayotenda katika Siku ya Hukumu.
Wakati wa Siku ya Hukumu, mabilioni ya watu watapata fursa ya kujifunza kwa mara ya kwanza mapenzi ya Mungu na kuishi kupatana nayo. Hivyo, kutakuwa na kazi kubwa ya kuwaelimisha watu. “Wakaaji wa nchi yenye kuzaa hakika watajifunza uadilifu.” (Isaya 26:9) Hata hivyo, si wote watakaofanya mapenzi ya Mungu. Andiko la Isaya 26:10 linasema: “Hata mwovu akionyeshwa kibali, yeye hatajifunza uadilifu. Atatenda isivyo haki katika nchi ya unyoofu, naye hatauona ukuu wa Yehova.” Waovu hao wataangamizwa milele wakati wa Siku ya Hukumu.—Isaya 65:20.
Mwishoni mwa Siku ya Hukumu, wale wanadamu wengine ‘watakuwa hai’ kikamili kwa sababu watakuwa wakamilifu. (Ufunuo 20:5) Hivyo, katika Siku ya Hukumu, wanadamu watarudishwa katika hali ya ukamilifu waliyokuwa nayo mwanzoni. (1 Wakorintho 15:24-28) Kisha kutakuwa na jaribu la mwisho. Shetani atafunguliwa kutoka katika abiso na kuruhusiwa ajaribu kuwapotosha wanadamu kwa mara ya mwisho. (Ufunuo 20:3, 7-10) Wale watakaompinga wataona utimizo kamili wa ahadi hii ya Biblia: “Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.” (Zaburi 37:29) Ndiyo, Siku ya Hukumu itakuwa baraka kwa wanadamu wote waaminifu!
-
-
1914—Mwaka Muhimu Katika Unabii wa BibliaBiblia Inafundisha Nini Hasa?
-
-
NYONGEZA
1914—Mwaka Muhimu Katika Unabii wa Biblia
MIAKA mingi mapema, wanafunzi wa Biblia walitangaza kwamba mambo muhimu yangetukia mwaka wa 1914. Ni mambo gani hayo, na ni uthibitisho gani unaoonyesha kwamba mwaka wa 1914 ungekuwa mwaka muhimu?
Kulingana na Luka 21:24, Yesu alisema: “Yerusalemu litakanyagwa-kanyagwa na mataifa, mpaka nyakati zilizowekwa za mataifa zitimie.” Yerusalemu lilikuwa jiji kuu la taifa la Kiyahudi—kiti cha utawala cha nasaba ya wafalme wa nyumba ya Mfalme Daudi. (Zaburi 48:1, 2) Hata hivyo, wafalme hao walikuwa tofauti na viongozi wa mataifa mengine. Waliketi juu ya “kiti cha ufalme cha Yehova” wakimwakilisha Mungu mwenyewe. (1 Mambo ya Nyakati 29:23) Kwa hiyo, Yerusalemu liliwakilisha utawala wa Yehova.
Hata hivyo, utawala wa Mungu ulianza ‘kukanyagwa-kanyagwa na mataifa’ jinsi gani na wakati gani? Mwaka wa 607 K.W.K., Yerusalemu liliposhindwa na Wababiloni. “Kiti cha ufalme cha Yehova” hakikuwa na mtu, nayo nasaba ya wafalme wa uzao wa Daudi ilikatishwa. (2 Wafalme 25:1-26) Je, ‘lingekanyagwa-kanyagwa’ milele? Hapana, kwa kuwa unabii wa Ezekieli ulisema hivi kuhusu Sedekia, mfalme wa mwisho wa Yerusalemu: “Kiondoe kilemba, na kulivua taji. . . . Hakika hili halitakuwa la mtu yeyote mpaka atakapokuja yule aliye na haki ya kisheria, nami nitampa yeye.” (Ezekieli 21:26, 27) Kristo Yesu ndiye aliye na “haki ya kisheria” ya taji la Daudi. (Luka 1:32, 33) Kwa hiyo, ‘kukanyaga-kanyaga’ kungeisha wakati ambapo Yesu angekuwa Mfalme.
Tukio hilo kuu lingetokea wakati gani? Yesu alionyesha kwamba Mataifa yangetawala kwa muda fulani uliowekwa. Masimulizi ya Danieli sura ya 4 yanatusaidia kujua urefu wa muda huo. Yanataja ndoto ya kinabii ambayo Mfalme Nebukadneza wa Babiloni aliota. Aliona mti mkubwa uliokatwa. Kisiki chake hakingeweza kukua kwa sababu kilikuwa kimefungwa kwa pingu ya chuma na ya shaba. Malaika alitangaza hivi: “Nyakati saba zipite juu yake.”—Danieli 4:10-16.
Katika Biblia, nyakati nyingine miti huwakilisha utawala. (Ezekieli 17:22-24; 31:2-5) Kwa hiyo, kukatwa kwa mti huo wa mfano kunaonyesha jinsi utawala wa Mungu, uliowakilishwa na wafalme wa Yerusalemu, ungekatishwa. Hata hivyo, maono hayo yaliashiria kwamba ‘kukanyagwa-kanyagwa kwa Yerusalemu’ kungekuwa kwa muda fulani—kipindi cha “nyakati saba.” Kipindi hicho kina urefu gani?
Andiko la Ufunuo 12:6, 14 linaonyesha kwamba nyakati tatu na nusu zinatoshana na “siku 1,260.” Kwa hiyo, “nyakati saba” zingekuwa mara mbili ya kipindi hicho, au siku 2,520. Lakini Mataifa hayakuacha ‘kukanyaga-kanyaga’ utawala wa Mungu siku 2,520 tu baada ya kuanguka kwa Yerusalemu. Basi, inaonekana kwamba unabii huo ulizungumzia muda mrefu zaidi. Kwa kutegemea andiko la Hesabu 14:34 na Ezekieli 4:6, yanayotaja “siku moja kwa mwaka mmoja,” zile “nyakati saba” zingekuwa miaka 2,520.
Miaka hiyo 2,520 ilianza Oktoba 607 K.W.K., Yerusalemu lilipoangushwa na Wababiloni na mfalme wa uzao wa Daudi akaondolewa katika kiti cha ufalme. Kipindi hicho kiliisha Oktoba 1914. Wakati huo, “nyakati zilizowekwa za mataifa” ziliisha, na Yesu Kristo akawekwa kuwa Mfalme wa mbinguni aliyechaguliwa na Mungu.a—Zaburi 2:1-6; Danieli 7:13, 14.
Kama Yesu alivyotabiri, matukio ya pekee ulimwenguni, kama vile, vita, njaa, matetemeko ya nchi, na tauni, yanaonyesha “kuwapo” kwake akiwa Mfalme mbinguni. (Mathayo 24:3-8; Luka 21:11) Matukio hayo yalitoa uthibitisho wa kwamba kwa kweli Ufalme wa mbinguni wa Mungu ulizaliwa mwaka wa 1914 na “siku za mwisho” za mfumo huu mbovu wa mambo zikaanza.—2 Timotheo 3:1-5.
a Tangu Oktoba 607 K.W.K. hadi Oktoba 1 K.W.K. ni miaka 606. Kwa kuwa hakuna mwaka wa sufuri, kuanzia Oktoba 1 K.W.K. hadi Oktoba 1914 W.K. ni miaka 1,914. Tukijumlisha miaka 606 na miaka 1,914, tunapata miaka 2,520. Unaweza kupata habari kuhusu kuanguka kwa Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K., katika makala “Chronology” katika Insight on the Scriptures au “Chronologie” katika Étude Perspicase, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
-
-
Yule Malaika Mkuu Mikaeli Ni Nani?Biblia Inafundisha Nini Hasa?
-
-
NYONGEZA
Yule Malaika Mkuu Mikaeli Ni Nani?
KIUMBE wa roho anayeitwa Mikaeli hatajwi mara nyingi katika Biblia. Hata hivyo, kila mara anatajwa akitenda jambo fulani. Katika kitabu cha Danieli, Mikaeli anapigana na malaika waovu; katika barua ya Yuda, anabishana na Shetani; na katika Ufunuo, anapigana na Ibilisi na malaika wake waovu. Anapoutetea utawala wa Yehova na kupigana na adui za Mungu, Mikaeli anatenda kupatana na maana ya jina lake—“Ni Nani Aliye Kama Mungu?” Lakini Mikaeli ni nani?
Nyakati nyingine, watu huitwa majina mbalimbali. Kwa mfano, mzee wa ukoo Yakobo aliitwa pia Israeli, na mtume Petro aliitwa Simoni. (Mwanzo 49:1, 2; Mathayo 10:2) Vivyo hivyo, Biblia inaonyesha kwamba Mikaeli ni jina lingine la Yesu Kristo, kabla na baada ya maisha yake duniani. Hebu tuone sababu za Kimaandiko zinazotufanya tukate kauli hiyo.
Malaika Mkuu. Neno la Mungu linamwita Mikaeli “yule malaika mkuu.” (Yuda 9) Ona kwamba Mikaeli anaitwa yule malaika
-